Na mwandishi wetu
Serikali imetekeleza ahadi ya zawadi ya fedha kwa timu za vijana chini ya miaka 17 au Serengeti Boys na wasichana chini ya miaka 20 maaufu Tanzanite Queens kutokana na mafanikio waliyoyapata.
Taarifa ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) iliyopatikana leo Jumatano Julai 15, 2026 ilieleza kuwa Serengeti Boys wamepewa zawadi yao ya Sh milioni 500 na Tanzanite Queens wamepewa zawadi ya Sh milioni 50.
Serengeti Boys imefuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika Qatar na timu hiyo pia ilifanikiwa kucheza hatua ya fainali ya Afcon dhidi ya Senegal lakini ilishindwa kubeba taji.
Kwa upande wa Tanzanite Queens wao wamefuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia ambazo zimepangwa kufanyika Septemba mwaka huu nchini Poland.
TFF katika taarifa hiyo waliishukuru serikali kwa kutekeleza ahadi ya zawadi hiyo ambayo wanaamini ilikuwa motisha kwa timu hizo.
Kimataifa Serengeti Boys wapewa Sh milioni 500
Serengeti Boys wapewa Sh milioni 500
Read also
