Na mwandishi wetu
Simba SC imetangaza kumsajili straika, Aubin Kramo Kouame (pichani) kutoka ASEC Mimosas ya Ivory Coast kwa mkataba wa miaka miwili.
Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa kwenye mitandao rasmi ya Simba, klabu hiyo inaamini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 raia wa Ivory Coast atakuwa msaada mkubwa kwenye kikosi chao kuelekea msimu mpya wa 2023/24 kutokana na uwezo alionao.
Kramo ambaye anatumia mguu wa kushoto ana uwezo wa kucheza nafasi mbalimbali uwanjani ikiwemo winga zote mbili na kucheza nyuma ya mshambuliaji kama namba 10.
Kramo pua katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika msimu uliopita, alifunga mabao manne katika mechi 10 alizocheza na kuisaidia timu hiyo kufika nusu fainali kabla ya kutupwa nje na USM Alger ya Algeria.
Kramo anakuwa mchezaji wa pili kutangazwa kusajiliwa na Simba kuelekea msimu mpya baada ya Leandre Willy Onana raia wa Cameroon aliyetangazwa juzi Jumanne.
Soka Straika wa Ivory Coast atua Simba
Straika wa Ivory Coast atua Simba
Read also
