JKT Tanzania - Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz Michezo na Burudani ni zaidi ya ajira Sat, 28 Feb 2026 08:45:58 +0000 en-GB hourly 1 https://wordpress.org/?v=6.9.1 https://www.greensports.co.tz/wp-content/uploads/2021/09/cropped-WhatsApp-Image-2021-09-02-at-13.12.19-1-32x32.jpeg JKT Tanzania - Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz 32 32 Simba yakwama, Yanga yapiga mtu mkono https://www.greensports.co.tz/2026/02/26/simba-yakwama-yanga-yapiga-mtu-mkono/ https://www.greensports.co.tz/2026/02/26/simba-yakwama-yanga-yapiga-mtu-mkono/#respond Thu, 26 Feb 2026 16:33:22 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14367 Na mwandishi wetuWakati Yanga ikishangilia ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mechi ya Ligi Kuu NBC, mambo hayakuwa mazuri kwa mtani wake Simba aliyelazimishwa sare ya bila kufungana na Dodoma Jiji FC.Mechi hizo zilizochezwa Jumatano Febuari 25, 2026 ni mechi za mwisho baina ya watani hao wa jadi kabla ya kukutana […]

The post Simba yakwama, Yanga yapiga mtu mkono first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Wakati Yanga ikishangilia ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mechi ya Ligi Kuu NBC, mambo hayakuwa mazuri kwa mtani wake Simba aliyelazimishwa sare ya bila kufungana na Dodoma Jiji FC.
Mechi hizo zilizochezwa Jumatano Febuari 25, 2026 ni mechi za mwisho baina ya watani hao wa jadi kabla ya kukutana Machi Mosi, 2026 kwenye dimba la New Amaan, Zanzibar katika mwendelezo wa mechi za ligi hiyo.
Karamu ya mabao matano ya Yanga au mkono ilipatikana kwenye Uwanja wa KMC, Kinondoni, Dar es Salaam kwa mabingwa hao watetezi wa ligi kuandika bao la kwanza kunako dakika ya saba mfungaji akiwa ni Mohamed Hussein au Zimbwe Junior baada ya kuinasa pasi ya Prince Dube.
JKT walipambana na kuonesha uhai na hadi timu zinakwenda mapumziko Yanga walikuwa mbele kwa bao hilo pekee licha ya mashambulizi ya mara kwa mara langoni mwa JKT.
Kipindi cha pili mambo yalianza kuwaharibikia JKT katika dakika ya 60 baada ya kufungwa bao la pili, mfungaji akiwa Dilson Depu aliyeitumia vizuri pasi ya Israel Mwenda.
Matumaini ya JKT kutaka bao la kufufua matumaini yalianza kufifia dakika tatu baada baada ya bao la Depu pale, Mudathir Yahya alipoiandikia Yanga bao la tatu.
Mabao mengine mawili ya Yanga yalifungwa na Dube katika dakika ya 83 na Shekhan Khamis aliyekamilisha karamu ya mabao hayo katika dakika ya 89.
Kwa ushindi huo Yanga imejikita kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa na pointi 28 katika mechi 10 sawa na JKT ingawa Yanga ina faida katika mabao ya kufunga na kufungwa.
Kwa upande wa Simba hali ilikuwa tete kwa dakika zote 90 kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana matokeo yanayowafanya mashabiki wa timu hiyo kubaki wakitafakari hatma ya timu yao kabla ya kuivaa Yanga.
Mechi hiyo kwa upande mwingine ilikuwa neema kwa kipa wa Dodoma Jiji, Daniel Mgore ambaye aliibuka mchezaji bora kwa namna ambavyo alifanikiwa kuzima ndoto za washambuliaji wa Simba kupata bao katika dakika zote 90.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo, Azam FC ikiwa nyumbani kwenye dimba la Azam Complex ilitoka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mtibwa Sugar.

The post Simba yakwama, Yanga yapiga mtu mkono first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/02/26/simba-yakwama-yanga-yapiga-mtu-mkono/feed/ 0
Simba yaitandika JKT Tanzania 2-1 https://www.greensports.co.tz/2025/11/09/simba-yaitandika-jkt-tanzania-2-1/ https://www.greensports.co.tz/2025/11/09/simba-yaitandika-jkt-tanzania-2-1/#respond Sun, 09 Nov 2025 08:29:14 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14083 Na mwandishi wetuSimba imetoka kifua mbele kwenye dimba la Meja Jenerali Isamuhyo baada ya kuitandika JKT Tanzania mabao 2-1 katika mechi ya Ligi Kuu NBC iliyochezwa Jumamosi Novemba 8, 2025.Timu zote zilikianza kipindi cha kwanza kwa kusomana na kufanya mashambulizi ya hapa na pale lakini hadi dakika 45 zinakamilika hakuna timu iliyoliona lango la mwenzake.JKT […]

The post Simba yaitandika JKT Tanzania 2-1 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Simba imetoka kifua mbele kwenye dimba la Meja Jenerali Isamuhyo baada ya kuitandika JKT Tanzania mabao 2-1 katika mechi ya Ligi Kuu NBC iliyochezwa Jumamosi Novemba 8, 2025.
Timu zote zilikianza kipindi cha kwanza kwa kusomana na kufanya mashambulizi ya hapa na pale lakini hadi dakika 45 zinakamilika hakuna timu iliyoliona lango la mwenzake.
JKT ndio waliokuwa wa kwanza kuzitikisa nyavu za Simba kwa bao la Edward Songo, lililopatikana katika dakika ya 60 ya mchezo huo kwa shuti la mbali lililomshinda kipa Yakoub Suleiman ambaye ni kipa wa zamani wa JKT.
Iliwachukua dakika zisizozidi tatu sIMBA kusawazisha bao hilo na aliyesawazisha bao ni Wilson Nangu, beki wa zamani wa JKT ambaye kama ilivyo kwa Suleiman naye alicheza dhidi ya waajiri wake wa zamani na ndiye aliyetajwa kuwa mchezaji bora wa mechi hiyo.
Bao la ushindi la Simba lilipatikana dakika ya 77 mfungaji akiwa Jonathan Sowah, nyota wa zamani wa Singida Black Stars ambaye hilo linakuwa bao lake la pili kwenye ligi msimu huu.
Kwa ushindi huo Simba sasa inashika usukani wa ligi hiyo ikiwa na pointi tisa baada ya kushinda mechi zake tatu ilizocheza hadi sasa.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo, Pamba FC ikiwa nyumbani kwenye Uwanja wa CCM Kirumba ilitoka sare ya bao 1-1 na Singida Black Stars, bao la Singida BS lilifungwa na Clatous Chama dakika ya 31 na Pamba kusawazisha dakika ya 51 kwa bao la Kelvin Nashon ambaye ni mchezaji wa zamani wa Singida BS.
Pamba baada ya matokeo hayo inashika nafasi ya pili ikiwa na pointi tisa kama Simba lakini Pamba imezidiwa kwa wastani wa mabao ya kufunga na kufungwa.

The post Simba yaitandika JKT Tanzania 2-1 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/11/09/simba-yaitandika-jkt-tanzania-2-1/feed/ 0
Ngoma aizamisha JKT Tanzania https://www.greensports.co.tz/2025/05/05/ngoma-aizamisha-jkt-tanzania/ https://www.greensports.co.tz/2025/05/05/ngoma-aizamisha-jkt-tanzania/#respond Mon, 05 May 2025 20:33:45 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=13398 Na mwandishi wetuBao pekee la Fabrice Ngoma limeiwezesha Simba kutoka na ushindi wa 1-0 dhidi ya JKT Tanzania na hivyo kujiimarisha katika mbio za kuliwania taji la Ligi Kuu NBC.Katika mechi hiyo iliyochezwa leo Jumatatu, Mei 5, 2025 kwenye Uwanja wa Ismuhuyo, Dar es Salaam, bao hilo lilipatikana muda mfupi kabla ya timu kwenda mapumziko […]

The post Ngoma aizamisha JKT Tanzania first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
Na mwandishi wetu
Bao pekee la Fabrice Ngoma limeiwezesha Simba kutoka na ushindi wa 1-0 dhidi ya JKT Tanzania na hivyo kujiimarisha katika mbio za kuliwania taji la Ligi Kuu NBC.
Katika mechi hiyo iliyochezwa leo Jumatatu, Mei 5, 2025 kwenye Uwanja wa Ismuhuyo, Dar es Salaam, bao hilo lilipatikana muda mfupi kabla ya timu kwenda mapumziko baada ya Ngoma kuinasa pasi ya Steven Mukwala.
Kwa ushindi huo Simba ambao pia wanajiandaa kwa mechi ya fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya RS Berkane ya Morocco, sasa wamefikisha pointi 63 katika mechi 24 walizocheza.
Timu hiyo hata hivyo bado ina kazi ya kufanya kuwaondoa mahasimu wa Yanga kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo wakiwa na pointi 70 katika mechi 26.
Kimahesabu Simba watakuwa na kazi nzito ya kuhakikisha wanashinda mechi zote zilizobaki ikiwamo mechi yao na Yanga ili kujihakikishia taji la ligi hiyo.
Kwa upande wa JKT wao wanabaki katika nafasi ya saba wakiwa na pointi 32 baada ya kucheza mechi 27.
Kocha wa Simba, Fadlu Davids baada ya mechi hiyo aliwapongeza wachezaji wake kwa namna walivyopambana na kufanya juhudi hadi kupata ushindi huku akisema kwamba mechi ilikuwa ngumu.
Naye kocha wa JKT, Ahmad Ally alisema kwamba makosa madogo waliyoyafanya dakika za mwisho mwisho za kipindi cha kwanza ndiyo yaliyowafanya waadhibiwe na Simba.

The post Ngoma aizamisha JKT Tanzania first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/05/05/ngoma-aizamisha-jkt-tanzania/feed/ 0
Yanga yaambulia pointi moja kwa JKT https://www.greensports.co.tz/2025/02/10/yanga-yaambulia-pointi-moja-kwa-jkt/ https://www.greensports.co.tz/2025/02/10/yanga-yaambulia-pointi-moja-kwa-jkt/#respond Mon, 10 Feb 2025 18:31:08 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=13001 Na mwandishi wetuYanga, Simba hazichekani, ndicho kilichotokea baada ya Yanga kugawana pointi moja moja na JKT Tanzania katika mechi ya Ligi Kuu NBC iliyopigwa leo Jumatatu Februari 10, 2025.Siku chache zilizopita, Yanga waliwacheka mno Simba wallpogawana pointi moja moja na Fountain Gate katika mechi ya ligi hiyo iliyoisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1.Yanga […]

The post Yanga yaambulia pointi moja kwa JKT first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
Na mwandishi wetu
Yanga, Simba hazichekani, ndicho kilichotokea baada ya Yanga kugawana pointi moja moja na JKT Tanzania katika mechi ya Ligi Kuu NBC iliyopigwa leo Jumatatu Februari 10, 2025.
Siku chache zilizopita, Yanga waliwacheka mno Simba wallpogawana pointi moja moja na Fountain Gate katika mechi ya ligi hiyo iliyoisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1.
Yanga ingawa wanaongoza ligi hiyo wakiwa na pointi 46, kushindwa kunyakua pointi zote tatu katika mechi ya leo inaweza kuwa sababu ya kukaa kileleni kwa muda mfupi.
Hiyo ni kwa sababu Simba wanaoshika nafasi ya pili wana pointi 44 na wapo nyuma kwa mechi moja, Yanga wamecheza mechi 18 wakati Simba wamercheza mechi 17 na kesho Juamnne wataikabili Tanzania Prisons.
Matarajio makubwa waliyokuwa nayo Yanga hii leo ni timu yao kutoka na ushindi kwenye dimba la Meja Jenerali Isamhuyo, Mbweni, Dar es Salaam lakini JKT wamewakatalia na kujikuta wakiambulia pointi moja.
JKT wana kila sababu ya kujipongeza kwa matokeo hayo na zaidi kumpongeza beki wao Wilson Nangu ambaye alikuwa mwiba kwa Yanga na haikushangaza baada ya mechi alipotangazwa kuwa mchezaji bora wa mechi hiyo.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo zilizochezwa leo, Ken Gold imetoka na ushindi wa mabao 2-0 mbele ya Fountain Gate wakati KMC ikiichapa Singida BS mabao 2-0.

The post Yanga yaambulia pointi moja kwa JKT first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/02/10/yanga-yaambulia-pointi-moja-kwa-jkt/feed/ 0
Ahoua azima ndoto za JKT https://www.greensports.co.tz/2024/12/24/ahoua-azima-ndoto-za-jkt/ https://www.greensports.co.tz/2024/12/24/ahoua-azima-ndoto-za-jkt/#respond Tue, 24 Dec 2024 18:08:49 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=12495 Na mwandishi wetuBao pekee la mkwaju wa penalti iliyofungwa kiufundi na Jean Ahoua leo Jumanne kwenye Uwanja wa KMC, Dar es Salaam limezima ndoto za JKT Tanzania kugawana pointi moja moja na Simba katika Ligi Kuu NBC.JKT ikilindwa vyema na kipa Yakoub Suleiman, aliyezuia mashuti ya mara kwa mara ya washambuliaji wa Simba, ilifanikiwa kumaliza […]

The post Ahoua azima ndoto za JKT first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
Na mwandishi wetu
Bao pekee la mkwaju wa penalti iliyofungwa kiufundi na Jean Ahoua leo Jumanne kwenye Uwanja wa KMC, Dar es Salaam limezima ndoto za JKT Tanzania kugawana pointi moja moja na Simba katika Ligi Kuu NBC.
JKT ikilindwa vyema na kipa Yakoub Suleiman, aliyezuia mashuti ya mara kwa mara ya washambuliaji wa Simba, ilifanikiwa kumaliza dakika 90 za kawaida timu zikiwa hazijafungana.
Timu hiyo hata hivyo ilifanya kosa katika dakika sita za nyongeza, kosa ambalo lilizaa penalti iliyoipa Simba ushindi wa bao hilo pekee na pointi tatu muhimu za kujiimarisha kileleni mwa ligi hiyo ikifikisha pointi 37 katika mechi 14.
Kosa hilo lilitokana na mpira wa juu uliopigwa na Ahoua aliyempenyezea Shomari Kapombe ambaye wakati akikimbia kuelekea kwenye lango la JKT na kumuacha beki Mohammed Bakar, beki huyo alimshika Kapombe na kumuangusha chini akiwa eneo la penalti.
Kwa kosa hilo mwamuzi alimpa Bakar kadi ya njano kabla ya kujiridhisha katika rekodi zake na kumpa kadi nyekundu kwa sababu tayari alikua na kadi ya kwanza ya njano.
Ahoua alirudi nyuma akamzuga kipa kabla ya kufumua shuti lililojaa wavuni upande wa kushoto wa kipa huyo ambaye alijichanganya na kuonekana kama alishindwa kujua afanye nini ili kuokoa mpira huo.
Timu zote ziliuanza mchezo kwa kushambuliana kwenye kipindi cha kwanza ingawa Simba ndio waliofanikiwa kupeleka mashambulizi mengi langoni mwa JKT na kama si umahiri wa kipa Suleiman, Simba wangetoka uwanjani na mabao mengi.
Katika dakika ya 16 Elly Mpanzu alipiga krosi safi lakini hakukuwa na mchezaji wa kumalizia na dakika moja baadaye, Ateba aliunganisha kwa kichwa krosi lakini Suleiman alikuwa imara na kuokoa.
JKT nao walifanya shambulizi dakika ya 22 baada ya nyota wa zamani wa Simba, Shiza Kichuya kumpasia Hassan Kapalata ambaye hata hivyo shuti lake lilitoka nje ya goli.
Kipindi cha pili Simba ilikianza kwa kuwatoa Awesu Awesu na nafasi yake kuingia Ahoua, baadaye wakatoka Mpanzu na Ateba na nafasi zao kuingia Mutale na Mukwala.
JKT nao wakafanya mabadiliko kwa kuwaingiza, Kichuya na Magulu na nafasi zao kuingia Matheo Anthony na Mohammed Bakar na baadaye akatoka Idd Gamba na kuingia nyota wa zamani wa Simba na Azam FC, John Bocco.
Simba nao waliendelea na mabadiliko kwa kumtoa Valentino Ouma na kumuingiza Mohamed Hussein ‘Zimbwe Jr’ na baadaye wakamalizia kwa kumuingiza Valentino Mashaka aliyechukua nafasi ya Deborah Fernandes.
Mabadiliko hayo yalionekana kuimarisha ulinzi kwa JKT wakati kwa Simba waliongeza mashambulizi na muda mwingi mpira ulikuwa langoni mwa JKT.
Mashambulizi hayo yalimuweka katika wakati mgumu kipa Suleiman wa JKT aliyekuwa na kazi ya kuokoa na kuchelewesha muda wakati Mussa Camara wa Simba alikuwa na kazi ndogo ya kuokoa mashambulizi machache na kupeleka mipira mbele kwa haraka huku akiwahimiza wachezaji waendeleze mashambulizi.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo, Singida Black Stars ikiwa nyumbani ilitoka na ushindi wa mabao 2-1 mbele ya Ken Gold.
Ushindi huo umeifanya Singida Black kufikisha pointi 33 sawa na Yanga inayoshika nafasi ya pili na Azam FC inayoshika nafasi ya tatu wakati Singida ni ya nne kwa kuwa imezidiwa wastani wa mabao.

The post Ahoua azima ndoto za JKT first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/12/24/ahoua-azima-ndoto-za-jkt/feed/ 0
Simba yaipiga JKT, yaisogelea Yanga https://www.greensports.co.tz/2024/02/15/simba-yaipiga-jkt-yaisogelea-yanga/ https://www.greensports.co.tz/2024/02/15/simba-yaipiga-jkt-yaisogelea-yanga/#respond Thu, 15 Feb 2024 20:08:36 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=9752 Na mwandishi wetuSimba leo imeendelea kuifukuzia Yanga kwenye Ligi Kuu NBC baada ya kutoka na ushindi wa bao 1-0 mbele ya JKT Tanzania katika mechi ya ligi hiyo iliyopigwa kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo.Kwa ushindi huo, Simba sasa inakuwa imefikisha pointi 36 katika mechi 15 ikiwa nafasi ya pili na hivyo inakuwa imezidiwa na […]

The post Simba yaipiga JKT, yaisogelea Yanga first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Simba leo imeendelea kuifukuzia Yanga kwenye Ligi Kuu NBC baada ya kutoka na ushindi wa bao 1-0 mbele ya JKT Tanzania katika mechi ya ligi hiyo iliyopigwa kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo.
Kwa ushindi huo, Simba sasa inakuwa imefikisha pointi 36 katika mechi 15 ikiwa nafasi ya pili na hivyo inakuwa imezidiwa na mahasimu wake Yanga wanaoongoza ligi hiyo kwa tofauti ya pointi nne tu na timu zote hizo zimecheza idadi sawa ya mechi hadi sasa.
Kwa mara nyingine alikuwa ni Clatous Chota Chama aliyewainua vitini mashabiki wa Simba kwa bao hilo pekee katika dakika ya 33 akiitumia vizuri pasi ya Saido Ntibazonkiza.
Hii ni mara ya pili kwa Chama kuifungia Simba bao muhimu katika mechi za hivi karibuni za Ligi Kuu NBC, mara ya mwisho alifanya hivyo katika mechi dhidi ya Azam FC na kuiwezesha Simba kutoka sare ya bao 1-1.
Simba na JKT kwa kipindi kirefu cha mchezo zote zilionesha uhai na uchu wa kusaka bao na JKT wangeweza kupata bao la kusawazisha katika dakika ya 68 lakini Ismail Aziz alishindwa kuitumia nafasi ambayo timu hiyo iliitengeneza kwa kupiga shuti ambalo kipa wa Simba, Ayoub Lakred alilidaka.
Ligi hiyo itaendelea kesho Ijumaa ambapo Azam watakuwa nyumbani Azam Complex kuumana na Geita Gold wakati Kagera Sugar watakuwa wenyeji wa Mashujaa FC kwenye Uwanja wa Kaitaba.

The post Simba yaipiga JKT, yaisogelea Yanga first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/02/15/simba-yaipiga-jkt-yaisogelea-yanga/feed/ 0
Kichuya kuipaisha JKT Tanzania https://www.greensports.co.tz/2024/01/24/kichuya-kuipaisha-jkt-tanzania/ https://www.greensports.co.tz/2024/01/24/kichuya-kuipaisha-jkt-tanzania/#respond Wed, 24 Jan 2024 06:10:00 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=9399 Na mwandishi wetuKocha mkuu wa timu ya JKT Tanzania, Malale Hamsini amesema usajili wa nyota wa zamani wa Simba, Shiza Kichuya utairudisha timu yake nafasi za juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu NBC.Akizungumza na GreenSports leo Jumanne, kocha huyo alisema uzoefu wake kwenye ligi pamoja na kucheza timu kubwa za Mtibwa Sugar, Simba na Namungo […]

The post Kichuya kuipaisha JKT Tanzania first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Kocha mkuu wa timu ya JKT Tanzania, Malale Hamsini amesema usajili wa nyota wa zamani wa Simba, Shiza Kichuya utairudisha timu yake nafasi za juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu NBC.
Akizungumza na GreenSports leo Jumanne, kocha huyo alisema uzoefu wake kwenye ligi pamoja na kucheza timu kubwa za Mtibwa Sugar, Simba na Namungo FC kutaongeza kitu kwao.
“Kichuya ni mchezaji mzoefu, lakini ameshapata mafanikio akiwa na Simba pia aliwahi kucheza soka la kulipwa nje, hivyo vyote vitatuongezea kitu sisi lakini pia wachezaji vijana watapata muda wa kujifunza kutoka kwake,” alisema Malale.
Pia Malale alisema mechi zilizopita walikuwa na mapungufu makubwa ya winga hivyo ujio wa mkongwe huyo umewasaidia kuwa na nafasi pana ya kubadili mifumo ya kucheza kulingana na mpinzani.
JKT Tanzania ipo nafasi ya 11 kwenye msimamo wa Ligi Kuu NBC, ikikusanya pointi 16 katika michezo 14 iliyocheza hadi sasa.

The post Kichuya kuipaisha JKT Tanzania first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/01/24/kichuya-kuipaisha-jkt-tanzania/feed/ 0
JKT Tanzania wahamia Chamazi https://www.greensports.co.tz/2023/10/18/jkt-tanzania-wahamia-chamazi/ https://www.greensports.co.tz/2023/10/18/jkt-tanzania-wahamia-chamazi/#respond Wed, 18 Oct 2023 05:15:42 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=8129 Na mwandishi wetuHatimaye timu ya JKT Tanzania imeeleza kuwa kwa sasa kuutumia Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam kwa ajili ya mechi zao za nyumbani za Ligi Kuu NBC.Hayo yameelezwa Jumanne hii na Ofisa Habari wa JKT, Masau Bwire baada ya awali uwanja wao wa nyumbani wa CCM Kambarage uliopo Shinyanga kufungiwa […]

The post JKT Tanzania wahamia Chamazi first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Hatimaye timu ya JKT Tanzania imeeleza kuwa kwa sasa kuutumia Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam kwa ajili ya mechi zao za nyumbani za Ligi Kuu NBC.
Hayo yameelezwa Jumanne hii na Ofisa Habari wa JKT, Masau Bwire baada ya awali uwanja wao wa nyumbani wa CCM Kambarage uliopo Shinyanga kufungiwa na Bodi ya Ligi kwa kukosa vigezo baada ya kutumika kwenye mechi mbili za ligi pekee.
“Tulipokea barua Oktoba 3, mwaka huu juu ya kufungwa kwa uwanja wetu kutokana na kukosa vigezo vilivyoelezwa katika muonekano kwa watazamaji, eneo la kuchezea na sehemu nyingine, sasa uwanja uko kwenye matengenezo kwa hiyo tumechagua uwanja wetu wa nyumbani kama tulivyoelekezwa.

“Na chaguo la timu limekuwa Uwanja wa Azam Complex na tayari ratiba imepangwa na inaonesha hivyo kwamba tutatumia uwanja huo wakati huu ambao Kambarage sasa upo kwenye matengenezo na marekebisho kulingana na namna ilivyoelekezwa,” alisema Bwire.


Katika mechi mbili ilizocheza Uwanja wa Kambarage, JKT ilipata sare ya bao 1-1 dhidi ya Kagera Sugar kabla ya kuichapa Mashujaa bao 1-0.
Timu hiyo ambayo ipo nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi saba, pia ilipata ushindi katika mechi na Namungo.

The post JKT Tanzania wahamia Chamazi first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/10/18/jkt-tanzania-wahamia-chamazi/feed/ 0
JKT waanza marekebisho CCM Kambarage https://www.greensports.co.tz/2023/10/06/jkt-waanza-marekebisho-ccm-kambarage/ https://www.greensports.co.tz/2023/10/06/jkt-waanza-marekebisho-ccm-kambarage/#respond Fri, 06 Oct 2023 07:24:26 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=7967 Na mwandishi wetuTimu ya JKT Tanzania imeanza haraka marekebisho ya uwanja wake wa CCM Kambarage, ikisema inapambana kuhakikisha unafunguliwa kabla ya mchezo wao wa nyumbani unaofuata.Akizungumza na GreenSports, Ofisa Habari wa JKT, Masau Bwire (pichani) alisema kwamba walianza zoezi la kuirekebisha Kambarage mapema baada ya juzi kupokea barua kutoka Bodi ya Ligi ya kufungwa kwa […]

The post JKT waanza marekebisho CCM Kambarage first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Timu ya JKT Tanzania imeanza haraka marekebisho ya uwanja wake wa CCM Kambarage, ikisema inapambana kuhakikisha unafunguliwa kabla ya mchezo wao wa nyumbani unaofuata.
Akizungumza na GreenSports, Ofisa Habari wa JKT, Masau Bwire (pichani) alisema kwamba walianza zoezi la kuirekebisha Kambarage mapema baada ya juzi kupokea barua kutoka Bodi ya Ligi ya kufungwa kwa uwanja huo kwa kutokidhi vigezo.
“Tunapambana kuona namna ya kushughulikia haya mapungufu. Tumeshaanza kwa nguvu kubwa kufanya marekebisho tukiamini mpaka kufikia siku ya mchezo wa nyumbani Oktoba 28 dhidi ya Tabora United tutakuwa tayari,” alisema Bwire.
Bwire alisema wanafahamu kikanuni uwanja unakaguliwa na kupitishwa siku saba kabla ya mechi, hivyo wanapambana kuhakikisha unakamilika mapema na kuja kufanyiwa ukaguzi na kuthibitishwa uwanja wao huo kabla ya Oktoba 21.
Uwanja wa Kambarage ulifungiwa na Bodi ya Ligi baada ya mchezo wao wa hivi karibuni dhidi ya Mashujaa ambao JKT walishinda kwa bao 1-0.
Uwanja huo ulifungiwa kwa madai ya kutokuwa tambarare na kukosa nyasi eneo la kuchezea, ukikosa vigezo vya kanuni na sheria za mpira wa miguu.

The post JKT waanza marekebisho CCM Kambarage first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/10/06/jkt-waanza-marekebisho-ccm-kambarage/feed/ 0
Yanga yaendeleza dozi ya tano tano https://www.greensports.co.tz/2023/08/30/yanga-yaendeleza-dozi-ya-tano-tano/ https://www.greensports.co.tz/2023/08/30/yanga-yaendeleza-dozi-ya-tano-tano/#respond Wed, 30 Aug 2023 08:25:06 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=7582 Na mwandishi wetuYanga imeendelea kutoa dozi ya tano tano katika Ligi Kuu NBC baada ya kuichapa JKT Tanzania 5-0 katika mechi iliyopigwa Jumanne hii usiku kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Dar es Salaam.Hii ni mechi ya tatu ya mashindano kwa Yanga kutoka na ushindi wa mabao matano na ya pili kwa Ligi Kuu NBC, […]

The post Yanga yaendeleza dozi ya tano tano first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Yanga imeendelea kutoa dozi ya tano tano katika Ligi Kuu NBC baada ya kuichapa JKT Tanzania 5-0 katika mechi iliyopigwa Jumanne hii usiku kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Dar es Salaam.
Hii ni mechi ya tatu ya mashindano kwa Yanga kutoka na ushindi wa mabao matano na ya pili kwa Ligi Kuu NBC, matokeo yanayotoa picha ya namna mabingwa hao watetezi wa ligi hiyo walivyojipanga kulitetea taji lao msimu huu.
Yanga tayari imefanya hivyo katika mechi nyingine ya ligi hiyo dhidi ya KMC iliyoichapa 5-0 lakini pia imeipa kipigo cha 5-1 Asas ya Djibout katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Ushindi dhidi ya JKT umeanza kuwapa jeuri mashabiki wa Yanga ambao katika vijiwe vyao wameanza kuitaja Simba kwamba ijiandae kukutana na dozi kama hiyo timu hizo zitakapokutana mapema mwezi Novemba.
Yanga sasa imefikisha pointi sita katika Ligi Kuu NBC sawa na Simba lakini Yanga inashika usukani ikiwa na faida ya mabao ya kufunga, ina mabao 10 wakati Simba ina mabao manne ikiwa nafasi ya tatu na Azam inashika nafasi ya pili ikiwa na mabao sita, timu zote hizo zina pointi sita katika mechi mbili.
JKT licha ya kupewa kipigo kikali na Yanga, katika kipindi cha kwanza hawakuonesha dalili zozote za kukutana na kipigo kikubwa namna hiyo kwa jinsi walivyouanza mchezo wakijaribu kuzuia na kukabiliana na kasi ya Yanga.
Mambo hata hivyo yalianza kuwaaribikia mwishoni mwa kipindi cha kwanza walipoanza kupoteana na kumruhusu Stephanie Aziz Ki kuipatia Yanga bao la kwanza kwa mpira wa adhabu muda mfupi kabla ya timu kwenda mapumziko.
Mambo yaliendelea kuwaharibikia JKT dakika 10 baada ya kuanza kipindi cha pili walipofungwa bao la tatu mfungaji akiwa ni Nickson Kibabage.
Dakika 10 baada ya Kibabage kufunga bao la pili, JKT walijikuta wakiokota mpira katika nyavu zao kwa bao la tatu lililofungwa na Yao Kouasi.
Karamu ya mabao ya Yanga ilihimitishwa na Maxi Nzengeli aliyefunga mabao mawili katika dakika za 79 na 88 na kukamilisha dozi ya mabao matano kwa Yanga.

The post Yanga yaendeleza dozi ya tano tano first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/08/30/yanga-yaendeleza-dozi-ya-tano-tano/feed/ 0