Manchester, England
Kai Rooney ambaye ni mtoto wa mshambuliaji wa zamani wa Man United, Wayne Rooney ameamua kufuata nyayo za baba yake baada ya kuonekana akiichezea timu hiyo dhidi ya Derby County katika mechi ya Kombe la FA kwa vijana.
Katika mechi hiyo iliyochezwa Ijumaa Januari 23, 2026 kwenye Uwanja wa Old Trafford, Rooney alikuwa jukwaani akimshuhudia mtoto wake akiingia kipindi cha pili kuiwakilisha timu ya vijana chini ya miaka 18 ya Man United.
Man United ilitoka na ushindi wa ushindi wa mabao 2-1 na kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano hiyo ambapo hadi Kai anaingia timu zilikuwa hazijafungana kabla ya mabao ya dakika za nyongeza ya Luca Crolla na Chido kuibeba Man United.
Mara baada ya mechi hiyo, Kai alionekana jukwaani akipiga picha ya selfie na ndugu wa familia yake akiwamo mama yake mzazi Coleen.
Kabla ya mechi Kai ambaye kwa sasa ana miaka 16, pia alitumia mtandao wa Instagram mapema kwa kutupia picha yake ya zamani akiwa mtoto mdogo ikimuonesha sambamba na baba yake kwenye Uwanja wa Old Trafford.
Mwezi uliopita Kai ambaye ni winga aliichezea timu ya vijana chini ya miaka 18 ya Man Unied na kufunga bao lakini haikuwa mechi ya ushindani na ilichezwa kwenye uwanja wa mazoezi wa Carrington.
Kai, alijiunga na akademi ya Man United mwaka 2020 ikiwa ni miaka mitatu baada ya baba yake kuachana na timu hiyo aliyoichezea kwa mafanikio kwa miaka 13 akiifungia mabao 253 katika mechi 559 na kubeba mataji na tuzo kadhaa.
Kimataifa Mtoto wa Rooney aibukia Man Utd
Mtoto wa Rooney aibukia Man Utd
Related posts
Read also
