Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz Michezo na Burudani ni zaidi ya ajira Fri, 05 Jun 2026 19:15:03 +0000 en-GB hourly 1 https://wordpress.org/?v=7.0 https://www.greensports.co.tz/wp-content/uploads/2021/09/cropped-WhatsApp-Image-2021-09-02-at-13.12.19-1-32x32.jpeg Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz 32 32 Serengeti Boys yatoa wanne Best Eleven Afcon-17 https://www.greensports.co.tz/2026/06/05/serengeti-boys-yatoa-wanne-best-eleven-afcon-17/ https://www.greensports.co.tz/2026/06/05/serengeti-boys-yatoa-wanne-best-eleven-afcon-17/#respond Fri, 05 Jun 2026 19:15:02 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14689 Rabat, MoroccoKikosi bora cha wachezaji 11 maarufu Best Eleven cha fainali za Kombe la Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 (Afcon-17) kimetajwa ambapo timu ya Tanzania, Serengeti Boys imetoa wachezaji wanne.Serengeti Boys imeweka rekodi kwa kufikia kwa mara ya kwanza hatua ya fainali kabla ya kulala mbele ya Senegal waliobeba taji hilo kwa ushindi […]

The post Serengeti Boys yatoa wanne Best Eleven Afcon-17 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Rabat, Morocco
Kikosi bora cha wachezaji 11 maarufu Best Eleven cha fainali za Kombe la Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 (Afcon-17) kimetajwa ambapo timu ya Tanzania, Serengeti Boys imetoa wachezaji wanne.
Serengeti Boys imeweka rekodi kwa kufikia kwa mara ya kwanza hatua ya fainali kabla ya kulala mbele ya Senegal waliobeba taji hilo kwa ushindi wa penalti 4-2 baada ya sare ya bao 1-1.
Timu hiyo iliweza kuonesha ubabe hatua ya robo fainali kwa kuitoa Algeria kabla ya kumalizia kwa kuitoa Misri katika nusu fainali na kuikabili Senegal katika fainali iliyopigwa Jumanne, Juni 2, 2026 kwenye Uwanja wa Moulay El Hassan mjini Rabat.
Wachezaji wanne wa Serengeti Boys waliomo katika Best Eleven au Best XI hiyo ni beki Hussein Mbegu na viungo Issa Chole na Dismas Athanas pamoja na winga Razak Mbegelendi.
Serengeti ambao pia wametwaa tuzo ya Fair Play, wachezaji wake mbali na kuingia katika Best XI, pia walitwaa tuzo akiwamo Chole aliyetwaa tuzo ya mchezaji bora wa fainali hizo.
Mchezaji mwingine ambaye pia yumo katika Best XI ni Athanas ambaye pia ndiye aliyetwaa tuzo ya mfungaji bora au Golden Boot akibebwa na mabao yake matatu.
Kikosi kamili cha wachezaji waliomo katika Best XI ya Afcon-17 na nchi wanazotoka katika mabano ni kama ifuatavyo…
Kipa
Thierno Sow (Senegal)
Mabeki
Thierno Sow (Senegal)
Hussein Mbegu (Tanzania)
Adam Soudi (Morocco)
Lamine Mbengue (Senegal)
Viungo
Issa Chole (Tanzania)
Ahmed Abdelhalim (Egypt)
Dismas Athanasi (Tanzania)
Washambuliaji
Razaki Mbegelendi (Tanzania)
Mohamed Amine Moustache (Morocco)
Mouhamed Wagne (Senegal)

The post Serengeti Boys yatoa wanne Best Eleven Afcon-17 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/06/05/serengeti-boys-yatoa-wanne-best-eleven-afcon-17/feed/ 0
Shakira, Burna Boy kutoa burudani Kombe la Dunia https://www.greensports.co.tz/2026/06/05/shakira-burna-boy-kutoa-burudani-kombe-la-dunia/ https://www.greensports.co.tz/2026/06/05/shakira-burna-boy-kutoa-burudani-kombe-la-dunia/#respond Fri, 05 Jun 2026 19:09:51 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14686 Mexico City, MexicoMwanamuziki wa Colombia, Shakira (pichani) atatoa burudani kwa kuimba wimbo maalum katika hafla ya fainali za Kombe la Dunia 2026 mjini Mexico City kabla ya mechi ya ufunguzi ya fainali hizo.Shakira atapanda jukwaani Juni 11, 2026 kuzipamba fainali hizo katika dimba la Azteca kabla ya mechi ya ufunguzi kati ya wenyeji Mexico watakaoumana […]

The post Shakira, Burna Boy kutoa burudani Kombe la Dunia first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Mexico City, Mexico
Mwanamuziki wa Colombia, Shakira (pichani) atatoa burudani kwa kuimba wimbo maalum katika hafla ya fainali za Kombe la Dunia 2026 mjini Mexico City kabla ya mechi ya ufunguzi ya fainali hizo.
Shakira atapanda jukwaani Juni 11, 2026 kuzipamba fainali hizo katika dimba la Azteca kabla ya mechi ya ufunguzi kati ya wenyeji Mexico watakaoumana na Afrika Kusini.
Wimbo maarufu wa Dai Dai wa lugha ya kitaliano ambao maana yake isiyo rasmi ni ‘twende pamoja au ‘njoo’ ulizinduliwa na kutangazwa kuwa ndio wimbo rasmi wa fainali hizo ambazo pia zitafanyika katika nchi za Canada na Marekani.
Katika kutoa burudani hiyo, Shakira atakuwa pamoja na mwanamuziki wa Nigeria, Burn Boy wakati wasanii wengine watakaotoa burudani ni J Balvin pia wa Colombia na Tyla wa Afrika Kusini.
Kwa Shakira hii si mara ya kwanza kupata fursa ya kutumbuiza kwenye fainali za Kombe la Dunia, anakumbukwa mwaka 2010 nchini Afrika Kusini alipotamba na kibao cha ‘Waka Waka This time for Afrika’.
Shakira ambaye amewahi kuwa mpenzi wa beki wa zamani wa Barcelona na timu ya taifa ya Hispania, Gerard Pique, pia alipata nafasi ya kutoa burudani kwenye fainali za Kombe la Dunia 2006 nchini Ujerumani na 2014 nchini Brazil.
Kwa mujibu wa Fifa, hafla za ufunguzi wa fainali za Kombe la Dunia zitafanyika kabla ya kila mechi ya kwanza katika nchi zote tatu mwenyeji za fainali hizo.
Kwa Canada burudani ya muziki itatolewa na wasanii Michael Bublé na Alanis Morissette mjini Toronto Juni 12 kwenye Uwanja wa BMO kabla ya mechi kati ya wenyeji Canada dhidi ya Bosnia & Herzegovina.
Nchini Marekani, burudani hiyo itatolewa na Katy Perry na Future mjini Los Angeles katika Uwanja wa SoFi kabla ya mechi kati ya wenyeji Marekani dhidi ya Paraguay ambayo pia itachezwa Juni 12.

The post Shakira, Burna Boy kutoa burudani Kombe la Dunia first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/06/05/shakira-burna-boy-kutoa-burudani-kombe-la-dunia/feed/ 0
Chole wa Serengeti Boys mchezaji bora Afcon-17 https://www.greensports.co.tz/2026/06/04/chole-wa-serengeti-boys-mchezaji-bora-afcon-17/ https://www.greensports.co.tz/2026/06/04/chole-wa-serengeti-boys-mchezaji-bora-afcon-17/#respond Thu, 04 Jun 2026 17:25:33 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14682 Rabat, MoroccoKiungo wa Serengeti Boys, Issa Chole ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) kwa vijana chini ya miaka 17 zilizofikia tamati Jumanne, Juni 2, 2026 nchini Morocco.Sambamba na Chole mchezaji mwingine wa Serengeti Boys, Dismas Shida alitwaa tuzo ya kiatu cha dhahabu Golden Boot, mshambuliaji huyo aliifungia […]

The post Chole wa Serengeti Boys mchezaji bora Afcon-17 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Rabat, Morocco
Kiungo wa Serengeti Boys, Issa Chole ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) kwa vijana chini ya miaka 17 zilizofikia tamati Jumanne, Juni 2, 2026 nchini Morocco.
Sambamba na Chole mchezaji mwingine wa Serengeti Boys, Dismas Shida alitwaa tuzo ya kiatu cha dhahabu Golden Boot, mshambuliaji huyo aliifungia Serengeti mabao matatu katika michuano hiyo.
Serengeti Boys iliweka rekodi kwa kufikia hatua ya fainali ya michuano hiyo kwa mara ya kwanza lakini ilishindwa na Senegal walioibuka vinara kwa penalti 4-2 baada ya sare ya bao 1-1 katika muda wa kawaida.
Timu hiyo chini ya kocha Elieneza Nsanganzelu ilianza mbio zake hadi fainali ikiongoza katika kundi lake kabla ya kuibwaga Algeria katika robo fainali na baada ya hapo kuitoa Misri katika nusu fainali kwa mikwaju ya penalti.
Wakati huo huo, kipa wa timu ya taifa ya vijana ya Senegal au The Young Lions of Teranga, Assane Sarr ametwaa tuzo ya kipa bora wa fainali hizo baada ya kuiwezesha timu yake kubeba taji la michuano hiyo.
Umahiri wa Sarr ambaye pia ndiye nahodha wa timu hiyo ulionekana kwa kipindi kirefu cha fainali hizo akiokoa michomo kadhaa iliyoelekezwa langoni mwake ikiwamo mikwaju ya penalti.

C

The post Chole wa Serengeti Boys mchezaji bora Afcon-17 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/06/04/chole-wa-serengeti-boys-mchezaji-bora-afcon-17/feed/ 0
Pérez kutangaza usajili mkubwa Real Madrid https://www.greensports.co.tz/2026/06/04/perez-kutangaza-usajili-mkubwa-real-madrid/ https://www.greensports.co.tz/2026/06/04/perez-kutangaza-usajili-mkubwa-real-madrid/#respond Thu, 04 Jun 2026 17:23:29 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14679 Madrid, HispaniaZikiwa zimebaki siku chache kabla ya uchaguzi wa rais wa klabu ya Real Madrid, rais wa sasa wa klabu hiyo, Florentino Pérez (pichani) ameahidi kutangaza jina kubwa la kwanza la mchezaji kwa ajili ya usajili wa msimu ujao.Wanachama wa klabu ya Real Madrid, Jumapili, Juni 7, 2026 watapiga kura kumchagua rais katika uchaguzi wa […]

The post Pérez kutangaza usajili mkubwa Real Madrid first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Madrid, Hispania
Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya uchaguzi wa rais wa klabu ya Real Madrid, rais wa sasa wa klabu hiyo, Florentino Pérez (pichani) ameahidi kutangaza jina kubwa la kwanza la mchezaji kwa ajili ya usajili wa msimu ujao.
Wanachama wa klabu ya Real Madrid, Jumapili, Juni 7, 2026 watapiga kura kumchagua rais katika uchaguzi wa kwanza katika kipindi cha miaka 20 ambao unatarajiwa kuwa na ushindani mkali.
Perez, 79 ,ambaye ni jina kubwa katika klabu hiyo anatarajia kupata upinzani kutoka kwa mfanyabiashara wa nishati jadidifu, Enrique Riquelme, 37.
Zipo habari kwamba Real Madrid ipo katika hatua nzuri za kumsajili beki Ibrahima Conte ambaye ameachana na klabu ya Liverpool na sasa ni mchezaji huru na huenda hilo likawa jina la kwanza kubwa katika usajili anaoutaja Perez.
Riquelme katika kampeni zake ameahidi akichaguliwa, mshambuliaji wa zamani wa timu hiyo, Raúl González atakuwa mkurugenzi wake wa michezo na anaamini kiungo wa Man City, Rodri ni aina ya mchezaji anayetakiwa kuichezea Real Madrid.
“Alhamisi hii nitatangza jina kubwa la usajili wa msimu ujao, kila mmoja anafahamu mipango yangu katika michezo, ni kusajili wachezaji bora na kuendeleza ushindi,” alisema Perez.
Kuhusu Jose Mourinho kuwa kocha mpya wa timu hiyo, Perez hakuwa tayari kumtaja kocha huyo badsala yake alisema kwamba hivi karibuni atatangaza nani kocha mpya Real Madrid.

The post Pérez kutangaza usajili mkubwa Real Madrid first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/06/04/perez-kutangaza-usajili-mkubwa-real-madrid/feed/ 0
Senegal bingwa Afcon-17, Serengeti Boys yakwama https://www.greensports.co.tz/2026/06/03/senegal-bingwa-afcon-17-serengeti-boys-yakwama/ https://www.greensports.co.tz/2026/06/03/senegal-bingwa-afcon-17-serengeti-boys-yakwama/#respond Wed, 03 Jun 2026 18:04:00 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14676 Rabat, MoroccoNdoto ya timu ya soka ya vijana chini ya miaka 17 ya Tanzania, Serengeti Boys, kutwaa Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon-17) zimeyeyuka baada ya kulala kwa penalti 4-2 mbele ya Senegal.Katika mechi hiyo iliyochezwa Jumanne Juni 2, 2026 kwenye Uwanja wa Moulay El Hassan mjini Rabat, timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1 […]

The post Senegal bingwa Afcon-17, Serengeti Boys yakwama first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Rabat, Morocco
Ndoto ya timu ya soka ya vijana chini ya miaka 17 ya Tanzania, Serengeti Boys, kutwaa Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon-17) zimeyeyuka baada ya kulala kwa penalti 4-2 mbele ya Senegal.
Katika mechi hiyo iliyochezwa Jumanne Juni 2, 2026 kwenye Uwanja wa Moulay El Hassan mjini Rabat, timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1 kabla ya kuingia kwenye mikwaju ya penalti.
Serengeti ndio waliouanza mchezo huo kwa kasi na mapema dakika ya saba waliandika bao mfungaji akiwa ni Hamis Chenga aliyemchungulia vyema kipa wa Senegal kabla ya kupiga shuti lililokwenda upande wa kushoto wa kipa huyo aliyeishia kuutazama mpira.
Senegal au The Young Lions of Teranga walisawazisha bao hilo dakika ya 64 mfungaji akiwa ni Ibrahima Dione aliyemalizia mpira wa adhabu uliopigwa na Souleymane Faye na kipa wa Serengeti, Haji Abdullah kushindwa kuumiliki mpira.
Juhudi za kila timu kupambana kusaka bao la kuongeza hazikuweza kuzaa matunda na ndipo utaratibu wa penalti ulipochukua nafasi yake.
Kwa upande wa Senegal waliofunga penalti zao ni Faye, Sadio, Dione na Thior wakati kwa Serengeti waliofunga ni Yusuph na Mbegelendi huku Klendemo na Mbegu wakikosa.
Hilo linakuwa taji la pili kwa Senegal wakati kwa Serengeti Boys ambao ni mara ya kwanza kufikia hatua ya fainali wameshindwa kutimiza ndoto ya kulibeba taji hilo kwa mara ya kwanza na sasa wanajiandaa kushiriki fainali za Kombe la Dunia.

The post Senegal bingwa Afcon-17, Serengeti Boys yakwama first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/06/03/senegal-bingwa-afcon-17-serengeti-boys-yakwama/feed/ 0
Declan Rice ajivunia Arsenal https://www.greensports.co.tz/2026/06/03/declan-rice-ajivunia-arsenal/ https://www.greensports.co.tz/2026/06/03/declan-rice-ajivunia-arsenal/#respond Wed, 03 Jun 2026 18:00:26 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14673 Budapest, HungaryKiungo wa Arsenal, Declan Rice amesema ameumizwa baada ya kushindwa kubeba taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya lakini anajivunia yeye na wachezaji wenzake kwa kufikia hatua ya fainali.Arsenal ilishindwa kutamba katika mechi ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya mbele ya PSG kwa mikwaju ya penalti 4-3 baada ya sare ya bao 1-1 katika […]

The post Declan Rice ajivunia Arsenal first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Budapest, Hungary
Kiungo wa Arsenal, Declan Rice amesema ameumizwa baada ya kushindwa kubeba taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya lakini anajivunia yeye na wachezaji wenzake kwa kufikia hatua ya fainali.
Arsenal ilishindwa kutamba katika mechi ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya mbele ya PSG kwa mikwaju ya penalti 4-3 baada ya sare ya bao 1-1 katika dakika 90 za kawaida na 30 za nyongeza mechi iliyochezwa Jumamosi Mei 30, 2026.
Mabingwa hao wa Ligi Kuu England walikuwa na matumaini makubwa ya kubeba taji hilo ikiwa ni mara yao ya kwanza kufikia hatua ya fainali ya michuano hiyo mikubwa ya klabu tangu wafanye hivyo mara ya mwisho mwaka 2006.
Rice alisema inaumiza na kukatisha tamaa unapolikosa taji la Ligi ya Mabigngwa Ulaya katika hatua ya fainali kwa mikwaju ya penalti.

“Tunajaribu kuchukua mitazamo mingi kwa kuzingatia hatua kubwa tuliyofikia tukiwa timu, ni msimu wa kipekee, hii mechi yetu ya mwisho ni ya 63 katika michuano yote, tulijitoa kwa kila kitu hadi hatua hii tuliyofikia,” alisema Rice.


Rice alisema waliifikisha mechi kwenye hatua ya penalti na aliifahamu hatua hiyo ni kamari lakini anaamini katika soka ni unashinda au unashindwa kwenye penalti, na zipo timu bora ambazo zimepoteza mechi kwenye penalti katika fainali.
Alisema wao Arsenal wapo katika kundi lililoshindwa lakini cha msingi ni kwamba wameshinda pamoja na kushindwa pamoja.
Rice aliongeza kwa kusema kuwa ingawa ameumizwa lakini akikumbuka jinsi walivyouanza msimu mwezi Julai na hadi walipofikia sasa kila kitu kinaonesha kuwa ilikuwa safari nzuri ya msimu.

The post Declan Rice ajivunia Arsenal first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/06/03/declan-rice-ajivunia-arsenal/feed/ 0
PSG yabeba tena taji Ulaya https://www.greensports.co.tz/2026/05/31/psg-yabeba-tena-taji-ulaya/ https://www.greensports.co.tz/2026/05/31/psg-yabeba-tena-taji-ulaya/#respond Sun, 31 May 2026 12:20:42 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14670 Budapest, HungaryParis St-Germain au PSG ya Ufaransa kwa mara ya pili mfululizo imedhihirisha ubora wake barani Ulaya kwa kubeba taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya na kufuta matumaini ya Arsenal kubeba taji hilo.PSG wamebeba taji hilo kwa ushindi wa penalti 4-3 dhidi ya Arsenal baada ya sare ya bao 1-1 katika mechi iliyochezwa Jumamosi, Mei […]

The post PSG yabeba tena taji Ulaya first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Budapest, Hungary
Paris St-Germain au PSG ya Ufaransa kwa mara ya pili mfululizo imedhihirisha ubora wake barani Ulaya kwa kubeba taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya na kufuta matumaini ya Arsenal kubeba taji hilo.
PSG wamebeba taji hilo kwa ushindi wa penalti 4-3 dhidi ya Arsenal baada ya sare ya bao 1-1 katika mechi iliyochezwa Jumamosi, Mei 30, 2026 mjini Budapest, Hungary.
Miezi 12 iliyopita, ni PSG hao hao waliolibeba taji hilo kwa kuichapa Inter Milan mabao 5-0 katika mechi ya fainali iliyopigwa mjini Munich, Ujerumani.
Arsenal waliouanza vyema mchezo wakiwa na matumaini makubwa yaliyozaa bao la mapema dakika ya sita mfungaji akiwa ni Havertz kwa pasi ya Trossard, bao lililodumu kwa dakika 45 za awali.
PSG walipambana na kupata bao la kusawazisha lililofungwa na Dembele katika dakika ya 65 kwa mkwaju wa penalti na hatimaye timu kumaliza dakika 90 kwa sare pamoja na 30 za nyongeza kabla ya kuingia kwenye penalti na PSG kuibuka mashujaa.
Furaha isiyo kifani ilidhihirika kwa kocha wa PSG, Luis Enrique anayeingia katika rekodi ya watu watano waliobeba taji hilo mara tatu na ambaye alinukuliwa baada ya mechi akisema kwamba amechanganywa kwa furaha.
“Nina furaha, uchovu wa akili na kila kitu lakini hili ni tukio muhimu la msimu, sisi bado ni mabingwa, mara mbili mfululizo, ni jambo la kipekee,” alisema Enrique.
Mtu mwingine aliyedhihirisha furaha ya ushindi huo ni rais wa klabu ya PSG, Nasser Al-Khelaifi ambaye baada ya Enrique kuvalishwa medali yake, wawili hao walionekana wakicheza mbele ya mashabiki kufurahia taji hilo.
PSG chini ya Enrique ambaye pia alilibeba taji hilo mwaka 2015 akiwa mchezaji wa Barcelona, tangu akabidhiwe jukumu la kuinoa timu hiyo Julai 2023 amefanikiwa kuigeuza kuwa timu bora.
Baada ya kuachana na baadhi ya wachezaji mastaa kina Lionel Messi, Kylian Mbappe, Neymar Jr na wengineo, Enrique ni kama alianza kufanya kazi ya kuisuka upya PSG na akafanikiwa kuifanya iwe katika ubora.
Ubora wa timu hiyo ukiendelea hakuna atakayeshangaa iwapo wataisogelea rekodi ya Real Madrid ya kutwaa mataji matano ya Ulaya kwa miaka mitano mfululizo waliyoiweka kati ya mwaka 1956 hadi 1960.

The post PSG yabeba tena taji Ulaya first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/05/31/psg-yabeba-tena-taji-ulaya/feed/ 0
Wawili Serengeti Boys waitwa Taifa Stars https://www.greensports.co.tz/2026/05/31/wawili-serengeti-boys-waitwa-taifa-stars/ https://www.greensports.co.tz/2026/05/31/wawili-serengeti-boys-waitwa-taifa-stars/#respond Sun, 31 May 2026 12:18:59 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14668 Na mwandishi wetuKocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania, ‘Taifa Stars’, Miguel Gamondi amewaita katika kikosi chake wachezaji wawili wa timu ya vijana chini ya miaka 17 ya Tanzania maarufu Serengeti Boys.Taarifa ya TFF iliyopatikana Ijumaa Mei 29, 2026 iliwataja wachezaji hao kuwa ni Kassim Juma na Luqman Mbalasalu ambao watajiunga katika kikosi hicho […]

The post Wawili Serengeti Boys waitwa Taifa Stars first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania, ‘Taifa Stars’, Miguel Gamondi amewaita katika kikosi chake wachezaji wawili wa timu ya vijana chini ya miaka 17 ya Tanzania maarufu Serengeti Boys.
Taarifa ya TFF iliyopatikana Ijumaa Mei 29, 2026 iliwataja wachezaji hao kuwa ni Kassim Juma na Luqman Mbalasalu ambao watajiunga katika kikosi hicho baada ya Juni 2, 2026.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyosainiwa na ofisa habari na mawasiliano wa TFF, Cliford Ndimbo, Taifa Stars itacheza mechi ya kirafiki iliyopo kwenye kalenda ya Fifa dhidi ya Uganda Cranes, Ijumaa, Juni 5, 2026.
Baada ya mechi hiyo, Stars itaingia tena uwanjani Jumanne, Juni 9, 2026 kwa mechi yake ya pili dhidi ya timu ya Rwanda, mechi zote hizo zitachezwa mjini Marakech, Morocco.
Wachezaji wengine wa timu hiyo waliotajwa katika kikosi cha Gamondi, wameanza kuingia kambini tangu Ijumaa iliyopita.
Kwa upande wa Serengeti Boys, timu hiyo itacheza mechi ya fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) chini ya miaka 17 dhidi ya Senegal, mechi itakayochezwa mjini Rabat, Morocco, usiku wa Jumanne, Juni 2, 2026 kwenye Uwanja wa Moulay El Hassan.

The post Wawili Serengeti Boys waitwa Taifa Stars first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/05/31/wawili-serengeti-boys-waitwa-taifa-stars/feed/ 0
Slot atimuliwa Liverpool https://www.greensports.co.tz/2026/05/31/slot-atimuliwa-liverpool/ https://www.greensports.co.tz/2026/05/31/slot-atimuliwa-liverpool/#respond Sun, 31 May 2026 08:53:43 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14664 Liverpool, EnglandKlabu ya Liverpool imetangaza kumfuta kazi aliyekuwa kocha wake, Arne Slot baada ya kuinoa timu hiyo kwa misimu miwili.Slot, 47, kocha kutoka Uholanzi msimu uliopita wa 2024-25 aliiongoza vyema timu hiyo hadi kubeba taji la Ligi Kuu England lakini msimu wake wa pili wa 2025-26 umekuwa mgumu.Liverpool imemaliza msimu ikiwa nafasi ya tano, nafasi […]

The post Slot atimuliwa Liverpool first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Liverpool, England
Klabu ya Liverpool imetangaza kumfuta kazi aliyekuwa kocha wake, Arne Slot baada ya kuinoa timu hiyo kwa misimu miwili.
Slot, 47, kocha kutoka Uholanzi msimu uliopita wa 2024-25 aliiongoza vyema timu hiyo hadi kubeba taji la Ligi Kuu England lakini msimu wake wa pili wa 2025-26 umekuwa mgumu.
Liverpool imemaliza msimu ikiwa nafasi ya tano, nafasi ambayo haikuwafurahisha mabosi wa timu hiyo hadi kumtimua kocha huyo huku majina kadhaa yakianza kutajwa likiwamo la aliyekuwa kocha wa Bournemouth, Andoni Iraola.
Taarifa ya wamiliki wa klabu ya Liverpool, Fenway Sports Group (FSG) imeuelezea uamuzi wa kumfuta kazi Slot kuwa ni mgumu kutokana na mchango wake kwa muda ambao amekuwa na timu hiyo.

“Huu ni uamuzi mgumu kwetu kuufanya kwa kuzingatia mchango wa Arne katika klabu ya Liverpool, muda ambao amekuwa hapa umekuwa wa mafanikio na wenye maana kubwa kwetu pamoja na mashabiki,” ilieleza taarifa ya FSG.


FSG pia walimshukuru kocha huyo kwa kila alichokifanikisha na kueleza kuwa shukrani hizo hazitoshi kwa namna ambavyo amekuwa akiwajibika kwa kuzingatia maadili ya kazi, umakini na kiwango cha juu cha utaalam.
Mambo yote hayo kwa mujibu wa FSG yanaendena na mtazamo wao kuwa Slot alikuwa kiongozi katika eneo lake.
Katika taarifa hiyo, FSG pia walibainisha kuwa tangu mara ya kwanza kukutana na Slot na kuanza kufanya naye kazi walibaini wazi kwamba hakuwa tu mtu mwenye kukubali majukumu yake bali aliyakumbatia.

The post Slot atimuliwa Liverpool first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/05/31/slot-atimuliwa-liverpool/feed/ 0
Ronaldo atajwa Kombe la Dunia 2030 https://www.greensports.co.tz/2026/05/31/ronaldo-atajwa-kombe-la-dunia-2030/ https://www.greensports.co.tz/2026/05/31/ronaldo-atajwa-kombe-la-dunia-2030/#respond Sun, 31 May 2026 08:51:44 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14662 Porto, UrenoKocha wa timu ya Ureno, Roberto Martinez amesema hakuna wa kutilia shaka habari kuwa Cristiano Ronaldo anaweza kucheza katika fainali za Kombe la Dunia 2030 wakati huo akiwa na miaka 45.Ronaldo atakuwa na timu ya Ureno kwenye fainali za Kombe la Dunia 2026 zinazotarajia kutimua vumbi Juni 11 katika nchi za Marekani, Mexico na […]

The post Ronaldo atajwa Kombe la Dunia 2030 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Porto, Ureno
Kocha wa timu ya Ureno, Roberto Martinez amesema hakuna wa kutilia shaka habari kuwa Cristiano Ronaldo anaweza kucheza katika fainali za Kombe la Dunia 2030 wakati huo akiwa na miaka 45.
Ronaldo atakuwa na timu ya Ureno kwenye fainali za Kombe la Dunia 2026 zinazotarajia kutimua vumbi Juni 11 katika nchi za Marekani, Mexico na Canada, hii ikiwa ni mara ya sita kwa mchezaji huyo kushiriki fainali hizo.
Fainali za Kombe la Dunia 2030 zitafanyika kwa ushirikiano katika mataifa ya Mexico na Hispania na Martinez anaamini kwa wakati huo haitokuwa ajabu jina la Ronaldo kuwamo kwenye kikosi cha Ureno.
Ronaldo alianza kuichezea Ureno mara ya kwanza mwaka 2003, kwa sasa ndiye anayeongoza kuichezea timu hiyo mara nyingi (226) akiwa amefunga mabao 143 na ni mchezaji pekee mwenye rekodi ya kufunga mabao katika fainali tano za Kombe la Dunia.
Martinez aliulizwa swali iwapo Ronaldo ataweza kushiriki fainali za Kombe la Dunia 2030 ambapo kocha huyo alisema hakuna anayeweza kutilia shaka jambo hilo.
Kauli ya Martinez imekuja wakati Ronaldo mwenyewe hajaweka wazi ni lini hasa atastaafu kuichezea timu hiyo hivyo haitokuwa ajabu akiwa na timu hiyo.
Ronaldo ambaye pia amewahi kutamba na timu za Man United na Real Madrid, kwa sasa anacheza soka Saudi Arabia katika klabu ya Al Nassr akiwa ndiye mchezaji anayelipwa fedha nyingi.
Ureno ipo Kundi K, itacheza mechi yake ya kwanza ya Kombe la Dunia Juni 17 dhidi ya DR Congo na kufuatiwa na mechi dhidi ya Uzbekistan Juni 23 na kumalizia mechi za makundi dhidi ya Colombia Juni 27.

The post Ronaldo atajwa Kombe la Dunia 2030 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/05/31/ronaldo-atajwa-kombe-la-dunia-2030/feed/ 0