Na mwandishi wetu
Kocha wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Miguel Gamondi amemuita katika kikosi chake kipa mzoefu wa Azam FC, Aishi Manula.
Manula ambaye pia amewahi kutamba na timu ya Simba, katika mechi za karibuni ameanza kuonesha ubora wake jambo ambalo linaaminika kumshawishi kocha huyo Mtaliano kumuita katika kikosi hicho.
Wachezaji wengine walioitwa katika timu hiyo itakayoingia kambini Machi 22, 2026 ni Mohamed Mussa (Mashujaa FC), Zubeir Foba (Azam), Yona Amosi (Pamba Jiji), Bakari Msimu (Coastal Union), Twalib Nuru (Azam) na Haji Mnoga (Sallford City-UK).
Wengine ni Elias Lameck (Azam), Nickson Kibabage (Simba), Bakari Mwamnyeto (Yanga), Mohamed Hussein (Yanga) Ibrahim Abdullah Bacca (Yanga), Yusuph Kagoma (Simba), Kelvin Nashon (Pamba Jiji), Mudathir Yahya (Yanga) na Alphonce Mabula (Shamakhi-Azerbaijan).
Katika orodha hiyo pia wamo Novatus Dismas (Goztepe FC-Uturuki), Feisal Salum (Azam), Simon Msuva (Al Taraba-Iraq), Idd Suleiman Nado (Azam), Kelvin John (Aalborg BK-Denmark), Charles M’mombwa (Floriana FC-Malta), Suleiman Mwalimu (Simba), Paul Peter (JTK Tanzania) na Tarryn Allarakhia (Rochdalle AFC-UK).
Kimataifa Gamondi amuita Manula Stars
Gamondi amuita Manula Stars
Read also
