Cairo, Misri
Droo ya timu nane zitakazocheza robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika itafanyika kesho Jumanne Februari 17, 2026 kwenye ofisi za Chama cha Soka Misri (EFA) mjini Cairo, Misri.
Droo hiyo itakayofanyika majira ya mchana itahusisha timu nane zitakazocheza hatua ya robo fainali ya michuano hiyo kwa ajili ya kuzipata timu nne zitakazoumana katika hatua ya nusu fainali.
Tukio hilo litarushwa moja kwa moja kwenye vyombo mbalimbali vya habari vikiwamo vile vya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kuanzia YouTube Channel, CAF TV na mitandao yote ya jamii iliyo chini ya CAF.
Timu zitakazohusika katika droo hiyo ni Esperance ya Tunisia, AS FAR Rabat na RS Berkane za Morocco, Al Hilal ya Sudan, Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini, Stade Malien ya Angola, Al Ahly na Pyramids za Misri,
Kimataifa Droo ligi ya mabingwa Jumanne
Droo ligi ya mabingwa Jumanne
Read also
