London, England
Kocha wa Tottenham, Antonio Conte amesema upasuaji wa kwenye kibofu aliofanyiwa umekwenda vizuri na anaendelea vizuri akisubiri kupona kabisa kabla ya kurudi katika kibarua chake.
Conte alihitaji kufanyiwa upasuaji ambao ulifanyika jana Jumatano baada ya kukutwa na uvimbeuchungu hali iliyomfanya kujisikia mgonjwa kabla ya kubainika kwamba alihitaji kufanyiwa upasuaji.
Haijaweza kufahamika mara moja ni lini kocha huyo atakuwa fiti na kurudi kibaruani ingawa inaaminika kwamba hatokuwepo katika mechi ya Jumapili ijayo dhidi ya Man City na hivyo msaidizi wake, Cristian Stellini ndiye atakayebeba majukumu.
“Ahsanteni kwa ujumbe wenu wa upendo, upasuaji niliofanyiwa ulikwenda vizuri na sasa tayari nimeanza kujisikia vizuri,” alisema kocha huyo mwenye umri wa miaka 53 kupitia mtandao wa Instagram.
Tottenham kwa sasa inashika nafasi ya tano katika Ligi Kuu England ikiwa na pointi 36, tofauti ya pointi 14 na Arsenal ambao ndio vinara wa ligi hiyo na mahasimu wao wa jiji la London.
Kimataifa Conte afanyiwa upasuaji, yuko poa
Conte afanyiwa upasuaji, yuko poa
Read also
