Salah - Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz Michezo na Burudani ni zaidi ya ajira Sun, 05 Jan 2025 14:01:57 +0000 en-GB hourly 1 https://wordpress.org/?v=6.8 https://www.greensports.co.tz/wp-content/uploads/2021/09/cropped-WhatsApp-Image-2021-09-02-at-13.12.19-1-32x32.jpeg Salah - Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz 32 32 Salah haiwazii hatma yake Liverpool https://www.greensports.co.tz/2025/01/01/salah-haiwazii-hatma-yake-liverpool/ https://www.greensports.co.tz/2025/01/01/salah-haiwazii-hatma-yake-liverpool/#respond Wed, 01 Jan 2025 17:54:48 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=12549 Liverpool, EnglandMshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah amesema bado hajaamua lolote kuhusu mambo yake ya baadaye na klabu hiyo wakati huu akiendelea kudhihirisha ubora wake.Salah hivi karibuni ameifungia Liverpool bao moja katika ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya West Ham na kutoa pasi zilizozaa mabao mengine mawili katika ushindi huo.Wachezaji wengine wa Liverpool, Virgil van Dijk […]

The post Salah haiwazii hatma yake Liverpool first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Liverpool, England
Mshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah amesema bado hajaamua lolote kuhusu mambo yake ya baadaye na klabu hiyo wakati huu akiendelea kudhihirisha ubora wake.
Salah hivi karibuni ameifungia Liverpool bao moja katika ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya West Ham na kutoa pasi zilizozaa mabao mengine mawili katika ushindi huo.
Wachezaji wengine wa Liverpool, Virgil van Dijk na Trent Alexander-Arnold kama ilivyo kwa Salah nao wapo katika miezi yao sita ya mwisho kabla ya mikataba yao kufikia ukomo ingawa Salah ndiye amekuwa mjadala zaidi.
Na ingawa kumekuwa na hofu kwamba anaweza akaondoka Liverpool, Salah amesema fikra zake kwa sasa zipo katika kuhakikisha anashinda taji akiwa na timu hiyo na yuko mbali na mpango wowote wa kusaini mkataba mpya.

“Hapana hilo jambo kwa sasa lipo mbali, na sitaki kuwe na chochote kwenye vyombo vya habari, kitu pekee kilicho katika fikra zangu ni kutaka Liverpool ibebe taji la ligi, nataka kuwa mmoja wa wahusika wa jambo hilo” alisema Salah.


Alifafanua kwamba atafanya kila kilicho bora kwa ajili ya timu kushinda taji na kwa sasa ni timu chache zinazowakaribia hivyo wanahitaji kuwa makini na kuendelea na kasi yao.
Kwa upande wake kocha wa Liverpool, Arne Slot amesema hana wasiwasi na wachezaji hao waandamizi kwamba wanaweza kuanza mazungumzo na klabu nyingine Januari Mosi kwa kuwa anaamini amekuwa mwenye usimamizi wa hatma yao.

The post Salah haiwazii hatma yake Liverpool first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/01/01/salah-haiwazii-hatma-yake-liverpool/feed/ 0
Salah aanza kuaga Liverpool https://www.greensports.co.tz/2024/12/02/salah-aanza-kuaga-liverpool/ https://www.greensports.co.tz/2024/12/02/salah-aanza-kuaga-liverpool/#respond Mon, 02 Dec 2024 12:40:54 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=12301 Liverpool, EnglandMshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah amesema ushindi wa timu hiyo wa mabao 2-0 wa jana Jumamosi dhidi ya Man City ni mechi ya mwisho kwake kuivaa timu hiyo kwenye dimba la Anfield.Kauli ya mchezaji hiyo inaashiria kwamba ataihama timu hiyo huku habari zaidi zikidai kwamba vigogo wa klabu ya PSG ya Ufaransa wako katika […]

The post Salah aanza kuaga Liverpool first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
Liverpool, England
Mshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah amesema ushindi wa timu hiyo wa mabao 2-0 wa jana Jumamosi dhidi ya Man City ni mechi ya mwisho kwake kuivaa timu hiyo kwenye dimba la Anfield.
Kauli ya mchezaji hiyo inaashiria kwamba ataihama timu hiyo huku habari zaidi zikidai kwamba vigogo wa klabu ya PSG ya Ufaransa wako katika mkakati mzito wa kumsajili mchezaji huyo.
Katika mechi ya jana Salah ndiye aliyetoa pasi iliyozaa bao la kwanza la Liverpool lililofungwa na Cody Gakpo na baada ya hapo akafunga bao la pili kwa penalti iliyotolewa baada ya Luis Diaz kuchezewa rafu na Stefan Ortega.
Ushindi huo umeifanya Liverpool kushika usukani katika Ligi Kuu England (EPL) ikiwa mbele kwa tofauti ya tisa na kuwaacha Man City ambao ni mabingwa watetezi kwa tofauti ya pointi 11.
Mara baada ya mechi hiyo Salah aliulizwa kuhusu mambo ya baadaye ndani ya Liverpool na kukiri kwamba huenda hiyo ikawa mechi yake ya mwisho dhidi Man City huku mkataba wake na Liverpool ukifikia ukomo mwishoni mwa msimu huu.

“Ukweli ni kwamba haya ni mambo yangu, hadi sasa hii ndiyo mechi yangu ya mwisho kuichezea Liverpool dhidi ya Man City kwa hiyo nilienda kuifurahia, mazingira yalikuwa ya kuvutia, hivyo naifurahia kila hatua, ni matumaini kwamba tutashinda taji la ligi na baada ya hapo mengine yatafuata,” alisema Salah.


Akifafanua zaidi kuhusu hatma yake ndani ya kikosi cha Liverpool Salah alisema kwamba huu ni mwezi Desemba na hajapata ofa yoyote ya kubaki katika klabu hiyo kwa hiyo huenda yeye ni wa kuondoka zaidi kuliko wa kubaki.
“Mnajua nimekuwa katika klabu hii kwa miaka mingi, hakuna klabu kama hii lakini mwisho wa siku si suala langu peke yangu, na kama nilivyosema hii ni Desemba na hakuna lolote lililofanyika kuhusu mambo yangu ya baadaye katika klabu hii,” alisema Salah.
Salah pia amekuwa akihusishwa kwenda kucheza soka Saudi Arabia ingawa PSG ndio wanaotajwa zaidi kuisaka saini ya mshambuliaji huyo kwa imani kwamba watamsajili baada ya msimu huu akiwa mchezaji huru.

The post Salah aanza kuaga Liverpool first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/12/02/salah-aanza-kuaga-liverpool/feed/ 0
Rodrygo kumrithi Salah Liverpool https://www.greensports.co.tz/2024/09/26/rodrygo-atajwa-kumrithi-salah-liverpool/ https://www.greensports.co.tz/2024/09/26/rodrygo-atajwa-kumrithi-salah-liverpool/#respond Thu, 26 Sep 2024 05:56:15 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=11944 Madrid, HispaniaLiverpool imeanza kupiga hesabu za kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid, Rodrygo ili achukue nafasi ya Mohamed Salah baada ya kuwapo habari kwamba Salah anajipanga kuihama timu hiyo.Hivi karibuni, Salah, 32, mshambuliaji tegemeo wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri, japo hakuwa wazi lakini alisema huu unaweza kuwa msimu wake wa mwisho kuvaa jezi […]

The post Rodrygo kumrithi Salah Liverpool first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Madrid, Hispania
Liverpool imeanza kupiga hesabu za kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid, Rodrygo ili achukue nafasi ya Mohamed Salah baada ya kuwapo habari kwamba Salah anajipanga kuihama timu hiyo.
Hivi karibuni, Salah, 32, mshambuliaji tegemeo wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri, japo hakuwa wazi lakini alisema huu unaweza kuwa msimu wake wa mwisho kuvaa jezi ya Liverpool.
Kauli hiyo inaonesha kwamba huenda Liverpool ikamkosa mshambuliaji huyo ambaye kwa muda mrefu amekuwa akiwindwa na klabu kadhaa za Saudi Arabia na ndio maana Liverpool imeanza mapema hesabu za mtu wa kuziba nafasi hiyo.
Katika harakati hizo, chanzo kimoja cha habari kimeripoti kuwa jina la Rodrygo, ambaye pia ni mshambuliaji wa timu ya Brazil ndilo linalotajwa zaidi na kuonekana anaweza kuwa mtu sahihi wa kuchukua nafasi hiyo.
Kwa upande wa Rodrygo kinachoonekana ni kwamba huenda akawa tayari kwa changamoto mpya hasa kutokana na ushindani wa namba ambao unatajwa katika kikosi cha kwanza cha Real Madrid.


Tangu Real Madrid imsajili Kylian Mbappe kumekuwa na hofu kuhusu nafasi ya Rodrygo ingawa kocha Carlo Ancelotti amekuwa akiwapa nafasi washambuliaji watatu kwenye kikosi cha kwanza.
Msimu uliopita, Real Madrid ilibeba mataji ya La Liga na Ligi ya Mabingwa Ulaya ambapo kwa La Liga Rodrygo alifunga mabao 10 katika mechi 34 na kwa Ligi ya Mabingwa alifunga mabao matano.
Rodrygo, 23, pamoja na kufunga mabao hayo, jina lake halimo katika wachezaji wanaowania tuzo ya Ballon d’Or jambo ambalo alisema limemsikitisha kwa kuwa anaamini alipaswa kuwamo.
Wachezaji wa Real Madrid waliomo katika orodha ya wanaowania tuzo hiyo ni Vinícius Júnior, Jude Bellingham, Federico Valverde, Toni Kroos, Antonio Rüdiger, Dani Carvajal na Mbappe.

The post Rodrygo kumrithi Salah Liverpool first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/09/26/rodrygo-atajwa-kumrithi-salah-liverpool/feed/ 0
Salah atangaza kuondoka Liverpool https://www.greensports.co.tz/2024/09/02/salah-atangaza-kuondoka-liverpool/ https://www.greensports.co.tz/2024/09/02/salah-atangaza-kuondoka-liverpool/#respond Mon, 02 Sep 2024 20:42:48 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=11850 Liverpool, EnglandMshambuliaji wa timu ya Liverpool, Mohamed Salah amesema kwamba huenda huu ukawa msimu wake wa mwisho kuichezea timu hiyo.Salah ambaye jana Jumapili aliiwakilisha Liverpool katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Man United kwenye Ligi Kuu England (EPL), mkataba wake na timu hiyo unafikia ukomo mwishoni mwa msimu huu wa 2024-25.Katika mechi hiyo, Salah, 32, […]

The post Salah atangaza kuondoka Liverpool first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Liverpool, England
Mshambuliaji wa timu ya Liverpool, Mohamed Salah amesema kwamba huenda huu ukawa msimu wake wa mwisho kuichezea timu hiyo.
Salah ambaye jana Jumapili aliiwakilisha Liverpool katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Man United kwenye Ligi Kuu England (EPL), mkataba wake na timu hiyo unafikia ukomo mwishoni mwa msimu huu wa 2024-25.
Katika mechi hiyo, Salah, 32, ambaye pia ni mshambuliaji wa timu ya taifa ya Misri, alifunga bao moja na kutoa asisti mbili.
“Nimekuwa na kipindi kizuri cha mapumziko ya kiangazi, nimekuwa na muda mrefu wa kukaa peke yangu na kufikiria mazuri, kama unavyofahamu huu ni mwaka wangu wa mwisho katika klabu hii,” alisema Salah.
Salah alisema anachotaka ni kuufurahia msimu huu na hadhani kama atakuwa mtu mwenye fikra nyingi badala yake anachoona ni kwamba yuko huru kucheza soka na mambo yajayo yatajulikana.
“Hakuna mtu yeyote aliyezungumza nami kuhusu mkataba wangu, kwa hiyo kilicho sahihi ni kuwa nitacheza katika msimu wangu wa mwisho na baada ya msimu tutaona itakavyokuwa, si juu yangu,” alisema Salah.
Septemba mwaka jana Liverpool ilikataa ofa ya Pauni 150 milioni kutoka klabu ya Al Ittihad ya Saudi Arabia na ingawa zipo habari za klabu hiyo kuanza upya mpango wa kumtaka Salah lakini jambo hilo bado halijawa rasmi.
Kwa upande wake kocha wa Liverpool, Arne Slot alisema kwamba hatojadili suala la mchezaji huyo kuhusu mkataba wake badala yake anachofahamu ni kwamba Salah ni mchezaji wao na jambo hilo linampa furaha.
Wachezaji wengine wa Liverpool ambao mikataba yao inafikia ukomo mwishoni mwa msimu huu ni pamoja n nahodha Virgil van Dijk na Trent Alexander-Arnold.

The post Salah atangaza kuondoka Liverpool first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/09/02/salah-atangaza-kuondoka-liverpool/feed/ 0
Salah aahidi kuipigania Liverpool https://www.greensports.co.tz/2024/05/22/salah-aahidi-kuipigania-liverpool/ https://www.greensports.co.tz/2024/05/22/salah-aahidi-kuipigania-liverpool/#respond Wed, 22 May 2024 07:50:24 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=11069 Liverpool, EnglandMshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah ameonesha dalili zote za kubaki Liverpool baada ya kuahidi kuendelea kuipigania mataji timu hiyo kwa nguvu zote licha ya kuondoka kwa kocha Jurgen Klopp.Salah anaingia katika mwaka wake wa mwisho wa mkataba wake wa sasa na hadi sasa hakuna makubaliano yoyote yaliyofikiwa baina ya klabu na mchezaji huyo ili […]

The post Salah aahidi kuipigania Liverpool first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Liverpool, England
Mshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah ameonesha dalili zote za kubaki Liverpool baada ya kuahidi kuendelea kuipigania mataji timu hiyo kwa nguvu zote licha ya kuondoka kwa kocha Jurgen Klopp.
Salah anaingia katika mwaka wake wa mwisho wa mkataba wake wa sasa na hadi sasa hakuna makubaliano yoyote yaliyofikiwa baina ya klabu na mchezaji huyo ili kumuongezea mkataba zaidi ya muda uliobaki.
Majira ya kiangazi msimu uliopita, Liverpool ilikataa ofa ya Pauni milioni 150 ili kumuuza Salah katika klabu ya Al Ittihad ya Saudi Arabia ingawa kwa sasa zipo habari kwamba klabu hiyo huenda ikaamsha upya mpango huo.
Mara baada ya Klopp kuaga rasmi Liverpool na kocha mpya, Arne Slot kutangazwa rasmi, majaliwa ya Salah katika klabu hiyo yalianza kujadiliwa na kukawa na hofu kwamba huenda naye akaondoka.
Kupitia mitandao ya kijamii, Salah hata hivyo ameupinga mpango wowote wa kuondoka baada ya kusema kwamba atakuwa na Liverpool msimu ujao na azma yake ni kuipa mafanikio timu hiyo.

“Tunajua kwamba mataji ndio kitu muhimu na tutafanya kila kinachowezekana kuliwezesha hilo msimu ujao, mashabiki wetu wana haki katika hilo na tutapambana hakuna mfano,” alisema Salah.


Salah, 31, pia alimpongeza kocha anayeondoka Klopp ambaye hivi karibuni walitibuana katika mechi dhidi ya West Ham kwa kinachodhaniwa kuwa alichukia kuwekwa benchi na kocha huyo.
“Ni jambo kubwa kubeba mataji na kupata uzoefu nawe katika miaka saba iliyopita, nakutakia heri kwa mambo yako yajayo, natumaini tutakutana tena,” alisema Salah katika posti yake kwenye mitandao ya kijamii iliyoambatana na picha yake akiwa na Klopp.

The post Salah aahidi kuipigania Liverpool first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/05/22/salah-aahidi-kuipigania-liverpool/feed/ 0
Klopp, Salah wamaliza utata https://www.greensports.co.tz/2024/05/04/klopp-salah-wamaliza-utata/ https://www.greensports.co.tz/2024/05/04/klopp-salah-wamaliza-utata/#respond Sat, 04 May 2024 18:57:35 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=10839 Liverpool, EnglandKocha wa Liverpool, Jürgen Klopp amesema kwamba mzozo ulioibuka kati yake na mshambuliaji wake, Mohamed Salah mwishoni mwa wiki iliyopita katika mechi yao na West Ham haupo tena.Klopp na Salah walionekana katika picha za televisheni wakitoleana kauli zilizoashiria kuwapo mzozo baina yao wakati wa mechi hiyo iliyoisha kwa sare ya mabao 2-2.Baada ya mechi […]

The post Klopp, Salah wamaliza utata first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Liverpool, England
Kocha wa Liverpool, Jürgen Klopp amesema kwamba mzozo ulioibuka kati yake na mshambuliaji wake, Mohamed Salah mwishoni mwa wiki iliyopita katika mechi yao na West Ham haupo tena.
Klopp na Salah walionekana katika picha za televisheni wakitoleana kauli zilizoashiria kuwapo mzozo baina yao wakati wa mechi hiyo iliyoisha kwa sare ya mabao 2-2.
Baada ya mechi hiyo, Salah ambaye alizozana na kocha wake wakati akiingia uwanjani kutokea benchi, alisema kwamba ‘moto ungeweza kuwaka’ iwapo angeamua kuzungumza kilichojiri.
Katika mkutano na waandishi wa habari jana Ijumaa, Klopp hakutaka kuelezea kwa nini waliingia katika mzozo yeye na mchezaji wake badala yake alisisitiza kwamba jambo hilo limepita na kwa sasa wanaangalia mbele.

“Yote yamemalizwa, hakuna tatizo, kama tungekuwa hatujuani kwa muda mrefu sina hakika kama tungeweza kulifanyia kazi suala hilo, lakini tunajuana kwa muda mrefu na vile vile tunaheshimiana,” alisema Klopp.


Klopp alisisitiza kwamba hakuna tatizo na mambo ya aina hiyo wanaweza kuyamaliza wao wenyewe bila ya kuwapo matarajio ya kuingiliwa na watu wengine wa nje.
Sare dhidi ya West Ham imezidi kufifisha matumaini ya Liverpool kubeba taji la Ligi Kuu England (EPL) kwani kwa sasa inashika nafasi ya tatu ikiwa imeachwa na vinara Arsenal kwa tofauti ya pointi tano zikiwa zimebaki mechi tatu kabla ya kumalizika kwa ligi hiyo.

The post Klopp, Salah wamaliza utata first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/05/04/klopp-salah-wamaliza-utata/feed/ 0
Klopp, Salah hali si shwari https://www.greensports.co.tz/2024/04/28/klopp-salah-hali-si-shwari/ https://www.greensports.co.tz/2024/04/28/klopp-salah-hali-si-shwari/#respond Sun, 28 Apr 2024 09:46:36 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=10769 Liverpool, EnglandKocha wa Liverpool, Jurgen Klopp na mshambuliaji wake, Mohamed Salah inaonekana hawana uhusiano mzuri baada ya kuzozana jana Jumamosi katika mechi ya Ligi Kuu England (EPL) dhidi ya West Ham.Katika mechi hiyo iliyoisha kwa sare ya mabao 2-2, Salah alionekana kama kutoleana maneno yasiyo mazuri na Klopp wakati akijiandaa kuingia uwanjani akitokea benchi katika […]

The post Klopp, Salah hali si shwari first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Liverpool, England
Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp na mshambuliaji wake, Mohamed Salah inaonekana hawana uhusiano mzuri baada ya kuzozana jana Jumamosi katika mechi ya Ligi Kuu England (EPL) dhidi ya West Ham.
Katika mechi hiyo iliyoisha kwa sare ya mabao 2-2, Salah alionekana kama kutoleana maneno yasiyo mazuri na Klopp wakati akijiandaa kuingia uwanjani akitokea benchi katika dakika ya 79.
Klopp baadaye alisema kwamba hawezi kuweka wazi mzozo ulioibuka baina yake na mchezaji huyo ingawa kilicho wazi ni kwamba hali haikuwa shwari baina ya wawili hao.
Akizungumzia tukio hilo, mshambuliaji wa zamani wa Liverpool, Peter Crouch alisema kwamba halikuwa jambo zuri kwa timu hiyo.
“Salah ni mchezaji ambaye katika mechi nyingi za Liverpool amekuwa akianza tangu kipindi cha kwanza na atakuwa mwenye hasira kwa kuanzia benchi,” alisema Crouch na kuongeza kuwa hakuna mtu anayependa kuona jambo kama hilo kwa kocha na mchezaji wake muhimu.
Kilichoonekana kwa Salah ni kama vile alichukizwa na jambo aliloambiwa na Klopp wakati akijiandaa kuingia uwanjani na alitaka kuendeleza mzozo huo lakini wachezaji wenzake, Darwin Nunez na Joe Gomez waliingilia kati na kumlazimisha aondoke.

Salah baada ya mechi alisema kama angeamua kuzungumza ‘moto ungewaka’ wakati Klopp alisema kwamba suala hilo lilizungumzwa kwenye vyumba vya kubadilishia nguo na limekwisha.
Sare hiyo ya mabao 2-2 iliyoipata Liverpool inazidi kuiweka timu hiyo pagumu kwenye mbio za kulisaka taji la EPL kwani inabaki katika nafasi yake ya tatu na inachoomba sasa ni Man City na Arsenal ziharibikiwe katika mechi zao.

The post Klopp, Salah hali si shwari first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/04/28/klopp-salah-hali-si-shwari/feed/ 0
Salah arudi Liverpool kufuata tiba https://www.greensports.co.tz/2024/01/22/salah-arudi-liverpool-kufuata-tiba/ https://www.greensports.co.tz/2024/01/22/salah-arudi-liverpool-kufuata-tiba/#respond Mon, 22 Jan 2024 09:01:09 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=9375 Abidjan, Ivory CoastMshambuliaji na nahodha wa timu ya taifa ya Misri, Mohamed Salah ataondoka kwenye kambi ya timu yake ya taifa nchini Ivory Coast na kwenda Liverpool kupata tiba ya matatizo ya misuli yanayomkabili.Salah yuko Ivory Coast akiiwakilisha timu ya taifa ya Misri kwenye fainali za Afcon na leo Jumatatu timu yake itacheza na Cape […]

The post Salah arudi Liverpool kufuata tiba first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Abidjan, Ivory Coast
Mshambuliaji na nahodha wa timu ya taifa ya Misri, Mohamed Salah ataondoka kwenye kambi ya timu yake ya taifa nchini Ivory Coast na kwenda Liverpool kupata tiba ya matatizo ya misuli yanayomkabili.
Salah yuko Ivory Coast akiiwakilisha timu ya taifa ya Misri kwenye fainali za Afcon na leo Jumatatu timu yake itacheza na Cape Verde na inadaiwa mchezaji huyo atakuwa jukwaani wakati wa mechi hiyo.
Chama cha Soka Misri (Efa) kimethibitisha kuwa Salah ataendelea na matibabu katika klabu yake ya Liverpool kama ilivyoshauriwa na kocha Jurgen Klopp jana Jumapili baada ya mechi ya Liverpool na Bournemouth katika Ligi Kuu England, mechi ambayo Liverpool ilishinda kwa mabao 4-0.

“Matumaini yetu ni kwamba tutakuwa naye katika hatua ya nusu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) kama tutafuzu hatua hiyo,” ilieleza taarifa ya Efa.


Salah aliumia Alhamisi iliyopita katika mechi dhidi ya Ghana iliyoisha kwa sare ya mabao 2-2 na hadi sasa haijawekwa wazi muda ambao majeraha yaliyompata yatapona.
Alipokutana na waandishi wa habari juzi Jumamosi, Salah hata hivyo alikwepa kuzungumzia hali ya majeraha yanayomkabili na anatarajia lini kupona.
Klopp alinukuliwa mara baada ya Salah kuumia akisema kwamba anatarajia mchezaji huyo atarudi Liverpool kwa ajili ya tiba au walau kupata wasaa wa kuwa pamoja na timu ya madaktari wa klabu hiyo.

The post Salah arudi Liverpool kufuata tiba first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/01/22/salah-arudi-liverpool-kufuata-tiba/feed/ 0
Salah ataka mauaji Gaza yasitishwe https://www.greensports.co.tz/2023/10/19/salah-ataka-mauaji-gaza-yasitishwe/ https://www.greensports.co.tz/2023/10/19/salah-ataka-mauaji-gaza-yasitishwe/#respond Thu, 19 Oct 2023 09:43:42 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=8162 Liverpool, EnglandMshambuliaji wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri, Mohamed Salah ametaka viongozi duniani kote kukaa pamoja ili kuzuia mauaji ya raia wasio na hatia yanayoendelea katika mzozo wa Israel-Gaza.Taarifa za maofisa wa afya zimeeleza kuwa maelfu ya watu wa Palestina wameuawa katika mlipuko wa bomu uliotokea katika hospitali moja katika mji ya Gaza […]

The post Salah ataka mauaji Gaza yasitishwe first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Liverpool, England
Mshambuliaji wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri, Mohamed Salah ametaka viongozi duniani kote kukaa pamoja ili kuzuia mauaji ya raia wasio na hatia yanayoendelea katika mzozo wa Israel-Gaza.
Taarifa za maofisa wa afya zimeeleza kuwa maelfu ya watu wa Palestina wameuawa katika mlipuko wa bomu uliotokea katika hospitali moja katika mji ya Gaza juzi Jumanne usiku.
Salah alisema kwamba ukatili na matukio ya umwagaji damu vimeongezeka huku akitaka misaada ya kibinadamu iruhusiwe kuwafikia wahanga wa machafuko hayo.
Maofisa wa Palestina walisema kwamba mlipuko huo wa bomu katika Hospitali ya Al-Ahli Arab ulitokana na uvamizi wa kutumia mabomu ya anga uliofanywa na Jeshi la Anga la Israel.
Taarifa za kijeshi za Israel hata hivyo zilidai kwamba mlipuko huo ni matokeo ya roketi iliyoshindwa kufanya kazi vizuri ambayo ilirushwa na kikundi cha Islamic Jihad cha Palestina, kauli ambayo imepingwa na kikundi hicho.
Ndege za kijeshi za Israel zimekuwa zikirusha mabomu katika maeneo ya Gaza ikiwa ni kujibu mapigo baada ya uvamizi uliofanywa Oktoba 7 na kundi la Hamas la Palestina na kusababisha vifo vya watu 1,400.
Akizungumzia matukio hayo kupitia video iliyowekwa kwenye mitandao ya kijamii, Salah alisema kwamba inasikitisha, “Mazingira katika hospitali yanasikitisha, watu wa Gaza wanahitaji chakula, maji na huduma za matibabu kwa haraka.”

“Nawasihi viongozi duniani kote kukaa pamoja ili kuzuia mauaji zaidi ya mioyo ya watu wasio na hatia, maisha ya watu lazima yalindwe, mauaji yanahitaji kukomeshwa, familia zimetenganishwa,” alisema Salah.


Shirikisho la Soka Algeria jana Jumatano lilitangaza kuahirisha mechi za mashindano ya soka nchini humo kwa nia ya kuwaunga mkono watu wa Palestina na kukubali timu ya Palestina kuweka kambi Algeria na kutumia viwanja vya nchini humo kwa mechi zao.

The post Salah ataka mauaji Gaza yasitishwe first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/10/19/salah-ataka-mauaji-gaza-yasitishwe/feed/ 0
Al-Ittihad wamfuata Salah England https://www.greensports.co.tz/2023/09/05/al-ittihad-wamfuata-salah-england/ https://www.greensports.co.tz/2023/09/05/al-ittihad-wamfuata-salah-england/#respond Tue, 05 Sep 2023 07:50:51 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=7665 London, EnglandJopo la vigogo wa klabu ya Al-Ittihad ya Saudi Arabia limetua England kuishawishi Liverpool kwa mara ya mwisho ili ikubali kuwauzia mshambuliaji wao, Mohamed Salah kwa ada inayofikia Pauni 200 milioni kabla ya keshokutwa Alhamisi.Alhamisi ndiyo siku ya mwisho kabla ya kufungwa rasmi kwa dirisha la usajili kwa ligi ya soka ya Saudi Arabia […]

The post Al-Ittihad wamfuata Salah England first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

London, England
Jopo la vigogo wa klabu ya Al-Ittihad ya Saudi Arabia limetua England kuishawishi Liverpool kwa mara ya mwisho ili ikubali kuwauzia mshambuliaji wao, Mohamed Salah kwa ada inayofikia Pauni 200 milioni kabla ya keshokutwa Alhamisi.
Alhamisi ndiyo siku ya mwisho kabla ya kufungwa rasmi kwa dirisha la usajili kwa ligi ya soka ya Saudi Arabia au Saudi Pro Ligi na kama Al-Ittihad itamkosa kabla ya siku hiyo mpango huo utakuwa umefeli.
Liverpool tayari imeshasema kwamba mshambuliaji huyo kutoka Misri ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 31 hauzwi, hiyo ni baada ya awali Al-Ittihad kumtangazia ofa ya Pauni 150 milioni.
Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp hataki kusikia habari ya Salah kuuzwa na kama akiuzwa mtu wa kwanza kukasirika atakuwa kocha huyo ambaye anaamini Salah ni mchezaji muhimu kwenye kikosi chake.
Juzi Jumapili, Salah aliifungia Liverpool bao wakati timu hiyo ikiibwaga Aston Villa 3-0 katika mechi ya Ligi Kuu England huku Klopp akisema Salah amejidhatiti kuhakikisha anabaki Liverpool msimu huu.
Klopp pamoja na kutoa kauli hiyo lakini kinachoonekana ni kama vile hana uhakika wa asilimia 100 kwamba Salah ni lazima abaki Liverpool.

“Hakuniambia (kama anabaki) lakini hana sababu ya kuniambia hilo, kila kitu kinaonekana, ni kama anazungumza hilo mazoezini kwa kujituma kwake na tabia zake, tulikuwa na kikao wiki hii na kikao hakikuwa kuhusu tuliyoyafanya siku za nyuma bali kilihusu nini tutakifanya siku zijazo,” alisema Klopp.


Wakati hatma ya Salah ikiwa hivyo, mchezaji huyo tayari amewashuhudia wachezaji wenzake aliowahi kuwa nao Liverpool kina Fabinho, Roberto Firmino, Jordan Anderson na Sadio Mane wote wakitimkia Saudi Arabia.

The post Al-Ittihad wamfuata Salah England first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/09/05/al-ittihad-wamfuata-salah-england/feed/ 0