Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz Michezo na Burudani ni zaidi ya ajira Tue, 21 Apr 2026 18:20:29 +0000 en-GB hourly 1 https://wordpress.org/?v=6.9.4 https://www.greensports.co.tz/wp-content/uploads/2021/09/cropped-WhatsApp-Image-2021-09-02-at-13.12.19-1-32x32.jpeg Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz 32 32 Simba yaicharaza Namungo 3-1 https://www.greensports.co.tz/2026/04/21/simba-yaicharaza-namungo-3-1/ https://www.greensports.co.tz/2026/04/21/simba-yaicharaza-namungo-3-1/#respond Tue, 21 Apr 2026 18:16:15 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14548 Na mwandishi wetuSimba imeendelea kujiimarisha katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu NBC kwa kuichapa Namungo FC mabao 3-1 katika mechi ilyochezwa Jumapili, Aptili 19, 2026 kwenye Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa, Lindi.Kwa ushindi huo, Simba sasa imefikisha point 42 katika mechi 19 ikiwa imetanguliwa na Yanga inayoshika usukani ikiwa na pointi 47 katika […]

The post Simba yaicharaza Namungo 3-1 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Simba imeendelea kujiimarisha katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu NBC kwa kuichapa Namungo FC mabao 3-1 katika mechi ilyochezwa Jumapili, Aptili 19, 2026 kwenye Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa, Lindi.
Kwa ushindi huo, Simba sasa imefikisha point 42 katika mechi 19 ikiwa imetanguliwa na Yanga inayoshika usukani ikiwa na pointi 47 katika mechi 19 kama ilivyo Simba.
Mashabiki wa Simba walianza kushangilia bao la kwanza kwa timu yao katika dakika ya 12 mfungaji akiwa ni Libasse Gueye akimalizia pasi ya Anthony Mligo.
Simba walipambana na kuongeza bao la pili dakika 12 baadaye, bao lililofungwa na Anicet Oura akiitumia vizuri pasi ya Yusuph Kagoma.
Namungo walipambana na kufanikiwa kuzichana nyavu za Simba katika dakika ya 33 kwa bao la Heritier Makambo alilofunga kwa mkwaju wa penalti iliyotolewa baada ya Kagoma kuunawa mpira katika eneo la hatari.
Simba hawakuridhika na mabao hayo mawili na katika dakika ya 74 walifunga bao la tatu mfungaji akiwa ni Ellie Mpanzu, bao lililofuta matumaini ya Namungo kupata bao la kusawazisha.

The post Simba yaicharaza Namungo 3-1 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/04/21/simba-yaicharaza-namungo-3-1/feed/ 0
Soka la Arsenal lamkosha Pep https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/soka-la-arsenal-lamkosha-pep/ https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/soka-la-arsenal-lamkosha-pep/#respond Sat, 18 Apr 2026 20:03:37 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14546 Manchester, EnglandKocha wa Man City, Pep Guardiola amesema anafurahia kuiangalia timu ya Arsenal ikicheza kwa kuwa anajifunza mambo mengi kupitia timu hiyo kwa namna tofauti.Aresenal au Gunners wako mstari wa mbele katika mbio za kusaka mataji mawili ya Ligi Kuu England pamoja na Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu.Katika ligi kuu timu hiyo inashika usukani […]

The post Soka la Arsenal lamkosha Pep first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Manchester, England
Kocha wa Man City, Pep Guardiola amesema anafurahia kuiangalia timu ya Arsenal ikicheza kwa kuwa anajifunza mambo mengi kupitia timu hiyo kwa namna tofauti.
Aresenal au Gunners wako mstari wa mbele katika mbio za kusaka mataji mawili ya Ligi Kuu England pamoja na Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu.
Katika ligi kuu timu hiyo inashika usukani kwa tofauti ya pointi sita na katika Ligi ya Mabingwa wanasubiri kuumana na Atletico Madrid katika hatua ya nusu fainali.
Pamoja na mafanikio hayo, staili ya uchezaji wa timu hiyo chini ya kocha Mikel Arteta imeendelea kupingwa kila kona kwa kinachotajwa kuwa asilimia 37 ya mabao yao 62 ya kwenye ligi yamefungwa kwa ‘set pieces’.
Arsenal chini ya Arteta ambaye amewahi kufanya kazi na Pep,, Jumapili Aprili 19, 2026 itasafiri hadi Manchester kuumana na Man City, timu ambayo inashika nafasi ya pili kwenye ligi hivyo ushindi ndio kitu pekee wanachohitaji Arsenal.
Ushindi utaiweka Arsenal katika mazingira mazuri ya kubeba taji la ligi hiyo msimu huu wa 2025-26 baada ya kulikosa kwa takriban miaka 22 sasa.
Kwa upande wake Pep alipoulizwa kama anafurahia kuwaona Arsenal wakicheza alijibu ndio na kufafanua kwamba anajifunza mambo mengi katika namna tofauti na anafahamu kwamba timu hiyo ina kitu cha kipekee.

“Watu wanachotaka ni kushinda na tutapambana, jambo la msingi hasa ni kwamba hatutapambana dhidi ya Arsenal iliyokosa taji kwa miaka 22, wana kitu kinachowafanya wawe wa kipekee, hilo ninalifahamu,” alisema Pep.


Pep alisisitiza kwamba wana wajibu wa kuwa makini na aina yao ya uchezaji na hicho ndicho kitu pekee wanachotakiwa kukipigania badala ya kupambana na rekodi ya Arsenal ya miaka 22 bila taji.

The post Soka la Arsenal lamkosha Pep first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/soka-la-arsenal-lamkosha-pep/feed/ 0
Gamondi, makocha Zanzibar kuteta https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/gamondi-makocha-zanzibar-kuteta/ https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/gamondi-makocha-zanzibar-kuteta/#respond Sat, 18 Apr 2026 19:59:21 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14544 Na mwandishi wetuKocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Miguel Gamondi anatarajia kushiriki katika warsha maalum na makocha wa timu zinazoshiriki Ligi Kuu Zanzibar.Taarifa ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) iliyopatikana Ijumaa Aprili 17, 2026 ilieleza kuwa warsha hiyo itafanyika Aprili 20, 2026 kwenye Ukumbi wa Uwanja wa New Amaan, Zanzibar.Katika taarifa […]

The post Gamondi, makocha Zanzibar kuteta first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Miguel Gamondi anatarajia kushiriki katika warsha maalum na makocha wa timu zinazoshiriki Ligi Kuu Zanzibar.
Taarifa ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) iliyopatikana Ijumaa Aprili 17, 2026 ilieleza kuwa warsha hiyo itafanyika Aprili 20, 2026 kwenye Ukumbi wa Uwanja wa New Amaan, Zanzibar.
Katika taarifa hiyo hata hivyo haikuwekwa wazi nini hasa mada itakayojadiliwa na Gamondi na makocha hao wa timu 16 zinazoshiriki ligi hiyo ambayo kwa sasa ipo katika raundi ya 23.
Timu zinazoshiriki Ligi Kuu Zanzibar ni pamoja na JKU, Chipukizi, Junguni, Kipanga, KMKM, Fufuni, Uhamiaji, Polisi, Zimamoto, Mafunzo, KVZ, Mwembemakumbi City, NS Town, New King, Mlandege na Malindi.
Tangu achaguliwe kuwa kocha mkuu wa Taifa Stars mwishoni mwa mwaka jana, hii itakuwa mara ya kwanza kwa Gamondi kupata nafasi ya kukaa pamoja na makocha wa timu za Ligi Kuu Zanzibar.

The post Gamondi, makocha Zanzibar kuteta first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/gamondi-makocha-zanzibar-kuteta/feed/ 0
Kocha Herve afutwa kazi Saudi Arabia https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/kocha-herve-afutwa-kazi-saudi-arabia/ https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/kocha-herve-afutwa-kazi-saudi-arabia/#respond Sat, 18 Apr 2026 19:56:19 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14541 Riyadh, Saudi ArabiaKocha Herve Renard amefutwa kazi katika timu ya taifa ya Saudi Arabia, ikiwa ni miezi miwili kabla ya kuanza kwa fainali za Kombe la Dunia 2026 zitakazofanyika katika nchi za Marekani, Canada na Mexico.Herve, 57, kocha kutoka Ufaransa amefutwa kazi rasmi Ijumaa Aprili 17, 2026, baada ya kukabidhiwa jukumu la kuinoa timu hiyo […]

The post Kocha Herve afutwa kazi Saudi Arabia first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Riyadh, Saudi Arabia
Kocha Herve Renard amefutwa kazi katika timu ya taifa ya Saudi Arabia, ikiwa ni miezi miwili kabla ya kuanza kwa fainali za Kombe la Dunia 2026 zitakazofanyika katika nchi za Marekani, Canada na Mexico.
Herve, 57, kocha kutoka Ufaransa amefutwa kazi rasmi Ijumaa Aprili 17, 2026, baada ya kukabidhiwa jukumu la kuinoa timu hiyo maarufu Green Falcons kwa mara ya pili mwaka 2024.
Kabla ya hapo kocha huyo alikuwa na timu hiyo kwenye fainali za Kombe la Dunia 2022 zilizofanyika Qatar na kuweka historia kwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Argentina ambao baadaye waliibuka mabingwa wa dunia.
Baada ya fainali za Kombe la Dunia 2022, Herve aliondoka Saudi Arabia na kujiunga na timu ya taifa ya wanawake Ufaransa ambayo aliiongoza kwenye Michezo ya Olimpiki ya Paris 2024 kabla ya kurudi Saudi Arabia kwa mara ya pili.
Kabla ya kutimuliwa kwa Herve, chanzo kimoja cha habari kiliripoti kuwa Saudi Arabia ilikuwa na mpango wa kumuajiri Matt Crocker katika nafasi ya ukurugenzi wa soka kazi ambayo pia amekuwa akifanya katika Shirikisho la Soka Marekani.
Katika fainali za Kombe la Dunia 2026 zitakazoanza Juni 11, Saudi Arabia imepangwa Kundi H pamoja na timu za Hispania, Cape Verde na Uruguay na mechi yao ya kwanza itakuwa Juni 15 dhidi ya Uruguay.

The post Kocha Herve afutwa kazi Saudi Arabia first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/kocha-herve-afutwa-kazi-saudi-arabia/feed/ 0
Yanga yaisulubu Mbeya City 6-0 https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/yanga-yaisulubu-mbeya-city-6-0/ https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/yanga-yaisulubu-mbeya-city-6-0/#respond Sat, 18 Apr 2026 19:53:28 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14537 Na mwandishi wetuVinara wa Ligi Kuu NBC, Yanga wameendelea kudhihirisha umahiri wao katika ligi hiyo kwa kuichapa Mbeya City mabao 6-0 katika mechi iliyopigwa Alhamisi Machi 16, 2026 kwenye dimba la KMC, Mwenge Dar es Salaam.Yanga ilianza kuonesha makali yake katika dakika ya saba ya mchezo huo kwa bao la Prince Dube aliyeutumia vyema mpira […]

The post Yanga yaisulubu Mbeya City 6-0 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Vinara wa Ligi Kuu NBC, Yanga wameendelea kudhihirisha umahiri wao katika ligi hiyo kwa kuichapa Mbeya City mabao 6-0 katika mechi iliyopigwa Alhamisi Machi 16, 2026 kwenye dimba la KMC, Mwenge Dar es Salaam.
Yanga ilianza kuonesha makali yake katika dakika ya saba ya mchezo huo kwa bao la Prince Dube aliyeutumia vyema mpira wa kona uliopigwa na Pacome Zouzoua.
Wakati Mbeya City wakianza kupambana kutaka kusawazisha bao hilo, dakika tatu baadaye walikatishwa tamaa kwa kufungwa bao la pili lililofungwa na Pacome.
Hali ikazidi kuwa ngumu kwa timu hiyo kutoka Mbeya baada ya kuchapwa bao la tatu mfungaji akiwa Maxi Nzengeli kabla ya timu hiyo kuokota tena mpira kwenye nyavu zao dakika ya 44 kwa bao la Pacome.
Katika dakika za nyongeza kabla ya timu kwenda mapumziko, Mohamed Hussein Zimbwe Jr aliipatia Yanga bao la tano baada ya kuinasa pasi ya Alan Okelo na kuzifanya timu hizo kwenda mapumziko Yanga wakiwa mbele kwa mabao 5-0.
Bao la sita lililohitimisha karamu ya mabao ya Yanga lilijazwa wavuni kwa mara nyingine na Prince Dube katika dakika ya 82
Ushindi huo unazidi kuiimarisha Yanga kileleni mwa msimamo wa ligi wakati kwa Mbeya City hali inazidi kuwa mbaya ambapo katika mechi zake 19, timu hiyo imekusanya pointi 17 tu ikizidi kujiweka katika hatari ya kushuka daraja.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo, Mashujaa na Singida Black Stars ziligawana pointi moja moja baada ya kutoka sare ya bao 1-1, mabao ya washindi yakifungwa na Elvis Rupia kwa Singida BS na Mgandila Shaaban kwa Mashujaa.

The post Yanga yaisulubu Mbeya City 6-0 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/yanga-yaisulubu-mbeya-city-6-0/feed/ 0
Carrick ampigia hesabu Rashford https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/carrick-ampigia-hesabu-rashford/ https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/carrick-ampigia-hesabu-rashford/#respond Sat, 18 Apr 2026 19:51:12 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14535 Manchester, EnglandKocha wa Man United, Michael Carrick amekataa kufuta uwezekano wa kurejea kwa mshambuliaji wa timu hiyo, Marcus Rashdord ambaye kwa sasa anacheza kwa mkopo katika klabu ya Barcelona.Kauli ya kocha huyo wa muda imekuja wakati huu kukiwa na hali isiyoeleweka kuhusu mambo ya baadaye ya Rashford katika kikosi cha Barcelona.Rashford, 28, ambaye pia ni […]

The post Carrick ampigia hesabu Rashford first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Manchester, England
Kocha wa Man United, Michael Carrick amekataa kufuta uwezekano wa kurejea kwa mshambuliaji wa timu hiyo, Marcus Rashdord ambaye kwa sasa anacheza kwa mkopo katika klabu ya Barcelona.
Kauli ya kocha huyo wa muda imekuja wakati huu kukiwa na hali isiyoeleweka kuhusu mambo ya baadaye ya Rashford katika kikosi cha Barcelona.
Rashford, 28, ambaye pia ni mshambuliaji wa timu ya taifa ya England mara ya mwisho kuichezea Man United, ilikuwa Desemba 2024 na kumalizia msimu uliopita akiwa Aston Villa kwa mkopo kabla ya kuhamia Barcelona katika msimu wa 2025-26.
Barcelona au Barca inaweza kumsajili Rashford kwa dau la Pauni 30 milioni wakati wa majira ya kiangazi kama sehemu ya makubaliano ambayo yatamfanya mshambuliaji huyo kubaki katika klabu hiyo.
Wakati huo huo Man United wanafuatilia kwa karibu habari za nchini Hispania zinazodai kwamba Barcelona wana nia ya kufanya mazungumzo mapya kuhusu mchezaji huyo ikiwamo kupunguza ada yake ili aendelee kuwa hapo kwa mkopo katika makubaliano mengine.
Kwa upande mwingine mabosi wa Man United wanadaiwa kutokuwa tayari kwa mazungumzo mengine kuhusu usajili wa mshambulijai huyo na badala yake wanataka kumrudisha katika klabu hiyo iwapo Barca hawatapanda dau.
Man United wanaamini kiwango cha Rashford katika La Liga kimekuwa juu hivyo wanaweza kuwa na nafasi ya kufanya mazungumzo na klabu nyingine ikiwamo kupandisha ada ya uhamisho iwapo Barca hawatakuwa tayari.

The post Carrick ampigia hesabu Rashford first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/04/18/carrick-ampigia-hesabu-rashford/feed/ 0
Simba, Azam zagawana pointi https://www.greensports.co.tz/2026/04/06/simba-azam-zagawana-pointi/ https://www.greensports.co.tz/2026/04/06/simba-azam-zagawana-pointi/#respond Mon, 06 Apr 2026 17:50:22 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14527 Na mwandishi wetuAzam FC imeshindwa kuutumia vyema uwanja wake wa nyumbani baada ya kutoka sare ya 0-0 na Simba katika mechi ya Ligi Kuu NBC iliyochezwa Jumapili, Aprili 5, 2028 kwenye dimba la Azam Complex, Dar es Salaam.Matokeo hayo yanaibakisha Simba katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 35 baada ya kucheza mechi 16 wakati […]

The post Simba, Azam zagawana pointi first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Azam FC imeshindwa kuutumia vyema uwanja wake wa nyumbani baada ya kutoka sare ya 0-0 na Simba katika mechi ya Ligi Kuu NBC iliyochezwa Jumapili, Aprili 5, 2028 kwenye dimba la Azam Complex, Dar es Salaam.
Matokeo hayo yanaibakisha Simba katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 35 baada ya kucheza mechi 16 wakati Azam ikibaki katika nafasi ya tatu na pointi zake 33 ikiwa imecheza mechi 17.
Azam iliuanza vizuri mchezo ikitawala kwa muda mrefu wa kipindi cha kwanz lakini haikuweza kufanya shambulizi lililozaaa matunda katika lango la Simba.
Kipindi cha pili, Simba nao walianza kuonesha uhai wakidhibiti mashambulizi ya Azam na kutengeneza nafasi kadhaa lakini walishindwa kumtungua kipa wao wa zamani, Aishi Manula.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo, TRA United wakiwa nyumbani Sheikh Amri Abeid walitoka na ushindi wa mabao dhidi ya Singida Black Stars.

The post Simba, Azam zagawana pointi first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/04/06/simba-azam-zagawana-pointi/feed/ 0
Rais wa soka Italia ajiuzulu https://www.greensports.co.tz/2026/04/06/rais-wa-soka-italia-ajiuzulu/ https://www.greensports.co.tz/2026/04/06/rais-wa-soka-italia-ajiuzulu/#respond Mon, 06 Apr 2026 17:48:30 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14524 Roma, ItaliaRais wa Shirikisho la Soka Italia (FIGC), Gabriele Gravina ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo ikiwa ni siku chache baada ya taifa hilo lenye heshima katika soka duniani kushindwa kufuzu fainali za Kombe la Dunia.Italia, mabingwa wa Kombe la Dunia 2006, wameshindwa kufuzu fainali hizo kwa mara ya tatu mfululizo kuanzia 2018 na 2022 na sasa […]

The post Rais wa soka Italia ajiuzulu first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Roma, Italia
Rais wa Shirikisho la Soka Italia (FIGC), Gabriele Gravina ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo ikiwa ni siku chache baada ya taifa hilo lenye heshima katika soka duniani kushindwa kufuzu fainali za Kombe la Dunia.
Italia, mabingwa wa Kombe la Dunia 2006, wameshindwa kufuzu fainali hizo kwa mara ya tatu mfululizo kuanzia 2018 na 2022 na sasa watakosekana katika fainali za mwaka 2026 zitakazoanza rasmi Juni 11 katika nchi za Mexico, Canada na Marekani.
Uamuzi wa Gravina kujiuzulu nafasi hiyo umechangiwa na shinikizo kutoka kwa wanasiasa na wadau mbalimbali wa soka ambao wamechukizwa na kufeli kwa timu hiyo licha ya heshima ya muda mrefu ya Italia katika soka duniani.
Baada ya kiongozi hiyo, kujiuzulu, mwingine aliyechukua uamuzi huo ni kipa mkongwe, Gianluigi Buffon ambaye naye ametangaza kuacha kuichezea timu ya taifa huku ikiaminika kuwa kocha Gennaro Gattuso naye yuko mbioni kuchukua uamuzi huo.
Waziri wa Michezo wa Italia, Andrea Abodi ametaka yafanyike mabadiliko katika uongozi wa soka nchini humo hasa baada ya nchi hiyo kushuhudiwa ikikosa mara mbili kushiriki fainali hizo chini ya Gravina.

“Ni jambo lililo wazi kwa kila mtu kwamba uongozi wa soka Italia unahitaji kufumuliwa na utekelezaji wa jambo hilo unatakiwa kuanzia kwa uongozi wa FIGC,” alisema Abodi.


Matarajio ya Italia kufuzu fainali za Kombe la Dunia yalikwama kwenye mechi za play-off baada ya timu hiyo mabingwa mara nne ya Kombe la Dunia kushindwa katika mikwaju ya penalti mbele ya Bosnia & Herzegovina.
Gravina alichukua uongozi wa FIGC mwaka 2018 kutoka kwa Carlo Tavecchio ambaye pia alijiuzulu baada ya Italia au Azzurri kushindwa kufuzu fainali hizo.

The post Rais wa soka Italia ajiuzulu first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/04/06/rais-wa-soka-italia-ajiuzulu/feed/ 0
Yanga yazidi kuizamisha Prisons https://www.greensports.co.tz/2026/04/06/yanga-yazidi-kuizamisha-prisons/ https://www.greensports.co.tz/2026/04/06/yanga-yazidi-kuizamisha-prisons/#respond Mon, 06 Apr 2026 17:45:53 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14521 Na mwandishi wetuYanga imezidi kuizamisha Prisons kwenye Ligi Kuu NBC baada ya kuinyuka mabao 3-0 katika mechi iliyochezwa Jumamosi Aprili 4, 2026 kwenye dimba la KMC, Mwenge, Dar es Salaam.Matokeo hayo yanazidi kufifisha matumaini ya Prisons kucheza ligi hiyo msimu ujao kwani hiyo inakuwa mechi ya tano mfululizo kwa timu hiyo bila kupata ushindi na […]

The post Yanga yazidi kuizamisha Prisons first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Yanga imezidi kuizamisha Prisons kwenye Ligi Kuu NBC baada ya kuinyuka mabao 3-0 katika mechi iliyochezwa Jumamosi Aprili 4, 2026 kwenye dimba la KMC, Mwenge, Dar es Salaam.
Matokeo hayo yanazidi kufifisha matumaini ya Prisons kucheza ligi hiyo msimu ujao kwani hiyo inakuwa mechi ya tano mfululizo kwa timu hiyo bila kupata ushindi na katika mechi 18 ilizocheza imeambulia pointi 13 na inashika nafasi ya 15.
Kwa upande wa Yanga matokeo hayo yanazidi kuiimarisha timu hiyo katika msimamo wa ligi ikiwa kileleni na pointi zake 41 baada ya kuingia dimbani mara 17.
Prisons iliuanza mchezo kwa kuonesha umakini ikishambulia na kujihami vizuri na haikushangaza katika dakika 45 za kwanza hakuna timu iliyoliona lango la mpinzani wake.
Kipindi cha pili Yanga ilikianza kivingine na kufanikiwa kuzichana nyavu za Prisons katika dakika ya 50 kwa bao lililofungwa na Allan Okelo aliyeitumia krosi ya Israel Mwenda.
Yanga iliendelea kulisakama lango la Prisons na kuongeza bao la pili dakika ya 68 lililofungwa na Mudathir Yahya baada ya kushirikiana vyema na Okello wakati bao la tatu lilifungwa na Pazome Zouzoua dakika ya 87 akiitumia pasi ya Duke Abuya.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo, Namungo walikuwa wenyeji wa JKT Tanzania na timu hizo zilimaliza dakika 90 kwa sare ya mabao 2-2.

The post Yanga yazidi kuizamisha Prisons first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/04/06/yanga-yazidi-kuizamisha-prisons/feed/ 0
Arteta awatetea waliojitoa timu za taifa https://www.greensports.co.tz/2026/04/06/arteta-awatetea-waliojitoa-timu-za-taifa/ https://www.greensports.co.tz/2026/04/06/arteta-awatetea-waliojitoa-timu-za-taifa/#respond Mon, 06 Apr 2026 17:43:37 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14519 London, EnglandKocha wa Arsenal, Mikel Arteta amewakingia kifua wachezaji wake waliojiweka kando na timu zao za taifa akidai kuwa klabu yao ina uhusiano mzuri na timu hizo licha ya uamuzi wa wachezaji hao.Katika mechi za hivi karibuni za timu za taifa wachezaji 228 kutoka timu 20 za Ligi Kuu England waliitwa kwenye timu zao za […]

The post Arteta awatetea waliojitoa timu za taifa first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

London, England
Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta amewakingia kifua wachezaji wake waliojiweka kando na timu zao za taifa akidai kuwa klabu yao ina uhusiano mzuri na timu hizo licha ya uamuzi wa wachezaji hao.
Katika mechi za hivi karibuni za timu za taifa wachezaji 228 kutoka timu 20 za Ligi Kuu England waliitwa kwenye timu zao za taifa kwa mechi za kirafiki, kati yao 23 walijitoa katika mechi hizo wengi wao wakiwa wa Arsenal.
Kitendo cha wachezaji wa Arsenal kutoungana na wenzao kwenye timu za taifa kimeibua uvumi kwamba uamuzi huo huenda unatokana na janga la wachezaji majeruhi katika timu hiyo au hofu ya wachezaji wengine kupata majeraha.
Arteta hata hivyo alipingana na mtazamo huo na kubainisha kuwa hali ya kiafya na uwapo wa wachezaji majeruhi vyote viliwekwa wazi kwa viongozi wa timu zao za taifa.

“Tuna uhusiano mzuri na tunawasiliana na timu karibu zote za taifa hasa kocha wa England, Thomas (Tuchel), tumekuwa tukiwapa ushirikiano wakati wote, tunapowasilisha taarifa kuhusu hali ya kila mchezaji tunakuwa wakweli na uamuzi unafikiwa kwa kuzingatia ripoti ya madaktari na baada ya hapo ndipo tunapofikia uamuzi wa mwisho,” alisema Arteta.


Baada ya Arsenal kushindwa kutamba mbele ya Man City kwenye mechi ya fainali ya Kombe la Carabao, beki William Saliba aliweka wazi kuwa hatoungana na wenzake kwenye timu ya taifa ya Ufaransa kwa sababu ya majeraha ya enka.
Wachezaji wengine waliochukua uamuzi kama wa Saliba ni beki mwenzake Gabriel aliyejitoa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Brazil kwa tatizo la goti pamoja na Bukayo Saka, Declan Rice na Noni Madueke waliojitoa kwenye timu ya England, Martin Zubimendi (Hispania) na Piero Hincapie (Ecuador).
Wengine waliotosa sababu za kuwa majeruhi na timu zao za taifa kwenye mabano ni Eberechi Eze (England), Martin Odegaard (Norway), Jurrien Timber (Uholanzi), Leandro Trossard (Ubelgiji).

The post Arteta awatetea waliojitoa timu za taifa first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/04/06/arteta-awatetea-waliojitoa-timu-za-taifa/feed/ 0