Kimataifa - Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz Michezo na Burudani ni zaidi ya ajira Wed, 23 Apr 2025 17:18:13 +0000 en-GB hourly 1 https://wordpress.org/?v=6.8 https://www.greensports.co.tz/wp-content/uploads/2021/09/cropped-WhatsApp-Image-2021-09-02-at-13.12.19-1-32x32.jpeg Kimataifa - Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz 32 32 Mo amshukuru Rais Samia https://www.greensports.co.tz/2025/04/23/mo-amshukuru-rais-samia/ https://www.greensports.co.tz/2025/04/23/mo-amshukuru-rais-samia/#respond Wed, 23 Apr 2025 17:14:27 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=13309 Na mwandishi wetuRais wa klabu ya Simba, Mohammed Dewji ‘Mo’ amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa msaada wake katika klabu hiyo inayoshiriki Kombe la Shirikisho Afrika.Taarifa ya Mo iliyopatikana leo Jumatano Aprili 23, 2025 ilielezea shukrani za klabu hiyo kwa mchango wa usafiri na malazi kuelekea mchezo wao wa […]

The post Mo amshukuru Rais Samia first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Rais wa klabu ya Simba, Mohammed Dewji ‘Mo’ amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa msaada wake katika klabu hiyo inayoshiriki Kombe la Shirikisho Afrika.
Taarifa ya Mo iliyopatikana leo Jumatano Aprili 23, 2025 ilielezea shukrani za klabu hiyo kwa mchango wa usafiri na malazi kuelekea mchezo wao wa marudiano dhidi ya Stellenbosch ya Afrika Kusini.
Simba itarudiana na timu hiyo Jumapili ijayo katika mechi ya pili ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho ikiwa na faida ya ushindi wa bao 1-0 ilioupata Jumapili iliyopita kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Katika taarifa hiyo, Mo ambaye pia ni mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa klabu hiyo, alisema Simba inatambua na kuthamini juhudi za Rais Samia katika sekta ya michezo nchini hasa mchezo wa soka.
Mo alitolea mfano wa goli la mama ambalo huhusisha zawadi ya Sh milioni 10 kwa kila goli linalofungwa kwenye mechi za kimataifa akisema jambo hilo limekuwa chanzo cha hamasa na ari kwa wachezaji na mashabiki.
Sambamba na Rais Samia, Mo pia alitoa shukrani zake kwa Wizara ya Fedha pamoja na Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo kwa namna wizara hizo zilivyoratibu safari ya Simba.
Mo pia alitoa shukran kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Shirika la Reli Tanzania (TRL).
Iwapo Simba itafanikiwa kuitoa Stellenbosch itaumana katika fainali na mshindi wa mechi kati ya RS Berkane na CS Constantine.

The post Mo amshukuru Rais Samia first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/04/23/mo-amshukuru-rais-samia/feed/ 0
Ancelotti: Lolote lawezekana https://www.greensports.co.tz/2025/04/22/ancelotti-lolote-lawezekana/ https://www.greensports.co.tz/2025/04/22/ancelotti-lolote-lawezekana/#respond Tue, 22 Apr 2025 15:36:42 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=13305 Madrid, HispaniaKocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti amezungumzia mambo yake ya baadaye katika klabu hiyo akisisitiza lolote linawezekana wakati huu timu yake ikichuana na Barcelona kuwania mataji ya La Liga na Kombe la Mafalme.Ancelotti amekuwa katika kipindi kigumu tangu timu yake itolewe na Arsenal kwenye hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa […]

The post Ancelotti: Lolote lawezekana first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
Madrid, Hispania
Kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti amezungumzia mambo yake ya baadaye katika klabu hiyo akisisitiza lolote linawezekana wakati huu timu yake ikichuana na Barcelona kuwania mataji ya La Liga na Kombe la Mafalme.
Ancelotti amekuwa katika kipindi kigumu tangu timu yake itolewe na Arsenal kwenye hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kipigo cha jumla cha mabao 5-1.
Real Madrid imeachwa na Barcelona kwa tofauti ya pointi nne katika La Liga zikiwa zimebaki mechi sita kabla ya kufikia tamati ya kwa ligi hiyo, pia Jumamosi itakuwa na kibarua kigumu dhidi ya timu hiyo kwenye Kombe la Mfalme.
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari leo Jumanne, Aprili 22, 2025 kabla ya kuumana na Getafe kwenye La Liga, Ancelotti alisema timu yake inaweza kubeba mataji yote hayo mawili.
Kuhusu presha ya nafasi yake ya ukocha, Ancelotti ambaye mkataba wake na Real Madtid unaishia 2026 alisema hali hiyo na yote yanayoendelea ni kama kichocheo kwake.
Kocha huyo badala yake aliwapa mashabiki wa timu hiyo habari njema kuhusu mshambuliaji Kylian Mbappe aliyeumia enka akisema anaendelea vizuri na anaweza kucheza mechi ya fainali ya Kombe la Mfalme.

“Katika soka lolote linawezekana, je mnashangazwa na mambo yote yanayotokea, hakuna kinachonishangaza mimi, kama ninavyosema wakati wote, naipenda hii kazi, nilipenda nilivyokuwa hapa awamu ya kwanza (2013 hadi 2015) napenda hii awamu ya pili kuanzia 2021 na nataka awamu hii iendelee kadri inavyowezekana,” alisema Ancelotti.


Ancelotti pia alisema kwamba ikifika siku ambayo kazi yake itafikia mwisho atakuwa mwenye kushukuru na kuvua kofia yake katika klabu hiyo kwani hiyo ndiyo hali halisi.
Kocha huyo Mtaliano amejijengea heshima kwa kuiwezesha Real Madrid kubeba mataji mawili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya lakini msimu huu umekuwa mgumu huku habari ya kutimuliwa kwake ikipamba moto siku hadi siku.

The post Ancelotti: Lolote lawezekana first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/04/22/ancelotti-lolote-lawezekana/feed/ 0
Yanga yaicharaza Fountain Gate mabao 4-0 https://www.greensports.co.tz/2025/04/21/yanga-yaicharaza-fountain-gate-mabao-4-0/ https://www.greensports.co.tz/2025/04/21/yanga-yaicharaza-fountain-gate-mabao-4-0/#respond Mon, 21 Apr 2025 18:56:01 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=13296 Na mwandishi wetuYanga imeipa kipigo cha mabao 4-0 Fountain Gate FC katika mechi ya Ligi Kuu NBC iliyopigwa leo Jumatatu Aprili 21, 2025 kwenye Uwanja wa Tanzanite, Kwaraa mjini Manyara.Yanga ilianza kuandika bao la kwanza katika dakika ya 38 lililofungwa na Clement Mzize ambaye aliyatumia vizuri makosa ya kipa wa Fountain Gate, John Noble kuipatia […]

The post Yanga yaicharaza Fountain Gate mabao 4-0 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
Na mwandishi wetu
Yanga imeipa kipigo cha mabao 4-0 Fountain Gate FC katika mechi ya Ligi Kuu NBC iliyopigwa leo Jumatatu Aprili 21, 2025 kwenye Uwanja wa Tanzanite, Kwaraa mjini Manyara.
Yanga ilianza kuandika bao la kwanza katika dakika ya 38 lililofungwa na Clement Mzize ambaye aliyatumia vizuri makosa ya kipa wa Fountain Gate, John Noble kuipatia Yanga bao.
Bao la pili la Yanga lilifungwa na Stephane Aziz Ki ambaye kama ilivyo kwa Mzize naye aliyatumia makosa ya kipa Noble aliyejichanganya wakati akiokoa mpira ulioelekezwa langoni mwake badala yake akamrudishia mfungaji.
Kipindi cha pili kiliendelea kuwa kigumu kwa Fountain Gate baada ya kupachikwa bao la tatu mfungaji akiwa Mzize katika dakika ya 69 akiitumia pasi ya Jonathan Ikangalombo.
Mzize ambaye pia aliibuka mchezaji bora wa mechi hiyo, bao hilo lina maana kubwa kwake kwani sasa amefikisha mabao 13 katika ligi hivyo kuwa kinara akifuatiwa na Jean Ahoua wa Simba mwenye mabao 12 sawa na Prince Dube wa Yanga.
Clatous Chama alikamilisha bao la nne kwa Yanga katika dakika ya 89 akifunga kwa mpira wa adhabu iliyotolewa baada ya Mtenje Albano kumchezea rafu Mzize nje kidogo ya eneo la penalti.
Ushindi huo unaifanya Yanga kuendelea kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi kwa kufikisha pointi 70 katika mechi 26 ikiiacha Simba nafasi ya pili ikiwa na pointi 57 katika mechi 22.

The post Yanga yaicharaza Fountain Gate mabao 4-0 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/04/21/yanga-yaicharaza-fountain-gate-mabao-4-0/feed/ 0
Papa Francis afariki, mechi Serie A zaahirishwa https://www.greensports.co.tz/2025/04/21/papa-francis-afariki-mechi-serie-a-zaahirishwa/ https://www.greensports.co.tz/2025/04/21/papa-francis-afariki-mechi-serie-a-zaahirishwa/#respond Mon, 21 Apr 2025 12:21:12 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=13289 Vatican City, VaticanMechi nne za ligi kuu ya soka ya Italia maarufu, Serie A zimeahirishwa kufuatia kifo cha Papa Francis ambaye amefariki leo Jumatatu Aprili 21 akiwa na umri wa miaka 88.Taarifa ya kifo hicho imetangazwa rasmi na mamlaka za Vatican leo ikiwa ni siku kadhaa zimepita baada ya kiongozi huyo mkuu wa Kanisa Katoliki […]

The post Papa Francis afariki, mechi Serie A zaahirishwa first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
Vatican City, Vatican
Mechi nne za ligi kuu ya soka ya Italia maarufu, Serie A zimeahirishwa kufuatia kifo cha Papa Francis ambaye amefariki leo Jumatatu Aprili 21 akiwa na umri wa miaka 88.
Taarifa ya kifo hicho imetangazwa rasmi na mamlaka za Vatican leo ikiwa ni siku kadhaa zimepita baada ya kiongozi huyo mkuu wa Kanisa Katoliki duniani kutoka hospitali alikolazwa kwa takriban wiki tano.
Kifo hicho kimekuja ikiwa ni siku moja baada ya kiongozi huyo kuonekana Jumapili ya Pasaka akiwa kwenye kiti cha magurudumu na kuwabariki waumini wa kikristo.
Mechi ambazo zimeahirishwa ni kati ya Torino dhidi ya Udinese, Cagliari na Fiorentina, Genoa na Lazio na Parma dhidi ya Juventus.
Bodi inayosimamia soka la Italia imetangaza uamuzi huo na kuahidi kuzipangia siku nyingine mechi hizo badala ya leo Jumatatu ambayo kwa kawaida ni siku mapumziko nchini Italia.
Papa Francis aliteuliwa kuongoza kanisa katoliki duniani mwaka 2013 akichukua nafasi ya Papa Benedict XVI aliyeushtua ulimwengu baada ya kuamua kung’atuka katika cheo hicho.
Kihistoria Papa Francis anatokea Argentina, alifahamika kwa kipindi kirefu kuwa mpenda soka na wakati akiwa kijana mdogo alikuwa shabiki wa timu ya San Lorenzo ya Argentina
Kutokana na msiba huo mkubwa klabu kadhaa za soka nchini Italia zimetuma salamu za rambirambi mojawapo ikiwa na klabu ya Roma ambayo imeeleza kuwa jiji lote la Roma na dunia kwa ujumla imesikitishwa na msiba huo.

“Imani yake, uvumilivu, ujasiri na kujitoa kwake ni mambo yaliyogusa mioyo ya mamilioni ya watu na kumfanya awe kielelezo cha kiroho katika zama zetu,” ilieleza taarifa ya klabu ya Roma.

The post Papa Francis afariki, mechi Serie A zaahirishwa first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/04/21/papa-francis-afariki-mechi-serie-a-zaahirishwa/feed/ 0
Simba yailaza Stellenbosch 1-0 https://www.greensports.co.tz/2025/04/20/simba-yailaza-stellenbosch-1-0/ https://www.greensports.co.tz/2025/04/20/simba-yailaza-stellenbosch-1-0/#respond Sun, 20 Apr 2025 16:23:52 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=13285 Na mwandishi wetuSimba imeanza vizuri mechi ya kwanza ya nusu fainali Kombe la Shirikisho Afrika kwa kuilaza Stellenbosch ya Afrika Kusini bao 1-0 kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar, leo Jumapili, Aprili 20, 2025.Bao pekee la Simba lilipatikana dakika ya 45 mfungaji akiwa ni Jean Ahoua kwa mpira wa adhabu uliokwenda moja kwa moja hadi wavuni […]

The post Simba yailaza Stellenbosch 1-0 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
Na mwandishi wetu
Simba imeanza vizuri mechi ya kwanza ya nusu fainali Kombe la Shirikisho Afrika kwa kuilaza Stellenbosch ya Afrika Kusini bao 1-0 kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar, leo Jumapili, Aprili 20, 2025.
Bao pekee la Simba lilipatikana dakika ya 45 mfungaji akiwa ni Jean Ahoua kwa mpira wa adhabu uliokwenda moja kwa moja hadi wavuni na kumshinda kipa Oscarine Masuluke.
Bao hilo liliibua utata baada ya wachezaji wa Stellenbosch kugomea wakidai wachezaji wa Simba waliotea hivyo kulazimika kutumia VAR kabla ya kutangazwa kuwa ni bao halali.
Simba waliutawala vyema mchezo huo kwa wachezaji wake kuonesha ubora wao wa kutengeneza nafasi nyingi za kufunga lakini tatizo la umaliziaji liliendelea kuiathiri timu hiyo.
Moja ya nafasi ya mapema Simba kuipata ni pale Kibu Dennis alipoambaa na mpira akiwa upande wa kushoto wa Stellenbosch na kupiga krosi ambayo Shomari Kapombe alibinuka vyema na kuupiga mpira staili ya tikitaka lakini mpira huo ulipaa nje ya lango.
Kasi ya Simba iliendelea na katika dakika ya 30, Ahoua aliunasa mpira na kumuunganishia Elly Mpanzu ambaye aliukokota kidogo kabla ya kufumua shuti kali la mguu wa kushoto ambalo liliokolewa vyema na kipa wa Stelenbosch.
Baada ya kuona kasi ya Simba inawazidi wachezaji wa Stellenbosch walianza kucheza rafu na mwamuzi kulazimika kuwapa kadi za njano Enyimnaya na Jabaar kwa kuwachezea rafu Mpanzu na Kibu.
Dakika tano baadaye Stellenbosch nao walijibu shambulizi baada ya kipa kuokoa mpira wa kona na kuwasaidia kutengeneza shambulizi lililoelekezwa upande wa kulia wa Simba.
Shambulizi hilo hata hivyo lilikwama baada ya Zimbwe Jr aliyehamia upande huo kumdhibiti mchezaji wa Stellenbosch wakati huo Kapombe anayecheza zaidi upande wa kulia akiwa amehamia upande wa kushoto ambao anacheza Zimbwe.
Kipindi cha pili, Stellenbosch walikianza kwa kufanya mabadiliko kadhaa yaliyoonekana kuwapa uhai na kumuweka katika wakati mgumu kipa Musa Camara wa Simba.


Simba nao walibadilika na kuanza kulisakama lango la wapinzani wao kwa kutengeneza nafasi nyingi ambazo hata hivyo walikwama katika kuzitumia nafasi hizo.
Nafasi mojawapo ya mwisho ni ile waliyoipata ikiwa imebaki dakika moja katika dakika sita za nyongeza baada ya Ahoua kuunganishiwa pasi ya chinichini na Mpanzu naye kumlamba chenga kipa Masuluke lakini shuti alilopiga la mguu wa kushoto lilitoka nje.
Katika mechi hiyo timu zote zilifanya mabadiliko kadhaa, Stellenbosch wakiwatoa De Jong na kumuingiza Bans na Jabaar ambaye nafasi yake aliingia Palace.
Simba iliwatoa Zimbwe na kuingia Valentine Nouma, Kibu akaingia Joshua Mutale, Deborah Fernandes akaingia kuchukua nafasi ya Chamaou Karabou wakati Ateba akaingia kuchukua nafasi ya Steven Mukwala.
Timu hizo zinatarajia kurudiana Aprili 27 nchini Afrika Kusini, mechi ambayo mshindi atajikatia moja kwa moja tiketi ya kucheza mechi ya fainali ya michuano hiyo dhidi ya mshindi wa mechi ya nusu fainali nyingine kati ya CS Constantine na RS Berkane.

The post Simba yailaza Stellenbosch 1-0 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/04/20/simba-yailaza-stellenbosch-1-0/feed/ 0
Ancelotti: Real Madrid tupo shwari https://www.greensports.co.tz/2025/04/20/ancelotti-real-madrid-tupo-shwari/ https://www.greensports.co.tz/2025/04/20/ancelotti-real-madrid-tupo-shwari/#respond Sun, 20 Apr 2025 08:41:47 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=13283 Madrid, HispaniaKocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti amekana kuwapo mgogoro wa chinichini katika klabu hiyo huku akiweka wazi kwamba mambo yake ya baadaye yatajadiliwa mwisho wa msimu huu.Nafasi ya Ancelotti imekuwa mjadala katika siku za karibuni hasa baada ya timu hiyo kuishia hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kutolewa na Arsenal.Real […]

The post Ancelotti: Real Madrid tupo shwari first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Madrid, Hispania
Kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti amekana kuwapo mgogoro wa chinichini katika klabu hiyo huku akiweka wazi kwamba mambo yake ya baadaye yatajadiliwa mwisho wa msimu huu.
Nafasi ya Ancelotti imekuwa mjadala katika siku za karibuni hasa baada ya timu hiyo kuishia hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kutolewa na Arsenal.
Real Madrid ikiwa nyumbani Santiago Bernabéu Jumatano iliyopita ililala kwa mabao 2-1 mbele ya Arsenal hiyo ni badaa ya kulala ugenini kwa mabao 3-0 na hivyo kutolewa katika michuano hiyo kwa jumla ya mabao 5-1.
Kocha huyo Mtaliano tangu ajiunge kwa mara ya pili na Real Madrid mwaka 2021 ameweza kujiwekea rekodi nzuri ya kubeba mataji ya La Liga mara mbili na Ligi ya Mabingwa Ulaya mara mbili.
Msimu huu hata hivyo umekuwa mgumu kwa Ancelotti, timu yake imetolewa kwenye ligi ya mabingwa, michuano ambayo ina hadhi ya juu Ulaya na dunia kote wakati huo huo inahaha kubeba taji la La Liga.
Real Madrid msimu huu imepoteza mechi kadhaa katika namna ambayo haikutarajiwa, wiki ijayo itacheza mechi ya fainali Kombe la Mfalme, taji inalotakiwa ilipiganie walau itoke na kitu msimu huu.

“Nimezungumza na wachezaji na viongozi, sote tunafikiria katika mtazamo mmoja ambao ni kuendelea kupigania mataji yaliyobaki,” alisema Ancelotti.


Ancelotti alisisitiza kwamba hakuna mgogoro wowote na klabu na kwamba wote wapo katika safari moja na yeyote anayesema kuna mgogoro na klabu au rais (Florentino Perez) huyo hasemi ukweli.
Mkataba wa Ancelotti na Real Madrid unafikia ukomo mwaka 2026 ingawa kumekuwapo habari kwamba klabu hiyo inataka kuachana na kocha huyo ambaye pia inadaiwa anawindwa kwa udi na uvumba kwenye timu ya taifa ya Brazil.

The post Ancelotti: Real Madrid tupo shwari first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/04/20/ancelotti-real-madrid-tupo-shwari/feed/ 0
Adhabu ya Sinner yamshangaza Serena Williams https://www.greensports.co.tz/2025/04/19/adhabu-ya-sinner-yamshangaza-serena-williams/ https://www.greensports.co.tz/2025/04/19/adhabu-ya-sinner-yamshangaza-serena-williams/#respond Sat, 19 Apr 2025 19:30:33 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=13278 New York, MarekaniNyota wa mchezo wa tenisi wa Marekani, Serena Williams (pichani) amesema kama yeye angekutwa na hatia ya kutumia dawa za kuongeza nguvu angefungiwa miaka 20 na kunyang’anywa tuzo zote za Grand Slams alizobeba.Serena alitoa kauli hiyo akionekana kushangazwa na adhabu aliyopewa bingwa namba moja wa mchezo huo duniani kwa upande wa wanaume, Jannik […]

The post Adhabu ya Sinner yamshangaza Serena Williams first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

New York, Marekani
Nyota wa mchezo wa tenisi wa Marekani, Serena Williams (pichani) amesema kama yeye angekutwa na hatia ya kutumia dawa za kuongeza nguvu angefungiwa miaka 20 na kunyang’anywa tuzo zote za Grand Slams alizobeba.
Serena alitoa kauli hiyo akionekana kushangazwa na adhabu aliyopewa bingwa namba moja wa mchezo huo duniani kwa upande wa wanaume, Jannik Sinner ambaye alikutwa na hatia ya kutumia dawa za kuongeza nguvu na Februari mwaka jana akafungiwa miezi mitatu.
Sinner alikubali kufungiwa miezi mitatu baada ya makubaliano na Wada, taasisi ya kimataifa inayojihusisha kukabiliana na matumizi ya dawa za kuongeza nguvu.
Wada walifikia hatua hiyo baada ya kupinga maamuzi ya tume huru iliyoamua kumfutia Sinner kosa hilo licha ya kupimwa mara mbili na kubainika kuwa alikuwa akitumia dawa hizo.
Serena alisema anampenda Sinner kwani ni shujaa katika mchezo wa tenisi na ingawa yeye amekuwa akishushwa chini sana lakini kwa upande wake hapendi kumshusha mtu hasa kwa kuwa mchezo wa tenisi kwa wanaume unamhitaji Sinner.

“Hata hivyo ukweli ni kwamba ningekuwa mimi ningefungiwa miaka 20 na kunyang’anywa tuzo zangu zote za Grand Slams,” alisema Serena ambaye amewahi kushinda Grand Slams kwa mara 23.


Serena, 43, alisema kwamba wakati wote katika mchezo wa tenisi amekuwa makini kwa kila kitu anachokiingiza mwilini mwake kwa hofu ya kuingia kwenye matatizo.
Katika hali ya dhihaka, Serena alisema kwamba jambo dogo tu lingeweza hata kumpeleka jela na kusikika kila kona katika namna nyingine.

The post Adhabu ya Sinner yamshangaza Serena Williams first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/04/19/adhabu-ya-sinner-yamshangaza-serena-williams/feed/ 0
Arteta amkumbuka Pep kabla ya kuitoa Real Madrid https://www.greensports.co.tz/2025/04/17/arteta-amkumbuka-pep-kabla-ya-kuitoa-real-madrid/ https://www.greensports.co.tz/2025/04/17/arteta-amkumbuka-pep-kabla-ya-kuitoa-real-madrid/#respond Thu, 17 Apr 2025 09:53:51 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=13269 Madrid, HispaniaBaada ya kuitoa Real Madrid katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na kutua nusu fainali kwa ushindi wa jumla wa mabao 5-1, kocha wa Arsenal, Mikel Arteta amemkumbuka mwalimu wake Pep Guardiola.Arsenal jana Jumatano ilifuzu hatua ya nusu fainali kwa kuichapa Real Madrid mabao 2-1 katika mechi ya pili ya robo fainali […]

The post Arteta amkumbuka Pep kabla ya kuitoa Real Madrid first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
Madrid, Hispania
Baada ya kuitoa Real Madrid katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na kutua nusu fainali kwa ushindi wa jumla wa mabao 5-1, kocha wa Arsenal, Mikel Arteta amemkumbuka mwalimu wake Pep Guardiola.
Arsenal jana Jumatano ilifuzu hatua ya nusu fainali kwa kuichapa Real Madrid mabao 2-1 katika mechi ya pili ya robo fainali baada ya kushinda kwa mabao 3-0 katika mechi ya kwanza.
Real Madrid ikiwa nyumbani Santiago Bernabeu ikilala kwa mabao ya Bukayo Saka ambaye pia alikosa penalti na Gabriel Martinelli aliyefunga la pili wakati bao pekee la Real Madrid likifungwa na Vinicius Junior.
Akimzungumzia Guardiola, Arteta alisema alimpigia simu mapema kocha huyo ambaye alidai anaendelea kufurahia ukaribu wao kikazi baada ya kufanya naye kazi Man City kwa miaka mitatu.

“Nilimpigia simu mapema (jana Jumatano) kwa sababu niko hapa na yeye namshukuru, nikiwa mchezaji na baadaye kocha amekuwa akinipa hamasa, nimekuwa na miaka minne mizuri pamoja naye na nitaendelea kumshukuru wakati wote,” alisema Arteta.


Kwa ushindi huo, Arsenal sasa inasubiri kuumana na PSG ya Ufaransa katika mechi ya kwanza ya nusu fainali itakayopigwa Aprili 29.
Akizungumzia mambo yajayo ya timu yake katika hatua waliyofikia, Arteta alisema kwa sasa wataendeleza wimbi la ushindi kwa sababu ari yao ipo vile vile.
“Kwa sasa tunatakiwa kuendelea kufanya tulichokifanya (ushindi) kwa sababu nadhani bado tuna ari ile ile,” alisema Arteta.
Arteta alisema jukumu lao ni kuwafanya watu wao wawe na furaha na anaamini watu hao wanajivunia wachezaji na timu na kilichobaki sasa ni wao kuangalia mambo ya mbele zaidi ya walipofikia sasa.
Naye Saka aliyepiga penalti kwa staili ya panenka na kukosa, alisema jambo hilo hutokea na kwamba alijaribu kufanya kitu tofauti lakini ikashindikana baada ya kipa Thibaut Courtois kuwa makini.
Kwa Arsenal hii inakuwa mara ya kwanza kufikia nusu fainali ya ligi ya mabingwa tangu mwaka 2009 wakati kwa Real Madrid wanakosa hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2020.

The post Arteta amkumbuka Pep kabla ya kuitoa Real Madrid first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/04/17/arteta-amkumbuka-pep-kabla-ya-kuitoa-real-madrid/feed/ 0
Marcelo aipasha Arsenal, ‘Real Madrid ni Real Madrid’ https://www.greensports.co.tz/2025/04/15/marcelo-aiambia-arsenal-real-madrid-ni-real-madrid/ https://www.greensports.co.tz/2025/04/15/marcelo-aiambia-arsenal-real-madrid-ni-real-madrid/#respond Tue, 15 Apr 2025 19:14:43 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=13256 Mexico City, MexicoBeki wa zamani wa Real Madrid, Marcelo amesema timu hiyo si ya kufutwa moja kwa moja wakati huu ikiwa na kibarua kigumu cha kupindua meza katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.Real Madrid ina kazi ngumu ya kuupanda mlima baada ya kulala kwa mabao 3-0 mbele ya Arsenal Jumatano iliyopita kwenye Uwanja wa Enmirates katika […]

The post Marcelo aipasha Arsenal, ‘Real Madrid ni Real Madrid’ first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
Mexico City, Mexico
Beki wa zamani wa Real Madrid, Marcelo amesema timu hiyo si ya kufutwa moja kwa moja wakati huu ikiwa na kibarua kigumu cha kupindua meza katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Real Madrid ina kazi ngumu ya kuupanda mlima baada ya kulala kwa mabao 3-0 mbele ya Arsenal Jumatano iliyopita kwenye Uwanja wa Enmirates katika mechi ya kwanza ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Marceloa ambaye ana rekodi ya kubeba mataji matano ya ligi ya mabingwa akiwa na Real Madrid anaamini hakuna jukumu ambalo ni kubwa zaidi kwa klabu hiyo.
“Huwezi kuifuta moja kwa moja Real Madrid, ingawa mabao matatu ni mengi lakini wakati wote huwa naifikiria Real Madrid na nina imani kubwa kwa timu hiyo kwamba inaweza kujibu mapigo, Real Madrid ni Real Madrid na inaweza kushinda,” alisema Marcelo.
Marcelo ambaye kwa sasa yuko nchini Mexico akijiandaa kucheza mechi ya El Clasico ambayo itahusisha wachezaji wa zamani wa Real Madrid na Barcelona, alisema katika mechi ya marudiano, Real Madrid itakuwa na faida ya kuwa nyumbani kwenye dimba la Bernabeu.

“Mechi ya marudiano itakuwa Bernabéu, mashabiki wataiunga mkono kwa nguvu na wachezaji wanaamini inawezekana, ingawa ni kweli hatujui nini kitatokea bali tuna imani na Real Madrid kujibu mapigo,” alisema Marcelo.

Marcelo aliongeza kwa kusema kuwa anadhani ushindi upo katika damu za wachezaji wa Real Madrid na ni kama vile ni jambo ambalo wanafundishwa mara tu wanapoanza kuvaa jezi ya timu hiyo.
“Nafikiri mara tu tunapojiunga na Real Madrid tunafundishwa kutokata tamaa na hilo kwa wakati wote linakuwa kwenye damu zetu, ni kufanya juhudi, kuvumilia, kujitoa kila siku pamoja na kuungwa mkono na mashabiki, ni kati ya vitu vinavyosaidia mambo yaende,” alisema Marcelo.

The post Marcelo aipasha Arsenal, ‘Real Madrid ni Real Madrid’ first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/04/15/marcelo-aiambia-arsenal-real-madrid-ni-real-madrid/feed/ 0
Wazo la timu 64 Kombe la Dunia lapingwa https://www.greensports.co.tz/2025/04/15/wazo-la-timu-64-kombe-la-dunia-lapingwa/ https://www.greensports.co.tz/2025/04/15/wazo-la-timu-64-kombe-la-dunia-lapingwa/#respond Tue, 15 Apr 2025 16:50:35 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=13249 Miami, MarekaniRais wa Shirkisho la Soka Marekani Kaskazini, Kati na Carribean (Concacaf), Victor Montagliani amepinga wazo la kiongozi wa Shirikisho la Soka Marekani Kusini (CONMEBOL), Alejandro Domínguez kutaka timu shiriki kwenye fainali za Kombe la Dunia 2030 ziwe 64.Domínguez aliwasilisha rasmi wazo la kupanua mashindano hayo kwenye kikao cha Baraza la Fifa kilichoendeshwa kwa mtandao […]

The post Wazo la timu 64 Kombe la Dunia lapingwa first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
Miami, Marekani
Rais wa Shirkisho la Soka Marekani Kaskazini, Kati na Carribean (Concacaf), Victor Montagliani amepinga wazo la kiongozi wa Shirikisho la Soka Marekani Kusini (CONMEBOL), Alejandro Domínguez kutaka timu shiriki kwenye fainali za Kombe la Dunia 2030 ziwe 64.
Domínguez aliwasilisha rasmi wazo la kupanua mashindano hayo kwenye kikao cha Baraza la Fifa kilichoendeshwa kwa mtandao akisisitiza timu shiriki ziongezwe kutoka 32 za sasa hadi kufikia 64.
“Kwa upande wetu Concacaf, tumeonesha tupo wazi kwa mabadiliko kwa kuunga mkono fainali za Kombe la Dunia kwa wanawake pamoja na muendelezo wa mabadiliko wa mashirikisho yetu kwa timu za wanaume na wanawake na mashindano ya klabu,” alisema Montagliani.
“Sidhani kama kuongeza timu katika fainali za Kombe la Dunia za wanaume kufikia 64 ni hatua sahihi kwa mashindano hayo pamoja na mustakabali mpana wa soka kwa mashindano ya timu za taifa, klabu, ligi na wachezaji,” alisema Montagliani.
Fifa itaanza kufanya majaribio ya mfumo wa timu 48 kwenye fainali za Kombe la Dunia 2026 lakini Domínguez alisisitiza haja ya kufanya zaidi ya hilo kwa kupanua wigo wa mashindano.
Naye Rais wa Umoja wa Vyama vya Soka Ulaya (Uefa) Aleksander Čeferin pia alionesha kutounga mkono hoja ya Domínguez akisema wazo la kuongeza idadi ya timu ni baya.

“Nafikiri ni wazo baya, si wazo zuri kwa fainali zenyewe za Kombe la Dunia, na pia si wazo zuri kwa timu zinazofuzu, kwa hiyo siungi mkono wazo hili, sijui limetokea wapi lakini ni hatari kwa sababu hatukufahamu lolote kabla ya wazo hili katika Baraza la Fifa,” alisema Ceferin.


Kwa upande wake Rais wa Shirikisho la Soka Asia, (AFC), Sheikh Salman bin Ibrahim alisisitiza kwamba ongezeko la idadi hiyo litahamasisha na kuwa mwanzo wa mvurugano.
“Kama jambo hili litakuwa wazi kwa mabadiliko maana yake ni kwamba mlango utakuwa wazi kwa kuongeza timu 64 lakini kuna mtu pia anaweza kuja na hoja ya kutaka idadi ya timu ifikie 132, mwisho itakuwaje? Ni mvurugano,” alisema Sheikh Salman.
Katika fainali za Kombe la Dunia 2026, majaribio yatafanyika kwa timu 48 ikiwa ni kwa mara ya kwanza katika historia ya fainali hizo zitakazochezwa Marekani, Mexico na Canada.

The post Wazo la timu 64 Kombe la Dunia lapingwa first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2025/04/15/wazo-la-timu-64-kombe-la-dunia-lapingwa/feed/ 0