Na mwandishi wetu
Imeelezwa kuwa bodi ya kusimamia ngumi za kulipwa nchini Uingereza imemfungia bondia Abdallah Pazi ‘Dullah Mbabe’ wa Tanzania kutozichapa kwa muda nchini humo.
Uamuzi wa bodi hiyo umekuja wiki mbili baada ya bondia huyo namba tatu nchini katika uzani wa super middle kupigwa kwa Knock Out (KO) ya raundi ya nne Machi 31, mwaka huu na Callum Simpson bondia namba 36 kidunia na namba tatu Uingereza katika uzani wa super middle.
Aidha, adhabu kama hiyo iliwahi kumkumba bondia Hassan Mwakinyo ambaye ni namba moja nchini kwenye uzani wa super welter mara baada ya pambano lake la Septemba 3 mwaka 2022,l alipochapwa kwa Technical Knock Out (TKO) ya raundi ya nne la Liam Smith.
Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBRC), Chaurembo Palasa ameiambia GreenSports kuwa adhabu hiyo itaisha kwa Mbabe baada ya muda mchache na ilitokana na kupigwa KO nchini humo, hivyo bodi ya huko imemfungia kwa muda asipigane kwao ili kuangalia afya yake.
Ngumi Dullah Mbabe apigwa stop Uingereza
Dullah Mbabe apigwa stop Uingereza
Read also