Tuchel - Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz Michezo na Burudani ni zaidi ya ajira Thu, 12 Jun 2025 09:24:50 +0000 en-GB hourly 1 https://wordpress.org/?v=6.9.1 https://www.greensports.co.tz/wp-content/uploads/2021/09/cropped-WhatsApp-Image-2021-09-02-at-13.12.19-1-32x32.jpeg Tuchel - Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz 32 32 Tuchel ataka England wacheze kwa raha zao https://www.greensports.co.tz/2025/06/10/tuchel-ataka-england-wacheze-kwa-raha-zao/ https://www.greensports.co.tz/2025/06/10/tuchel-ataka-england-wacheze-kwa-raha-zao/#respond Tue, 10 Jun 2025 09:59:23 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=13565 London, EnglandKocha wa England, Thomas Tuchel amewataka wachezaji kucheza kama wanapokuwa mazoezini kwa kucheza wakiwa na nyuso za furaha wakati wakijiandaa kuivaa Senegal, leo Jumanne, Juni 10, 2025.Tuchel, alionekana kutofurahia uchezaji wa timu yake licha ya ushindi wa bao 1-0 ambao timu hiyo iliupata dhidi ya Andorra katika mechi ya kufuzu fainali za Kombe la […]

The post Tuchel ataka England wacheze kwa raha zao first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
London, England
Kocha wa England, Thomas Tuchel amewataka wachezaji kucheza kama wanapokuwa mazoezini kwa kucheza wakiwa na nyuso za furaha wakati wakijiandaa kuivaa Senegal, leo Jumanne, Juni 10, 2025.
Tuchel, alionekana kutofurahia uchezaji wa timu yake licha ya ushindi wa bao 1-0 ambao timu hiyo iliupata dhidi ya Andorra katika mechi ya kufuzu fainali za Kombe la Dunia, Jumamosi iliyopita.
Kocha huyo wa zamani wa Chelsea alisema kwamba wachezaji wake walifanya mazoezi tofauti na sasa amewataka kucheza wakiwa huru na kufuata maelekezo.
Tuchel ambaye ni Mjerumani, alianza kazi ya kuinoa England Januari mwaka huu na mechi ya leo ya kirafiki dhidi ya Senegal ni mechi yake ya nne akiwa na timu hiyo.
“Naona tunafanya mazoezi tukiwa na tabasamu lakini hatuchezi mechi tukiwa na tabasamu, kwa hakika tunahitaji kuwa bora zaidi, tunatakiwa kuchangamka katika kundi letu, naona kama tunajitenga uwanjani,” alisema Tuchel.
Tuchel aliongeza kwa kusema kwamba timu hiyo ina mambo mengi mazuri ya kuyafanya nje ya uwanja wa mazoezi ambayo amekuwa akiyaona na kinachotakiwa ni kuhakikisha yote yanahamia uwanjani wakiwa kwenye mechi.
“Jambo la muhimu ni kuweka umakini katika kanuni za mchezo, kupeana maelekezo sahihi miongoni mwa wachezaji na kile tunachokitarajia katika majukumu yao,” alisema Tuchel.

The post Tuchel ataka England wacheze kwa raha zao first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/06/10/tuchel-ataka-england-wacheze-kwa-raha-zao/feed/ 0
Tuchel aanza kibarua England https://www.greensports.co.tz/2025/01/01/tuchel-aanza-kibarua-england/ https://www.greensports.co.tz/2025/01/01/tuchel-aanza-kibarua-england/#respond Wed, 01 Jan 2025 20:22:00 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=12555 London, EnglanedKocha wa zamani wa Chelsea na Bayern Munich, Thomas Tuchel, leo Januari Mosi, 2025 ameanza rasmi kazi yake mpya ya kuinoa timu ya taifa ya England akiwa na mkataba wa miezi 18.Tuchel ambaye Oktoba mwaka jana, alitangazwa rasmi kuchukua nafasi hiyo iliyokuwa ikishikliwa na Gareth Southgate ataiongoza timu hiyo hadi baada ya fanali za […]

The post Tuchel aanza kibarua England first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

London, Englaned
Kocha wa zamani wa Chelsea na Bayern Munich, Thomas Tuchel, leo Januari Mosi, 2025 ameanza rasmi kazi yake mpya ya kuinoa timu ya taifa ya England akiwa na mkataba wa miezi 18.
Tuchel ambaye Oktoba mwaka jana, alitangazwa rasmi kuchukua nafasi hiyo iliyokuwa ikishikliwa na Gareth Southgate ataiongoza timu hiyo hadi baada ya fanali za Kombe la Dunia 2026.
Ikiwa na Southgate, England ilifikia hatua ya fainali ya Kombe la Ulaya 2024 au Euro 2024 nchini Ujerumani lakini licha ya matarajio makubwa timu hiyo ilishindwa kutamba mbele ya Hispania waliobeba taji hilo.
Katika kibarua hicho kipya, Tuchel atakuwa akisaidiwa na Anthony Barry ambaye pia amefanya naye kazi tangu akiwa Chelsea na baadaye Bayern Munich.
England kwenye kusaka tiketi ya kushiriki fainali za Kombe la Dunia 2026 imepangwa kundi moja na timu za Serbia, Latvia, Albania na Andora.
Kati ya timu hizo, Tuchel ambaye pia amewahi kuzinoa timu za Borussia Dortmund ya Ujeruani na PSG ya Ufaransa alisema anaziheshimu Serbia na Albania ambazo alisema zina uwezo wa kuibua mshangao.
Kibarua cha kwanza kwa Tuchel na timu ya England kwenye kufuzu Kombe la Dunia 2026 kitakuwa Machi 21 mwaka huu dhidi ya Albania na siku tatu baadaye dhidi ya Latvia mechi ambazo zitapigwa kwenye dimba la Wembley.
Mara baada ya kuondoka kwa Southgate, England imekuwa chini ya kocha wa muda, Lee Carsey ambaye ana rekodi ya kushinda mechi tano kati ya sita.

The post Tuchel aanza kibarua England first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/01/01/tuchel-aanza-kibarua-england/feed/ 0
Tuchel kuinoa England? https://www.greensports.co.tz/2024/10/16/tuchel-kupewa-majukumu-england/ https://www.greensports.co.tz/2024/10/16/tuchel-kupewa-majukumu-england/#respond Wed, 16 Oct 2024 06:03:11 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=12010 London, EnglandChama cha Soka England, (FA) kinadaiwa kuanza mazungumzo na kocha wa zamani wa klabu za Chelsea na Bayen Munich, Thomas Tuchel ili akabidhiwe jukumu la kuinoa timu ya taifa ya England.Iwapo mpango huo utafanikiwa Tuchel atakuwa kocha wa tatu wa kigeni kuinoa timu hiyo baada ya Sven Goran Eriksson wa Sweden na Fabio Capelo […]

The post Tuchel kuinoa England? first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

London, England
Chama cha Soka England, (FA) kinadaiwa kuanza mazungumzo na kocha wa zamani wa klabu za Chelsea na Bayen Munich, Thomas Tuchel ili akabidhiwe jukumu la kuinoa timu ya taifa ya England.
Iwapo mpango huo utafanikiwa Tuchel atakuwa kocha wa tatu wa kigeni kuinoa timu hiyo baada ya Sven Goran Eriksson wa Sweden na Fabio Capelo wa Italia kuwahi kuinoa timu hiyo.
Kwa sasa timu ya England inanolewa na kocha wa muda, Lee Carsley ambaye amekuwa akiinoa timu hiyo tangu kujiuzulu kwa Gareth Southgate ambaye alidumu kwa miaka minane.
Southgate aliamua kujiuzulu baada ya tmu hiyo kufikia hatua ya fainali ya michuano ya Kombe la Ulaya au Euro 2024 nchini Ujerumani lakini ikashindwa kutamba mbele ya Hispania waliobeba taji.
Taarifa kuhusu mpango huo ilieleza kuwa mazungumzo ya awali na kocha huyo Mjerumani yameshafanyika huku kocha huyo akipewa nafasi kubwa ya kuchukua kibarua hicho.
Tuchel alilazimika kuachana na klabu ya Bayern Mei mwaka huu licha ya kuwa na mwaka mmoja katika mkataba wake lakini aliondoka kwa kuwa mwenendo wa timu haukuwafurahisha mabosi wake.
Kocha huyo ambaye aliiwezesha Chelsea kubeba taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya, mambo yake hayakuwa mazuri Bayern baada ya timu hiyo kushindwa kubeba taji la Ligi Kuu Ujerumani au Bundesliga ikiwa ni mara ya kwanza tangu msimu wa 2011-12.

The post Tuchel kuinoa England? first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/10/16/tuchel-kupewa-majukumu-england/feed/ 0
Tuchel akataa kumrithi Ten Hag https://www.greensports.co.tz/2024/06/10/tuchel-akataa-kumrithi-ten-hag/ https://www.greensports.co.tz/2024/06/10/tuchel-akataa-kumrithi-ten-hag/#respond Mon, 10 Jun 2024 07:30:42 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=11284 Munich, UjerumaniKocha wa zamani wa Bayern Munich na Chelsea, Thomas Tuchel ambaye amekuwa akihusishwa na mipango ya kujiunga na Man United amejiweka kando na kazi hiyo kwa alichodai kuwamba kwa sasa anataka kupumzika.Tuchel, 50, ni kati ya makocha ambao katika siku za karibuni wamekuwa wakipewa nafasi kubwa ya kumrithi Erik Ten Hag ambaye kwa muda […]

The post Tuchel akataa kumrithi Ten Hag first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Munich, Ujerumani
Kocha wa zamani wa Bayern Munich na Chelsea, Thomas Tuchel ambaye amekuwa akihusishwa na mipango ya kujiunga na Man United amejiweka kando na kazi hiyo kwa alichodai kuwamba kwa sasa anataka kupumzika.
Tuchel, 50, ni kati ya makocha ambao katika siku za karibuni wamekuwa wakipewa nafasi kubwa ya kumrithi Erik Ten Hag ambaye kwa muda mrefu sasa hatma yake Man United ipo njia panda.
Kwa sasa vigogo wa Man United wanafanya tathmini ya mwenendo wa timu yao kwa msimu mzima wa 2023-24 na bado hawajatoa hitimisho la nini kitafanyika kuelekea msimu ujao na hata Ten Hag hajawa na uhakika kama ataendelea kuinoa timu hiyo au la.
Wakati hayo yakiendelea zipo habari kwamba Tuchel aliwahi kukutana na mmiliki mwenza wa Man United Sir Jim Ratcliffe nchini Ufaransa ingawa undani wa mazungumzo ya wawili hao haukuwahi kuwekwa wazi.
Kwa upande wake, Tuchel ambaye pia amewahi kuzinoa klabu za PSG na Borussia Dortmund hata hivyo amedai kwamba kwa sasa anataka kupumzika baada ya kuachana na Bayern mwishoni mwa msimu.
Makocha wengine ambao wamekuwa wakitajwa kuchukua nafasi ya Ten Hag Man United ni pamoja na Graham Potter, Thomas Frank pamoja na kocha wa England, Gareth Southgate.

The post Tuchel akataa kumrithi Ten Hag first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/06/10/tuchel-akataa-kumrithi-ten-hag/feed/ 0
Tuchel atangaza, anaondoka Bayern https://www.greensports.co.tz/2024/05/18/tuchel-atangaza-anaondoka-bayern/ https://www.greensports.co.tz/2024/05/18/tuchel-atangaza-anaondoka-bayern/#respond Sat, 18 May 2024 17:06:42 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=11011 Munich, UjerumaniKocha wa Bayern Munich, Thomas Tuchel amethibitisha kuwa ataachana na timu hiyo mara baada ya msimu huu licha ya kuwapo mazungumzo kuhusu uwezekano wa kuendelea na kibarua hicho.Bayern ilitangaza Februari mwaka huu kwamba imekubliana na Tuchel mwenye umri wa miaka 50 kuwa ataachana na timu hiyo akiwa amebakisha mwaka mmoja katika mkataba wake.Tuchel amepitia […]

The post Tuchel atangaza, anaondoka Bayern first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Munich, Ujerumani
Kocha wa Bayern Munich, Thomas Tuchel amethibitisha kuwa ataachana na timu hiyo mara baada ya msimu huu licha ya kuwapo mazungumzo kuhusu uwezekano wa kuendelea na kibarua hicho.
Bayern ilitangaza Februari mwaka huu kwamba imekubliana na Tuchel mwenye umri wa miaka 50 kuwa ataachana na timu hiyo akiwa amebakisha mwaka mmoja katika mkataba wake.
Tuchel amepitia katika msimu mgumu na timu hiyo ambayo imepoteza taji la Ligi Kuu Ujerumani au Bundesliga mbele ya Bayer Leverkusen baada ya kulibeba kwa miaka 11 mfululizo.
Baadhi ya mashabiki wa klabu hiyo walisikika hivi karibuni wakiendesha kampeni kumtaka kocha huyo wa zamani wa Chelsea kuendelea kuinoa timu hiyo lakini Tuchel amesema kwamba hakuna makubaliano yoyote yaliyofikiwa katika suala hilo.
“Makubaliano yetu ya tangu Februari yanabaki kama yalivyo,” alisema Tuchel ambaye alikabidhiwa majukumu ya kuinoa timu hiyo, Machi 2023.
Habari za Tuchel kubaki Bayern zilipata nguvu baada ya kocha huyo kuiwezesha timu hiyo kuitoa Arsenal katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya lakini ilijikuta ikishindwa kutamba mbele ya Real Madrid katika nusu fainali ya ligi hiyo.
Bayern imekuwa ikihaha kusaka mrithi wa Tuchel ambaye katika siku za karibuni zimekuwapo habari kwamba huenda akajiunga na Man United kuchukua nafasi ya Erik ten Hag.
Makocha waliotajwa kuwindwa na Bayern, Xabi Alonso wa Leverkusen na Ralf Rangnick wa timu ya taifa ya Austria wote wameikataa ofa hiyo.
Alonso alikataa ofa hiyo akidai kwamba anaamini bado anahitaji kumalizia kazi aliyoianza akiwa na Leverkusen wakati Rangnick naye alisema anataka kuendelea na kibarua chake Austria.

The post Tuchel atangaza, anaondoka Bayern first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/05/18/tuchel-atangaza-anaondoka-bayern/feed/ 0
Tuchel: Mwamuzi kaisaliti Bayern https://www.greensports.co.tz/2024/05/10/tuchel-mwamuzi-kaisaliti-bayern/ https://www.greensports.co.tz/2024/05/10/tuchel-mwamuzi-kaisaliti-bayern/#respond Fri, 10 May 2024 07:34:11 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=10901 Madrid, HispaniaKocha wa Bayern Munich, Thomas Tuchel amesema kitendo cha mwamuzi kusimamisha mchezo kabla ya timu yake kufunga bao la kusawazisha katika mechi ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid ni mfano wa usaliti.Katika mechi hiyo iliyopigwa Jumatano usiku kwenye dimba la Bernabeu, Bayern walikuwa mbele kwa bao 1-0 hadi […]

The post Tuchel: Mwamuzi kaisaliti Bayern first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Madrid, Hispania
Kocha wa Bayern Munich, Thomas Tuchel amesema kitendo cha mwamuzi kusimamisha mchezo kabla ya timu yake kufunga bao la kusawazisha katika mechi ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid ni mfano wa usaliti.
Katika mechi hiyo iliyopigwa Jumatano usiku kwenye dimba la Bernabeu, Bayern walikuwa mbele kwa bao 1-0 hadi dakika ya 88 baada ya Joselu aliyeingia kipindi cha pili kufunga bao la kwanza na kuongeza la pili katika dakika tatu.
Wakati Bayern ikiwa nyuma kwa mabao 2-1 katika dakika za nyongeza, Matthijs de Ligt aliifungia Bayern bao na kudhani kuwa alisawazisha lakini mshika kibendera tayari aliinua kidendera kuashiria kwamba mfungaji alikuwa ameotea.
Mabeki wa Real Madrid, walisimama kabla ya De Ligt kuujaza mpira wavuni na baadaye marudio ya kwenye televisheni yalionesha kuwa uamuzi wa awali usingekuwa wa mchezaji kuotea na hilo lingeweza kufanyiwa mapitio ya VAR.
Hata hivyo kwa kuwa mchezo ulishasimamishwa, VAR haikuweza kutumiwa jambo ambalo Tuchel amelitaja kuwa ni uamuzi mbaya mno na ambao pia ni kinyume na taratibu.
“Kumekuwa na uamuzi wa hovyo kutoka kwa mshika kibendera na mwamuzi, mwisho wa yote tunaona kama ni kusalitiwa,” alisema Tuchel.

“Mshika kibendera alisema samahani lakini hilo halisaidii kitu, kuinua kibendera katika kipindi kama hicho, mwamuzi aliona tulikuwa tunaupata mpira na kuupiga golini, ni ngumu kukubali lakini hivyo ndivyo mambo yalivyo,” alisema Tuchel.


Baadaye Tuchel alisema kwamba mwamuzi Szymon Marciniak ambaye pia ndiye aliyechezesha mechi ya fainali ya Kombe la Dunia 2022 pia aliomba msamaha lakini kwa Tuchel jambo hilo pia haliwezi kusaidia kitu.
Kwa ushindi huo, Real sasa inasubiri kuumana na Borussia Dortmund katika mechi ya fainali ambayo itapigwa Juni Mosi mwaka huu kwenye dimba la Wembley.

The post Tuchel: Mwamuzi kaisaliti Bayern first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/05/10/tuchel-mwamuzi-kaisaliti-bayern/feed/ 0
Tuchel anaweza kubaki Bayern https://www.greensports.co.tz/2024/05/04/tuchel-anaweza-kubaki-bayern/ https://www.greensports.co.tz/2024/05/04/tuchel-anaweza-kubaki-bayern/#respond Sat, 04 May 2024 18:41:35 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=10833 Munich, UjerumaniKocha wa Bayern Munich ambaye tayari amefikia makubaliano ya kuachana na timu hiyo baada ya msimu huu, Thomas Tuchel amesema pamoja na makubaliano hayo lakini lolote linawezekana.Mapema Feberuari mwaka huu klabu ya Bayern ilitangaza kuwa Tuchel ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 50 ataachana na timu hiyo mwishoni mwa msimu huu baada ya […]

The post Tuchel anaweza kubaki Bayern first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Munich, Ujerumani
Kocha wa Bayern Munich ambaye tayari amefikia makubaliano ya kuachana na timu hiyo baada ya msimu huu, Thomas Tuchel amesema pamoja na makubaliano hayo lakini lolote linawezekana.
Mapema Feberuari mwaka huu klabu ya Bayern ilitangaza kuwa Tuchel ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 50 ataachana na timu hiyo mwishoni mwa msimu huu baada ya makubaliano ya pande zote mbili.
Uamuzi wa Bayern umetokana na mwenendo mbaya wa timu hiyo kwenye Ligi Kuu Ujerumani au Bundesliga ambapo timu hiyo iliyokuwa ikiwania kulibeba taji hilo kwa mara ya 12 mfululizo imeshindwa kufanya hivyo.
Badala yake Bayer Leverkusen imeibuka kuwa tishio kwenye ligi hiyo na tayari imeshatawazwa kuwa bingwa mpya wa taji hilo na kuiacha Bayern na rekodi yake ya kubeba taji la ligi hiyo kwa misimu 11 mfululizo.
Mambo hata hivyo yako tofauti kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya ambapo timu hiyo imefuzu hatua ya nusu fainali na katika mechi ya kwanza dhidi ya Real Madrid imefanikiwa kutoka sare ya mabao 2-2.
Alipoulizwa kuhusu uwezekano wa kuendelea kuwa na timu hiyo Tuchel alisema kwamba hayo ni makubaliano ambayo hayawezi kubadilika lakini hapo hapo akasema kwamba lolote linawezekana.

“Ni kweli kwamba unaweza kubadili mkataba wowote kwa makubaliano, na hapa tuna mkataba ambao tulikubaliana kuumaliza mapema, lakini katika mkataba huo pia lolote linawezekana,” alisema Tuchel.


Taarifa nyingine hata hivyo zinadai kwamba Tuchel anajiandaa kuachana na timu hiyo na hesabu zake zipo katika klabu ya Man United ambayo kocha wake, Erik ten Hag naye anapitia wakati mgumu.

The post Tuchel anaweza kubaki Bayern first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/05/04/tuchel-anaweza-kubaki-bayern/feed/ 0
Tuchel kwa raha zake https://www.greensports.co.tz/2024/04/18/tuchel-kwa-raha-zake/ https://www.greensports.co.tz/2024/04/18/tuchel-kwa-raha-zake/#respond Thu, 18 Apr 2024 06:19:36 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=10650 Munich, UjerumaniKocha wa Bayern Munich anayejiandaa kuachana na timu hiyo, Thomas Tuchel amejawa furaha akijivunia kuiwezesha timu hiyo kufuzu nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kuichapa Arsenal bao 1-0.Ushindi huo unakuwa faraja kubwa kwa kocha huyo anayepitia katika kipindi kigumu cha lawama na shutuma akiwa tayari ametangaziwa rasmi siku ya kuondoka katika timu […]

The post Tuchel kwa raha zake first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Munich, Ujerumani
Kocha wa Bayern Munich anayejiandaa kuachana na timu hiyo, Thomas Tuchel amejawa furaha akijivunia kuiwezesha timu hiyo kufuzu nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kuichapa Arsenal bao 1-0.
Ushindi huo unakuwa faraja kubwa kwa kocha huyo anayepitia katika kipindi kigumu cha lawama na shutuma akiwa tayari ametangaziwa rasmi siku ya kuondoka katika timu hiyo baada ya mabosi Bayern kutoridhishwa na utendaji wake.
Arsenal na Bayern ziliumana jana Jumatano usiku katika mechi ya marudiano ya robo fainali ya ligi hiyo na Bayern kutoka na ushindi wa bao hilo pekee lililofungwa na Joshua Kimmich baada ya sare ya mabao 2-2 katika mechi ya kwanza.
Katika siku za karibuni Tuchel amekuwa akishutumiwa kwa matokeo mabaya ya timu hiyo ikiwamo kupoteza taji la Ligi Kuu Ujerumani au Bundesliga kwa mara ya kwanza baada ya kuweka rekodi ya kulibeba kwa miaka 11 mfululizo.
Mwenendo mbaya wa timu hiyo uliwafanya mabosi wa Bayern kutangaza hivi karibuni uamuzi wa kuachana na kocha huyo mara baada ya msimu huu.
“Hivyo ndivyo ilivyo, nilijitoa kwa yote tangu siku ya kwanza na nimejitoa hadi siku ya mwisho,” alisema Tuchel ambaye sasa anakuwa kocha wa kwanza Mjerumani mwenye rekodi ya kuzifikisha timu za mataifa matatu tofauti nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, alifanya hivyo na Chelsea mwaka 2021 pamoja na PSG mwaka 2020.

“Nusu fainali ni hatua kubwa, timu nne za mwisho, inafurahisha, ni jambo kubwa furaha na faraja, hii ni hatua ya kipekee, tumeifunga moja ya timu kubwa katika Ligi Kuu England, tunasubiri kuona ushindi huu utakuwa na maana gani kwa klabu hii, msimu hata hivyo bado haujafikia mwisho,” alisema Tuchel.


Tuchel aliongeza kuwa wanajivunia kufikia hatua hiyo kubwa na sasa wanasubiri kuona hali itakavyokuwa katika wiki mbili zijazo kwenye mechi ya kwanza ya nusu fainali dhidi ya Real Madrid.
Wakati huo huo, rais wa Bayern, Herbert Hainer baada ya ushindi dhidi ya Arsenal, alimpongeza Tuchel na kusifia kazi yake akisema kwamba mbinu za kocha huyo zilikuwa za kipekee.
Man City nje
Katika mechi nyingine ya nusu fainali mabingwa watetezi Man City ambao msimu uliopita walibeba mataji matatu, ‘treble’ ndoto zao za kubeba taji hilo msimu huu ziliota mbawa baada ya sare ya bao 1-1 na Real Madrid na hatimaye Real Madrid kusonga mbele kupitia penalti.
Katika mechi hiyo ambayo Man City walikuwa nyumbani Itihad, Real Madrid ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Rodrygo katika dakika ya 12 wakati Man City walisawazisha kupitia kwa De Bruyne dakika ya 76.
Katika mechi ya kwanza baina ya timu hizo iliyopigwa kwenye dimba la Barnebeu, mechi iliisha kwa sare ya mabao 3-3 na hivyo matokea ya jumla kuwa sare ya 4-4 na hatimaye Real Madrid kusonga mbele kwa mikwaju ya penalti 4-3 ambapo waliofunga kwa Real Madrd ni Bellingham, Lucas Vazquez, Nacho Fernandez na Antonio Rudiger wakati Luka Modric alikosa. Kwa City waliofunga ni Julian Alvarez, Phil Foden na Ederson Moraes wakati Mateo Kovacic na Bernado Silva walikosa.
Mechi za nusu fainali zitakazopigwa Aprili 30 na Mei mosi ni kama ifuatavyo
Real Madrid v Bayern Munich
PSG v B.Dortmund

The post Tuchel kwa raha zake first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/04/18/tuchel-kwa-raha-zake/feed/ 0
Tuchel aifuta Bayern mbio za ubingwa https://www.greensports.co.tz/2024/03/31/tuchel-aifuta-bayern-mbio-za-ubingwa/ https://www.greensports.co.tz/2024/03/31/tuchel-aifuta-bayern-mbio-za-ubingwa/#respond Sun, 31 Mar 2024 12:09:38 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=10461 Munich, UjerumaniKocha wa Bayern Munich, Thomas Tuchel ametangaza rasmi kuitoa timu yake katika mbio za kuliwania taji la Ligi Kuu Ujerumani au Bundesliga msimu huu baada ya kuchapwa mabao 2-0 na Borussia Dortmund.Bayern ikiwa nyumbani Munich jana Jumamosi ilikumbana na kichapo hicho matokeo ambayo yanaifanya kuwa nyuma ya vinara wa ligi hiyo, Bayern Leverkusen kwa […]

The post Tuchel aifuta Bayern mbio za ubingwa first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Munich, Ujerumani
Kocha wa Bayern Munich, Thomas Tuchel ametangaza rasmi kuitoa timu yake katika mbio za kuliwania taji la Ligi Kuu Ujerumani au Bundesliga msimu huu baada ya kuchapwa mabao 2-0 na Borussia Dortmund.
Bayern ikiwa nyumbani Munich jana Jumamosi ilikumbana na kichapo hicho matokeo ambayo yanaifanya kuwa nyuma ya vinara wa ligi hiyo, Bayern Leverkusen kwa tofauti ya pointi 13.
Leverkusen inayonolewa na kocha Xabi Alonso ambaye ametangaza kuendelea kubaki na timu hiyo licha ya kutakiwa Liverpool, yenyewe ilitoka na ushindi wa mabao 2-1 mbele ya Hoffenheim.
Alipoulizwa kama Bayern imetoka moja kwa moja katika mbio za kusaka taji hilo, Tuchel ambaye anasubiri msimu huu uishe aondoke katika nafasi hiyo alijibu, ‘ndio, hilo ni dhahiri.

“Baada ya mechi ya leo (jana Jumamosi) hakuna sababu tena ya kuhesabu pointi, ni pointi ngapi kwa sasa, hapana, hongera kwa Leverkusen,” alisema Tuchel.


Kwa Dortmund ushindi huo dhidi ya Bayern unakuwa ni wa kwanza baada ya miaka takriban 10 lakini pia umefufua matumaini ya timu hiyo kumaliza ligi ikiwa kwenye top four.
Alonso sasa anahitaji kuiwezesha Leverkusen kushinda mechi tatu kati ya saba zilizobaki kabla ya kumalizika kwa msimu huu ili timu hiyo itangazwe kinara wa taji la Bundesliga na hivyo kufuta ubabe wa Bayern iliyokuwa ikiwania kulibeba taji hilo kwa mwaka wa 12 mfululizo.
Matokeo ya mechi za Bundesliga Jumamosi…
B Leverkusen 2-1 Hoffenheim
Bayern Munich 0-2 B Dortmund
B Mgladbach 0-3 Freiburg
Frankfurt 0-0 Union Berlin
RB Leipzig 0-0 Mainz
Werder Bremen 0-2 Wolfsburg

The post Tuchel aifuta Bayern mbio za ubingwa first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/03/31/tuchel-aifuta-bayern-mbio-za-ubingwa/feed/ 0
Tuchel atajwa Chelsea, Arteta Barca https://www.greensports.co.tz/2024/03/08/tuchel-atajwa-chelsea-arteta-barca/ https://www.greensports.co.tz/2024/03/08/tuchel-atajwa-chelsea-arteta-barca/#respond Fri, 08 Mar 2024 07:03:09 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=10079 Barcelona, HispaniaKlabu za Barcelona na Chelsea zinatajwa kuwa na mkakati wa kubadili makocha kutokana na matokeo yasiyoridhisha ya timu hizo huku Mikel Arteta wa Arsenal na Thomas Tuchel wa Bayern Munich wakianza kutajwa.Kwa upande wa Barca tayari kocha wa timu hiyo, Xavi ametangaza kuondoka baada ya msimu huu na jina lililoibuka na kuwa juu ya […]

The post Tuchel atajwa Chelsea, Arteta Barca first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Barcelona, Hispania
Klabu za Barcelona na Chelsea zinatajwa kuwa na mkakati wa kubadili makocha kutokana na matokeo yasiyoridhisha ya timu hizo huku Mikel Arteta wa Arsenal na Thomas Tuchel wa Bayern Munich wakianza kutajwa.
Kwa upande wa Barca tayari kocha wa timu hiyo, Xavi ametangaza kuondoka baada ya msimu huu na jina lililoibuka na kuwa juu ya mengine ni la kocha wa Arsenal, Arteta.
Chelsea nao wanadaiwa kuwa na mpango huo, kocha Mario Pochettino inadaiwa huenda akatimuliwa wakati wowote baada ya msimu huu na mpango wa timu hiyo ni kumrudisha kocha wao wa zamani Thomas Tuchel.
Tuchel (pichani juu) ambaye ana rekodi ya kuvutia Chelsea baada ya kuiwezesha kubeba taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya kabla ya kutimuliwa, amekuwa na msimu wa hovyo Bayern Munich na tayari klabu hiyo imekubaliana na kocha huyo kuachana baada ya msimu huu.
Chelsea ambayo imefanya uwekezaji mkubwa inaona Pochettino ameshindwa kuendana na uwekezaji huo hivyo mabadiliko ni jambo lisiloepukika na mtu ambaye wamemfikiria kuchukua nafasi hiyo ni Tuchel.
Barca nayo licha ya Xavi kuiwezesha kubeba taji la La Liga msimu uliopita na ingawa timu hiyo inaendelea na mbio hizo msimu huu, kocha huyo amewahi kulalamika juhudi zake kutothaminiwa na mabosi wa klabu hiyo na ndio maana akatangaza kujiweka kando baada ya msumu huu.
Arsenal pia imekuwa na mwenendo mzuri kwenye Ligi Kuu England (EPL) msimu huu na hata msimu uliopita lakini imeendelea kuwa na tatizo la kuyumba mwishoni mwa msimu jambo ambalo huenda likamshawishi Arteta kuwa tayari kwenda Barca kupata changamoto mpya.

The post Tuchel atajwa Chelsea, Arteta Barca first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/03/08/tuchel-atajwa-chelsea-arteta-barca/feed/ 0