London, England
Siku chache baada ya klabu ya Barcelona kutangaza faida ya Pauni 86 milioni, mambo si mazuri kwa Man United ambayo imetangaza kupata hasara ya Pauni 115.5 milioni kwa msimu wa 2021/22.
Man United inayotumia Uwanja wa Old Trafford, hata hivyo ina kila sababu ya kujifariji kwa kuwa mapato yao yameanza kuongezeka kwa asilimia 18.
Takwimu zilizotolewa zikihusisha mwisho wa mwaka wa fedha Juni mwaka huu zilionyesha kwamba hasara kwa klabu hiyo pia iliongezeka kwa Pauni 23.3 milioni kulinganisha na hali ilivyokuwa mwaka 2021 wakati deni la klabu pia liliongezeka kutoka Pauni 419.5 milioni kwa mwaka 2021 hadi 514 milioni kwa mwaka huu, hiyo ikiwa ni ongezeko la karibu asilimia 23.
“Mkakati wa klabu yetu ni kushinda kwenye soka na kuwaburudisha mashabiki wetu,” alisema Ofisa Mtendaji Mkuu, Richard Arnold.
Kutokana na usajili mpya uliofanywa msimu uliopita kwa kusajiliwa nyota kadhaa akiwamo Cristiano Ronaldo, Jadon Sancho na Raphael Varane, gharama za mishahara pia ziliongezeka kwa asilimia 19 ambalo ni ongezeko la Pauni 61.6 milioni na hivyo kufikia Pauni 384.2 milioni.
Ongezeko hilo ni kubwa katika historia ya Ligi Kuu England ikiwa imepita rekodi ya msimu uliopita ya jumla ya Pauni 355 milioni iliyofikiwa na majirani zao wa Manchester City.
“Mahesabu yetu katika fedha kwa mwaka 2022 yanaonyesha mambo kuanza kuwa sawa baada ya janga, mashabiki kuanza kurudi kwa nguvu na ushirikiano mzuri wa kibiashara pamoja na ongezeko la uwekezaji kwenye kikosi,” alisema bwana fedha mkuu, Cliff Baty.
Malipo mengine kwa klabu hiyo pia yalitolewa kwa makocha Ole Gunnar Solskjaer aliyetimuliwa Novemba 2021 na Ralf Rangnick pamoja na jopo la wasaidizi wao, klabu hiyo ililazimika kuwalipa jumla ya Pauni 25 milioni. Rangnick alikuwa na mkataba wa miaka miwili wa kazi ya ushauri ambayo hata hivyo hakuifanya na badala yake akawa kocha wa muda wa klabu hiyo.
Kimataifa Man United yapata hasara
Man United yapata hasara
Related posts
Read also