Kimataifa - Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz Michezo na Burudani ni zaidi ya ajira Tue, 18 Aug 2026 18:27:22 +0000 en-GB hourly 1 https://wordpress.org/?v=7.0.4 https://www.greensports.co.tz/wp-content/uploads/2021/09/cropped-WhatsApp-Image-2021-09-02-at-13.12.19-1-32x32.jpeg Kimataifa - Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz 32 32 Fifa yalaumiwa kwa usaliti https://www.greensports.co.tz/2026/08/18/fifa-yalaumiwa-kwa-usaliti/ https://www.greensports.co.tz/2026/08/18/fifa-yalaumiwa-kwa-usaliti/#respond Tue, 18 Aug 2026 18:27:21 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14834 Nyon, UswiziShirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) na rais wake, Gianni Infantino wamelaumiwa kwa usaliti kupitia barua ya wazi ya mashirikisho ya soka Ulaya (Uefa), Marekani Kusini (Concacaf) na Asia.Barua hiyo ambayo imesainiwa marais na makatibu wakuu wa mashirikisho hayo matatu, imeeleza kuwa hoja ya hivi karibuni yenye utata inayohusisha Fifa Foward Enterprise (FFE) msingi […]

The post Fifa yalaumiwa kwa usaliti first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
Rais wa Fifa, Gianni Infantino

Nyon, Uswizi
Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) na rais wake, Gianni Infantino wamelaumiwa kwa usaliti kupitia barua ya wazi ya mashirikisho ya soka Ulaya (Uefa), Marekani Kusini (Concacaf) na Asia.
Barua hiyo ambayo imesainiwa marais na makatibu wakuu wa mashirikisho hayo matatu, imeeleza kuwa hoja ya hivi karibuni yenye utata inayohusisha Fifa Foward Enterprise (FFE) msingi wake ni kuhusu hadhi ya soka na hadhi ya waliochaguliwa kuongoza mchezo huo.
Kwa mantiki hiyo FFE ilitaka kuwe na taasisi mpya itakayoundwa kusimamia haki za kibiashara na mauzo ya tiketi katika mashindano yote yanayosimamiwa na Fifa zikiwamo fainali za Kombe la Dunia ambapo asilimia 21 ingeuzwa kwa kampuni binafsi.
Mpango huo ulivunjwa baada ya kuibuka shutuma kutoka mashirikisho ya soka yakiongozwa na Uefa, shirisho ambalo lilitishia kususia mashindano yote ya soka yanayoandaliwa na Fifa.

“Inapotokea uaminifu ukavunjwa kwa kufanyika ulaghai, pale mtu mmoja anapoamua kujiweka juu ya ushirika uliomuamini na kumpa madaraka, hapo uaminifu unakuwa umewekwa kando,” ilieleza sehemu ya barua hiyo.


“Uongozi wa soka si jambo analomiliki mtu, si suala linaloshikiliwa na mtu au kulazimisha kushika madaraka badala yake ni wajibu wa kuzihudumia mamlaka za familia ya soka ambazo zimekuamini,” ilieleza barua hiyo.
Barua hiyo hata hivyo haikumtaja moja kwa moja Rais wa Fifa, Gianni Infantino lakini kilichopo ni kwamba mlengwa mkuu wa hoja hizo ni kiongozi huyo ambaye ni kama vile anatakiwa ajiuzulu.
Barua ya mashirikisho hayo imekuja ikiwa ni siku chache baada ya Fifa kutoa taarifa kwenye vyombo vya habari ikielezea kuhusu inachokiona kuwa ni juhudi za kififisha hadhi ya shirikisho hilo na Infantino.

The post Fifa yalaumiwa kwa usaliti first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/08/18/fifa-yalaumiwa-kwa-usaliti/feed/ 0
Tamasha Yanga Day laingia doa https://www.greensports.co.tz/2026/08/18/tamasha-yanga-day-laingia-doa/ https://www.greensports.co.tz/2026/08/18/tamasha-yanga-day-laingia-doa/#respond Tue, 18 Aug 2026 18:23:37 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14831 Na mwandishi wetuTamasha ya Yanga Day limeingia doa baada ya timu hiyo kuchapwa mabao 2-1 na timu ya Aigles du Congo ya DR Congo katika mechi ya kirafiki iliyochezwa Jumapili Agosti 8, 2026 kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.Katika mchezo huo uliotanguliwa na shamrashamra za kuwatambulisha wachezaji wapya wa Yanga kwa ajili ya msimu […]

The post Tamasha Yanga Day laingia doa first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Tamasha ya Yanga Day limeingia doa baada ya timu hiyo kuchapwa mabao 2-1 na timu ya Aigles du Congo ya DR Congo katika mechi ya kirafiki iliyochezwa Jumapili Agosti 8, 2026 kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Katika mchezo huo uliotanguliwa na shamrashamra za kuwatambulisha wachezaji wapya wa Yanga kwa ajili ya msimu mpya wa 2026-26, Yanga walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na mchezaji wao mpya, Peter Shalulile.
Shalulile alifunga bao hilo katika dakika ya 27 kwa mkwaju wa penalti lakini iliwachukua Aigles dakika 10 kupata bao la kusawazisha lililofungwa na Talasy Tonny na kuzifanya timu ziende mapumziko zikiwa sare.
Aigles waliandika bao la pili katika dakika ya 65, mfungaji kwa mara nyingine akiwa Tony na kuifanya timu yake itoke uwanjani na ushindi.
Mchezo huo umelipa benchi la ufundi la Yanga nafasi nzuri ya kukifanyia tathmini kikosi hicho kipya kabla ya kuanza mbio za kulitetea taji la Ligi Kuu NBC msimu wa 2026-27.
Yanga itaanza kuufungua msimu mpya kwa kuumana na mahasimu wao Simba katika mechi ya Ngao ya Jamii itakayopigwa Jumatano Agosti 12, 2026 kwenye Uwanja wa New Amaan, Zanzibar.

The post Tamasha Yanga Day laingia doa first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/08/18/tamasha-yanga-day-laingia-doa/feed/ 0
Baada ya kumkosa Vini Jr, Arteta ajipanga upya https://www.greensports.co.tz/2026/08/16/baada-ya-kumkosa-vini-jr-arteta-ajipanga-upya/ https://www.greensports.co.tz/2026/08/16/baada-ya-kumkosa-vini-jr-arteta-ajipanga-upya/#respond Sun, 16 Aug 2026 19:43:28 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14828 London, EnglandKocha wa Arsenal, Mikel Arteta amesema ataendelea kusajili wachezaji ili kukifanya kikosi chake kiwe bora baada ya kumkosa Vinicius Junior ‘Vini Jr’ aliyekubali kuongeza mkataba Real Madrid.Baada ya kuwapo uvumi kuhusu Arsenal kumsajili Vini Jr kutoka Real Madrid, hali ilibadilika kwa mchezaji huyo kukubali ofa nono ya miaka sita na sasa Arsenal wameamua kuhamishia […]

The post Baada ya kumkosa Vini Jr, Arteta ajipanga upya first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

London, England
Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta amesema ataendelea kusajili wachezaji ili kukifanya kikosi chake kiwe bora baada ya kumkosa Vinicius Junior ‘Vini Jr’ aliyekubali kuongeza mkataba Real Madrid.
Baada ya kuwapo uvumi kuhusu Arsenal kumsajili Vini Jr kutoka Real Madrid, hali ilibadilika kwa mchezaji huyo kukubali ofa nono ya miaka sita na sasa Arsenal wameamua kuhamishia nguvu zao kwingineko.
Arteta aliulizwa na waandishi wa habari baada ya mechi ya kirafiki dhidi ya Borussia Dortmund Jumapili iliyopita iwapo mashabiki watarajie ongezeko la wachezaji, kocha huyo alisema hicho ndicho wanachotaka kukifanya.

“Ni lazima awe mchezaji sahihi katika soko ili kukifanya kikosi chetu kiwe bora zaidi, tunaliangalia hilo kwa sasa,” alisema Arteta.


Kabla ya Arsenal kufungwa mabao 3-2 na Borussia Dortmund kwenye Uwanja wa Emirates, siku hiyo hiyo walimtambulisha Bruno Guimarães kutoka Newcastle, aliyesajiliwa kwa Pauni 75 milioni.
Habari za ndani hata hivyo zinadai kwamba bado Arteta anataka mchezaji wa hadhi ya juu wa nafasi ya winga ya kushoto, matarajio ya awali yalikuwa kwa Vinicius kwa imani kuwa angekuwa na mchango mkubwa.
Arsenal pia inadaiwa kusaka mchezaji mahiri wa nafasi ya ulinzi wakati kukiwa na habari kwamba William Saliba anatarajia kuwa nje ya uwanja kwa kipindi kirefu akisumbuliwa na matatizo ya mgongo.
Arteta alikiri timu yake kufanya makosa yaliyosababisha wafungwe mabao matatu jambo ambalo alisema wanatakiwa kulifanya kazi ili kuhakikisha wanakuwa bora kwa kuanzia na wachezaji waliopo.

The post Baada ya kumkosa Vini Jr, Arteta ajipanga upya first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/08/16/baada-ya-kumkosa-vini-jr-arteta-ajipanga-upya/feed/ 0
Polisi Kenya watibua sherehe miaka 90 Simba https://www.greensports.co.tz/2026/08/09/polisi-kenya-watibua-sherehe-miaka-90-simba/ https://www.greensports.co.tz/2026/08/09/polisi-kenya-watibua-sherehe-miaka-90-simba/#respond Sun, 09 Aug 2026 19:12:45 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14825 Na mwandishi wetuSherehe za Simba Day zilizoandamana na kumbukumbu ya miaka 90 tangu kuanzishwa kwa klabu ya Simba zimeingia doa baada ya timu hiyo kuchapwa bao 1-0 na Polisi Kenya, mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.Simba na Polisi Kenya zimeumana Jumamosi Agosti 8, 2026, mechi iliyotanguliwa na sherehe hizo sambamba na utambulisho […]

The post Polisi Kenya watibua sherehe miaka 90 Simba first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Sherehe za Simba Day zilizoandamana na kumbukumbu ya miaka 90 tangu kuanzishwa kwa klabu ya Simba zimeingia doa baada ya timu hiyo kuchapwa bao 1-0 na Polisi Kenya, mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Simba na Polisi Kenya zimeumana Jumamosi Agosti 8, 2026, mechi iliyotanguliwa na sherehe hizo sambamba na utambulisho wa wachezaji wa timu hiyo kwa ajili ya msimu mpya wa 2026-27.
Sherehe hizo zilipambwa na burudani ya muziki iliyofanywa na wasanii mbalimbali wakiongozwa na Ali Kiba ambapo mashabiki pia walimshuhudia mnyama Simba akiingizwa kunogesha tukio hilo.
Aliyepeleka kilio Simba alikuwa ni mshambuliaji wa zamani wa Singida Black Stars, Elvis Rupia aliyefunga bao hilo pekee katika dakika ya 90 ya mchezo huo.
Simba licha ya kufungwa bao hilo pekee lakini waliweza kukonga nyoyo za mashabiki waliofurika uwanjani hapo kwa kucheza soka safi na la kuvutia.
Timu hiyo ilitengeneza nafasi kadhaa za kufunga ambazo walishindwa kuzitumia huku wapinzani wao kutoka Kenya wakicheza kwa tahadhari kubwa hadi walipopata bao hilo pekee.
Kabla ya kuanza msimu mpya wa Ligi Kuu NBC, Simba itapata nafasi nyingine ya kupima ubora wa kikosi chake kwa kuumana na mahasimu wao Yanga katika mechi ya Ngao ya Jamii itakayopigwa Agosti 12, 2026 kwenye Uwanja wa New Amaan, Zanzibar.
Sherehe za Simba Day hufanyika kila mwaka tangu kuasisiwa mwaka 2009 na aliyekuwa mwenyekiti wa klabu hiyo, Hassan Dalali na katibu wake, Mwina Kaduguda.
Kwa mwaka huu sherehe za Simba Day zimenogeshwa na tukio la kumbukumbu ya miaka 90 tangu kuanzishwa kwa klabu hiyo mwaka 1936.

The post Polisi Kenya watibua sherehe miaka 90 Simba first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/08/09/polisi-kenya-watibua-sherehe-miaka-90-simba/feed/ 0
Viní Jr aongeza miaka 6 Real Madrid https://www.greensports.co.tz/2026/08/09/vini-jr-aongeza-miaka-6-real-madrid/ https://www.greensports.co.tz/2026/08/09/vini-jr-aongeza-miaka-6-real-madrid/#respond Sun, 09 Aug 2026 19:10:47 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14823 Madrid, HispaniaMshambuliaji Vinícius Junior ‘Vini Jr’ wa Real Madrid hatimaye amevunja ukimya kwa kukubali ofa mpya inayoandamana na mkataba wa miaka sita itakayomfanya awe na klabu hiyo hadi mwaka 2032.Klabu ya Real Madrid imethibitisha hilo Alhamisi Agosti 6, 2026 na hivyo kumaliza uvumi wa siku za hivi karibuni kuhusu hatma ya Vini Jr ambaye pia […]

The post Viní Jr aongeza miaka 6 Real Madrid first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Madrid, Hispania
Mshambuliaji Vinícius Junior ‘Vini Jr’ wa Real Madrid hatimaye amevunja ukimya kwa kukubali ofa mpya inayoandamana na mkataba wa miaka sita itakayomfanya awe na klabu hiyo hadi mwaka 2032.
Klabu ya Real Madrid imethibitisha hilo Alhamisi Agosti 6, 2026 na hivyo kumaliza uvumi wa siku za hivi karibuni kuhusu hatma ya Vini Jr ambaye pia huichezea timu ya taifa ya Brazil.
Mazungumzo baina ya wawakilishi wa Vini na mabosi wa Real Madrid yalikwenda vizuri na inadaiwa kuwa makubaliano yamefikiwa baada ya maslahi ya mchezaji huyo kuboreshwa.
Kabla ya hapo mazungumzo yaliyoanza takriban mwaka mmoja uliopita baina ya pande mbili husika yalikuwa yakikwama na kuibua hofu kuhusu hatma ya Vini Jr na Real Madrid.
Mkataba wa Vini Jr na Real Madrid unafikia ukomo Juni 2027 na kukaibuka habari zilizodai kwamba mchezaji huyo hatoongeza mkataba na tayari alianza kuhusishwa na klabu kadhaa lakini hatimaye amekubali kuongeza mkataba Real Madrid hadi 2032.

“Real Madrid na Vinícius tumekubaliana kuongeza mkataba wa mchezaji wetu, atakuwa katika klabu hii hadi Juni 2032,” ilieleza taarifa ya klabu hiyo.


Vini Jr alijiunga na Real Madrid Julai 2018 wakati huo akiwa na umri wa miaka 18 na katika misimu yake minane na klabu hiyo hadi sasa amebeba mataji mbalimbali.
Awali kulikuwa na habari kuwa Real Madrid ilikuwa tayari kumuuza Vini Jr kama makubaliano yasingefikiwa na moja ya klabu iliyokuwa ikimtaka kwa hali na mali ni Arsenal ya England.
Viní Jr tayari ameshaanza mazoezi katika uwanja wa mazoezi wa Valdebebas unaomilikiwa na Real Madrid baada ya mapumziko.
Mara ya mwisho alionekana akiiwakilisha Brazil kwenye fainali za Kombe la Dunia 2026 kabla ya timu hiyo kutolewa na Norway katika hatua ya robo fainali.

The post Viní Jr aongeza miaka 6 Real Madrid first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/08/09/vini-jr-aongeza-miaka-6-real-madrid/feed/ 0
Hersi apewa miaka mingine minne Yanga https://www.greensports.co.tz/2026/08/09/hersi-apewa-miaka-mingine-minne-yanga/ https://www.greensports.co.tz/2026/08/09/hersi-apewa-miaka-mingine-minne-yanga/#respond Sun, 09 Aug 2026 19:05:14 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14820 Na mwandishi wetuInjinia Hersi Said ataendelea kuiongoza klabu ya Yanga kwa kipindi kingine cha miaka minne baada ya kupita bila kupingwa katika uchaguzi mkuu wa klabu hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam Jumapili, Agosti 2, 2026.Ushindi huo umekuja katika mkutano mkuu wa uchaguzi wa klabu hiyo ambapo kiongozi huyo hakuwa na mpinzani kama ilivyokuwa kwa […]

The post Hersi apewa miaka mingine minne Yanga first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Injinia Hersi Said ataendelea kuiongoza klabu ya Yanga kwa kipindi kingine cha miaka minne baada ya kupita bila kupingwa katika uchaguzi mkuu wa klabu hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam Jumapili, Agosti 2, 2026.
Ushindi huo umekuja katika mkutano mkuu wa uchaguzi wa klabu hiyo ambapo kiongozi huyo hakuwa na mpinzani kama ilivyokuwa kwa makamu wake, Arafat Haji ambao wataendelea kuiongoza klabu hiyo.
Katika nafasi za wajumbe watano wa kamati ya utendaji ya klabu hiyo, walioshinda ni Munir Seleman, Alexander Ngai, Yanga Makaga, Julius Koi na Fahd Afif.
Akizungumza baada ya uchaguzi huo, Hersi aliwataka wanachama wa klabu hiyo kuvunja kambi zilizotokana na makundi ya uchaguzi na kuwa kitu kimoja.
Kwa upande wa wagombea walioshindwa katika uchaguzi huo, Hersi aliwataka kutoyapokea matokeo hayo kwa chuki kwa kuwa wao bado ni wanachama wa Yanga.
Hersi aliwapongeza wagombea ambao wamefanikiwa kushinda katika nafasi za ujumbe wa kamati ya utendaji wakiwamo wawili aliosema kuwa ni wapya na wengine watatu wamebaki.
“Wagombea waliokosa nafasi nao ni washindi licha ya kwamba kura hazikutosha, hawatakiwi kuwa maadui wa klabu yetu badala yake wanapaswa kuwa sehemu ya klabu yao,” alisema Hersi.
Katika mkutano huo, Hersi pia alipata nafasi ya kuwaeleza wanachama mafanikio ya uongozi wake tangu akabidhiwe jukumu hilo takriban miaka minne iliyopita.

The post Hersi apewa miaka mingine minne Yanga first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/08/09/hersi-apewa-miaka-mingine-minne-yanga/feed/ 0
Hispania bingwa Kombe la Dunia 2026 https://www.greensports.co.tz/2026/07/20/hispania-bingwa-kombe-la-dunia-2026/ https://www.greensports.co.tz/2026/07/20/hispania-bingwa-kombe-la-dunia-2026/#respond Sun, 19 Jul 2026 23:05:28 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14816 New York, MarekaniFerran Torres ameibuka shujaa baada ya kufunga bao pekee na kuiwezesha Hispania kutoka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Argentina na kutwaa Kombe la Dunia 2026.Iliwachukua Hispania dakika 106 kupata bao hilo licha ya kuutawala mchezo na kufanya mashambulizi mengi langoni mwa Argentina lakini mashambulizi hayo hayakuweza kuzaa bao kwa dakika 90 […]

The post Hispania bingwa Kombe la Dunia 2026 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

New York, Marekani
Ferran Torres ameibuka shujaa baada ya kufunga bao pekee na kuiwezesha Hispania kutoka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Argentina na kutwaa Kombe la Dunia 2026.
Iliwachukua Hispania dakika 106 kupata bao hilo licha ya kuutawala mchezo na kufanya mashambulizi mengi langoni mwa Argentina lakini mashambulizi hayo hayakuweza kuzaa bao kwa dakika 90 za kawaida.
Kikwazo kikubwa kwa Hispania alikuwa kipa wa Argentina, Emilio Martinez ambaye aliokoa michomo kadhaa ya Hispania hadi kumaliza dakika 90 timu hizo zikiwa hazijafungana ndipo zilipoongezwa dakika 30.
Katika dakika 30 za nyongeza Hispania waliendelea kulisakama lango la Argentina huku Argentina wakitumia muda mwingi kujihami kabla hawajaadhibiwa dakika ya 106 na Torres aliyefunga bao kwa shuti kali la mguu wa kushoto.
Bao hilo lilianzia kwa mpira mrefu uliopigwa na Lamine Yamal na kumkuta Nico William ambaye alimuunganishia Torres pasi ya kichwa na Torres kufumua shuti lililomshinda Martinez.
Baada ya kuingia bao hilo, Argentina waliokuwa wamezidiwa kila idara, waliamka na kuanza mashambulizi wakiongozwa na Lionel Messi na kuibua hali ya hofu kwa Hispania.
Messi ambaye alishindwa kuonesha umahiri wake kwa kipindi kirefu, bao la Hispania ni kama lilimpa nguvu ya kuongoza mashambulizi yaliyozaa kona mbili za haraka kwenye lango la Hispania.
Ukiachana na mashambulizi hayo yaliyopamba moto baada ya Argentina kufungwa, kwa dakika zote 120, timu hiyo ilifanikiwa kupiga mashuti mawili tu ya maana langoni mwa Hispania.
Dalili za Hispania kutoka na ushindi zilianza kuonekana mapema kwa namna walivyotawala mchezo na kulisakama lango la Argentina waliokuwa na kazi ya kujihami huku wakishindwa kutengeneza mashambulizi ya maana.
Kasi ya mashambulizi ya Hispania kwenye lango la Argentina ilianza kuonekana mapema dakika za 4 na 5, Lamine Yamal alionesha umahiri lakini mashuti yake mawili yaliishia mikononi mwa kipa Martinez.
Hispania kwa mara nyingine dakika ya 38 ilifanya shambulizi langoni mwa Argentina lakini shuti la chinichini la mguu wa kushoto lililopigwa na Mikel Oyarzabal lilidakwa na kipa Martinez.
Hispania pia mara kadhaa ilifanya mashambulizi yaliyotokea upande wa kushoto kwa beki Cucurella lakini krosi za beki huyo ziliokolewa au kutoka nje ya lango.
MAmbo yalizidi kuwaharibikia Argentina baada ya nyota wao Enzo Fernandes kulimwa kadi ya pili ya njano kwa kucheza rafu na hivyo kutoka uwanjani akiwaacha wenzake 10 kupambana katika dakika 30 za nyongeza.
Hispania ambao mara ya mwisho walilibeba Kombe la Dunia mwaka 2010 katika fainali zilizofanyika nchini Afrika Kusini, pia ndio mabingwa wa Kombe la Ulaya 2024 au Euro 2024.
Fainali za Kombe la Dunia zilianza kutimua vumbi Juni 11, 2026 katika nchi za Canada, Mexico na kuhitimishwa Jumapili, Julai 19, 2026 nchini Marekani kwa mechi iliyopigwa mjini New York kwenye Uwanja wa New Jersey.

The post Hispania bingwa Kombe la Dunia 2026 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/07/20/hispania-bingwa-kombe-la-dunia-2026/feed/ 0
England yashika nafasi ya tatu https://www.greensports.co.tz/2026/07/19/england-yashika-nafasi-ya-tatu/ https://www.greensports.co.tz/2026/07/19/england-yashika-nafasi-ya-tatu/#respond Sun, 19 Jul 2026 14:53:40 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14810 Miami, MarekaniEngland imeshika nafasi ya tatu kwenye fainali za Kombe la Dunia 2026 ikiilaza Ufaransa mabao 6-4 huku Jude Bellingham akiweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza wa timu hiyo kufunga mabao saba katika moja ya Kombe la Dunia.Timu hizo ziliumana katika mechi ya kusaka mshindi wa tatu Jumamosi Julai 18, 2026 huku mechi ya […]

The post England yashika nafasi ya tatu first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Miami, Marekani
England imeshika nafasi ya tatu kwenye fainali za Kombe la Dunia 2026 ikiilaza Ufaransa mabao 6-4 huku Jude Bellingham akiweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza wa timu hiyo kufunga mabao saba katika moja ya Kombe la Dunia.
Timu hizo ziliumana katika mechi ya kusaka mshindi wa tatu Jumamosi Julai 18, 2026 huku mechi ya fainali kati ya Hispania na Argentina ikisubiriwa kupigwa Jumapili Julai 19, 2026.
Bellingham ambaye pia ni kiungo wa Real Madrid, awali alifungana na nahodha na mshambuliaji wa England, Harry Kane aliyefunga mabao sita katika fainali za Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi.
Rekodi kama hiyo ya mabao sita kabla ya hapo ilikuwa ikishikiliwa na Garry Lineker aliyeifungia England idadi mabao kama hiyo ya mabao kwenye fainali za Kombe la Dunia 1986 nchini Mexico.
Katika mechi dhidi ya Ufaransa, Bellingham, 23, aliingizwa uwanjani dakika ya 79 na kufunga bao lililotokana na shambulizi la kushtukiza.
Dakika 12 kabla ya hapo alikuwa afunge bao kwa mkwaju wa penalti lakini akaamua kumpa nafasi hiyo Bukayo Saka ambaye hakumuangusha, aliitumia vyema penalti hiyo kuipatia England bao.
Saka hata hivyo baada ya mechi alisema kwamba ni Bellingham ndiye aliyemwambia aende akapige mpira huo wa penalti ili apate hat trick (mabao matatu).
Katika mechi hiyo mbali na Bellingham, mabao mengine ya England yalifungwa na Declan Rice dakika ya tatu, Konsa dakika ya 18 na Saka ambaye alifunga dakika za 37, 45 na 87.
Mabao ya Ufaransa yalifungwa na Kylian Mbappe aliyefunga mawili dakika za 48 na 66 wakati mengine mawili yalifungwa na Barcola dakika ya 54 na Dembele dakika ya 90.

The post England yashika nafasi ya tatu first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/07/19/england-yashika-nafasi-ya-tatu/feed/ 0
Trump naye amlaumu Tuchel https://www.greensports.co.tz/2026/07/19/trump-naye-amlaumu-tuchel/ https://www.greensports.co.tz/2026/07/19/trump-naye-amlaumu-tuchel/#respond Sun, 19 Jul 2026 11:32:21 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14805 New York, MarekaniRais wa Marekani, Donald Trump naye ameibuka na kumlaumu kocha wa England, Thomas Tuchel kwa mbinu alizotumia katika mechi ya nusu fainali ya Kombe la Dunia dhidi ya Argentina.Katika hoja yake hiyo, Trump kwa kiasi kikubwa amehoji majukumu ya ulinzi ambayo Thuchel alimpa mshambuliaji wa timu hiyo, Harry Kane hasa katika kipindi cha […]

The post Trump naye amlaumu Tuchel first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

New York, Marekani
Rais wa Marekani, Donald Trump naye ameibuka na kumlaumu kocha wa England, Thomas Tuchel kwa mbinu alizotumia katika mechi ya nusu fainali ya Kombe la Dunia dhidi ya Argentina.
Katika hoja yake hiyo, Trump kwa kiasi kikubwa amehoji majukumu ya ulinzi ambayo Thuchel alimpa mshambuliaji wa timu hiyo, Harry Kane hasa katika kipindi cha pili.
Tuchel ameshutumiwa baada ya England kufungwa mabao 2-1 na Argentina na kutolewa katika hatua ya nusu ya fainali ingawa bado anaungwa mkono na mabosi wa Chama cha Soka England na inaaminika ndiye atakayeiongoza timu hiyo kwenye fainali za Kombe la Ulaya 2028 au Euro 2028.
England walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Anthony Gordon dakika ya 55 na baada ya hapo Tuchel alijaza mabeki sita nyuma lakini Argentina walimzidi ujanja na kufunga mabao mawili dakika za 85 na 92 (90+2).
Akitoa hoja yake dhidi ya mbinu za Tuchel, Trump awali alianza kwa kumsifia Kane na kukumbushia walivyowahi kucheza naye golfu kwenye ufukwe wa West Palm takriban miezi 18 iliyopita.

“England mna mchezaji mzuri, mchezaji ambaye niliwahi kucheza naye golfu, mnamjua huyo? ni Harry ambaye amekuwa mchezaji mahiri, nafikiri walikosea kumfanya awe mchezaji wa ulinzi,” alisema Trump.

Trump alifafanua akisema kilichotokea ni kwamba England walipata bao la kuongoza na baada ya hapo walichofanya ni kumchukua mchezaji wao bora na kumuweka katika eneo la ulinzi.

The post Trump naye amlaumu Tuchel first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/07/19/trump-naye-amlaumu-tuchel/feed/ 0
Tuchel ajitetea baada ya England kutolewa https://www.greensports.co.tz/2026/07/18/tuchel-ajitetea-baada-ya-england-kutolewa/ https://www.greensports.co.tz/2026/07/18/tuchel-ajitetea-baada-ya-england-kutolewa/#respond Sat, 18 Jul 2026 19:34:22 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14802 Miami, MarekaniKocha mkuu wa timu ya taifa ya England, Thomas Tuchel ametetea maamuzi yake katika mechi ya nusu fainali ya Kombe la Dunia 2026 dhidi ya Argentina licha ya timu hiyo kushindwa.Akizungumza kabla ya mechi ya kusaka mshindi wa tatu dhidi ya Ufaransa, kocha huyo Mjerumani alisema kama anahitajika mtu wa kulaumiwa basi yeye yuko […]

The post Tuchel ajitetea baada ya England kutolewa first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Miami, Marekani
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya England, Thomas Tuchel ametetea maamuzi yake katika mechi ya nusu fainali ya Kombe la Dunia 2026 dhidi ya Argentina licha ya timu hiyo kushindwa.
Akizungumza kabla ya mechi ya kusaka mshindi wa tatu dhidi ya Ufaransa, kocha huyo Mjerumani alisema kama anahitajika mtu wa kulaumiwa basi yeye yuko tayari kubeba zigo la lawama.
Tuchel hata hivyo alisema hana cha kujutia na kuongeza kuwa timu yake ndiyo iliyoumizwa zaidi kuliko yeyote na kwamba kilichotokea ni jeraha ambalo wanalazimika kulibeba.
Katika mechi hiyo, England walikuwa wakipambana kuweka rekodi ya kufikia hatua ya fainali ya Kombe la Dunia mara ya kwanza tangu kufanya hivyo mara ya mwisho mwaka 1966, miaka 60 iliyopita.
Kilichotokea katika mechi hiyo kiliiumiza mno England kwani baada ya kuongoza kwa bao 1-0 mambo yalibadilika mwishoni na kujikuta wakilala kwa mabao 2-1 huku wakipigwa presha na Messi.
Mabao ya Argentina yaliyopatikana dakika za 85 na 90 (+2) yaliwaumiza mno mashabiki wa England huku baadhi ya wachambuzi wakilaumu maamuzi kadhaa ya Tuchel ikiwamo kujihami zaidi badala ya kushambulia.
Alipoulizwa ni kwa nini timu yake ilicheza kwa kujihami zaidi Tuchel alisema hicho ndicho kilichotakiwa kufanywa kwa namna Argentina walivyokuwa na hajutii uamuzi wake katika hilo.

“Nilichukua maamuzi mengi, niliamini fikra zangu, uzoefu wangu, niliamini katika upambanaji wangu na nilichukua maamuzi kwa lengo la kuisaidia timu kupata matokeo lakini hatukupata matokeo,” alisema Tuchel.


England inacheza mechi ya kusaka mshindi wa tatu dhidi ya Ufaransa, mechi itakayopigwa Jumamosi Julai 18, 2026 wakati mechi ya fainali kati ya Argentina na Hispania itapigwa Jumapili Julai 19, 2026.

The post Tuchel ajitetea baada ya England kutolewa first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/07/18/tuchel-ajitetea-baada-ya-england-kutolewa/feed/ 0