Ntibazonkiza - Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz Michezo na Burudani ni zaidi ya ajira Sat, 22 Jun 2024 12:53:51 +0000 en-GB hourly 1 https://wordpress.org/?v=6.9.1 https://www.greensports.co.tz/wp-content/uploads/2021/09/cropped-WhatsApp-Image-2021-09-02-at-13.12.19-1-32x32.jpeg Ntibazonkiza - Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz 32 32 Namuona Ntibazonkiza, Coastal, Azam https://www.greensports.co.tz/2024/06/22/namuona-ntibazonkiza-coastal-azam/ https://www.greensports.co.tz/2024/06/22/namuona-ntibazonkiza-coastal-azam/#respond Sat, 22 Jun 2024 12:53:49 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=11407 Na Hassan KinguSimba imeachana na kiungo wake, Saido Ntibazonkiza ambaye habari za kuachwa kwake zimewekwa wazi kwenye mitandao ya kijamii katika siku za hivi karibuni.Baadhi yetu tayari tulilitambua hilo mapema hasa kwa jinsi baadhi ya mashabiki walivyoanza kumzungumzia vibaya mchezaji huyo kabla hata ya uamuzi wa kuachana naye kufikiwa.Uamuzi wa Simba hata hivyo haumaanishi kuwa […]

The post Namuona Ntibazonkiza, Coastal, Azam first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na Hassan Kingu
Simba imeachana na kiungo wake, Saido Ntibazonkiza ambaye habari za kuachwa kwake zimewekwa wazi kwenye mitandao ya kijamii katika siku za hivi karibuni.
Baadhi yetu tayari tulilitambua hilo mapema hasa kwa jinsi baadhi ya mashabiki walivyoanza kumzungumzia vibaya mchezaji huyo kabla hata ya uamuzi wa kuachana naye kufikiwa.
Uamuzi wa Simba hata hivyo haumaanishi kuwa Ntibazonkiza amefikia mwisho wa maisha yake ya soka, hapana, bado ana nafasi ya kuendelea kucheza soka tena la ushindani, iwe hapa Tanzania au nje ya Tanzania.
Sina uhakika na timu za nje lakini kwa hapa Tanzania naiona nafasi yake katika kikosi cha Coastal Union, naiona nafasi hiyo hiyo pia katika kikosi cha Azam FC.
Timu zote hizo mbili msimu ujao wa 2024-25 zitashiriki michuano ya klabu barani Afrika, Azam watashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika na Coastal watashiriki Kombe la Shirikisho Afrika kama ilivyo kwa Yanga.
Michuano hii ni mikubwa na sitoshangaa baadhi ya timu za hapa Tanzania zikiaga mapema kama ilivyokuwa miaka ya nyuma, kwa mantiki hiyo suala la kuimarisha vikosi kwa kuongza nguvu ni jambo muhimu.
Azam wamelitambua hilo na tayari wameanza na hapana shaka wanaendelea kukiimarisha kikosi chao, Coastal nao wanatakiwa kufanya hivyo na kwangu mtu wa kwanza ambaye wanaweza kumchukua ni Ntibazonkiza.
Ni mchezaji mbunifu ambaye anaweza kuongeza kitu katika eneo la kiungo, amedhihirisha hilo akiwa Simba na nadhani kwa Coastal anaweza kuwa mpishi mzuri na ambaye ataipa nguvu safu ya ushambuliaji ya timu hiyo.
Coastal wasione ajabu kumchukua Ntibazonkiza eti kwa kuwa ameachwa na Simba badala yake waangalie mahitaji ya kikosi chao, Yanga na Simba si mara moja wamekuwa wakiacha wachezaji na kuchukuliwa upande wa pili.
Mfano wa karibuni ni kwa Jonas Mkude ambaye Simba walimuacha Yanga wakamsajili, hivyo haitokuwa ajabu Coastal kumchukua Ntibazonkiza kutokana na mahitaji ya timu na hata uwezo wao kiuchumi.
Nasema hivyo kwa sababu Coastal wanaenda kwenye mashindano magumu yanahitaji aina ya wachezaji wabunifu, wazoefu ambao wana uwezo wa kubadili matokeo.
Nimewahi kusema huko nyuma kwamba Ntibazonkiza ni aina ya mchezaji ambaye anaweza kuingia uwanjani muda ambao timu pinzani imeamua kupaki basi na akasaidia kubadili matokeo kutokana na aina ya uchezaji wake wa kujiamini ikibidi hata kupiga chenga kufungua vyumba.
Ninachokiona ni kwamba hadi sasa Coastal bado hawajafanya usajili wowote unaoendana na hadhi ya timu inayojiandaa kushindana katika mashindano ya klabu barani Afrika, badala yake tulichosikia ni kwamba beki wao amehamia Simba.
Kwangu mimi naona Ntibazonkiza ni mmoja wa wachezaji wenye hadhi si ya Ligi Kuu NBC na michuano mingine ya ndani bali hata michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika hivyo anaweza na ana sifa zote za kuisaidia timu hiyo.
Bado sioni tatizo au ubaya wowote kwa Coastal kukiongezea nguvu kikosi chake kwa kumsajili Ntibazonkiza, naamini wakifanya uamuzi huo hawawezi kujuta.
Najua wapo wanaoweza kushangaa ninapomtaja Ntibazonkiza na kumhusisha na Azam, tusishangae hoja yake inasimamia maandalizi ya timu kwenye Ligi ya Mabingwa, hata ni mashindano makubwa ambayo timu shiriki inatakiwa iwe imekamilika kila idara.
Msimu uliopita, Azam ililalamikiwa mara kwa mara kwa kukosa kipa mzuri, hilo wamelifanyia kazi, Mustapha Mohamed unaweza kumtaja kuwa kipa mwenye hadhi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, anaweza kuwa msaada na hata akipatakana aliye bora zaidi yake ni vizuri zaidi.
Ni hivi karibuni tu Azam wametudhihirishia udhaifu wao kwenye mikwaju wa penalti hadi kushindwa kutamba mbele ya Yanga kwenye Kombe la Shirikisho CRDB, walioangalia mechi ile hadi kwenye penalti watakubaliana na mimi.
Sasa kama kweli wanakwenda Ligi ya Mabingwa na hawataki udhaifu wowote kwenye timu yao basi kwenye penalti, Ntibazonkiza ni chaguo sahihi.
Hili nalo linaweza kushangaza wengi na kuhoji yaani asajiliwe kwa ajili ya penalti tu au mipira ya adhabu, hapana Ntibazonkiza ana sifa nyingine kama ambavyo nimezieleza hapo juu lakini hili la penalti nalo si la kupuuza hata kidogo, si udhaifu wa kuachwa kama una uwezo ni vyema kuuziba.
Katika Ligi ya Mabingwa linapozungumziwa suala la timu kuwa kamili maana yake ni kutoupa nafasi udhaifu wowote kwenye timu na kuingia nao katika mashindano hayo, kufanya hivyo ni kujiruhusu kushindwa. Una tatizo la penalti, tafuta wapiga penalti kabisa.
Udhaifu huu wa penalti upo hadi Yanga, kitendo cha kupigiana penalti hadi tisa na Azam maana yake ni kwamba kuna tatizo katika eneo hilo na wanahitaji kulifanyia kazi kama kweli wanahitaji kuwa washindani kwenye Ligi ya Mabingwa.
Tena Yanga ndio wanatakiwa kuliangalia hili kwa macho mapana zaidi kwani wameshindwa kuweka historia ya kufikia nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa kwa kukosa wapiga penalti wazuri, nao wanatakiwa kujiandaa na hilo vinginevyo watakwama tena.
Sisemi wamsajili Ntibazonkiza lakini wanatakiwa kukubali kilicho wazi kwamba penalti ni mtihani kwao, walifanyie kazi hilo hasa kwa kuwa anayesajiliwa hasajiliwi ili apige penalti tu bali anakuwa na sifa nyingine za ziada kama ilivyo kwa Ntibazonkiza.

The post Namuona Ntibazonkiza, Coastal, Azam first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/06/22/namuona-ntibazonkiza-coastal-azam/feed/ 0
Saido hajayafurahia matokeo na Ahly https://www.greensports.co.tz/2023/10/21/saido-hajayafurahia-matokeo-na-ahly/ https://www.greensports.co.tz/2023/10/21/saido-hajayafurahia-matokeo-na-ahly/#respond Sat, 21 Oct 2023 14:54:48 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=8180 Na mwandishi wetuKiungo mshambuliaji wa Simba, Saido Ntibazonkiza amesema matokeo waliyoyapata dhidi ya Al Ahly ya Misri si mazuri sana na sasa wanajipanga kuhakikisha wanapata matokeo mechi ya marudiano.Wekundu hao walipata sare ya mabao 2-2 jana Ijumaa kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam ikiwa ni mchezo wa ufunguzi wa michuano mipya ya African Football […]

The post Saido hajayafurahia matokeo na Ahly first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
Saido Ntibazonkiza

Na mwandishi wetu
Kiungo mshambuliaji wa Simba, Saido Ntibazonkiza amesema matokeo waliyoyapata dhidi ya Al Ahly ya Misri si mazuri sana na sasa wanajipanga kuhakikisha wanapata matokeo mechi ya marudiano.
Wekundu hao walipata sare ya mabao 2-2 jana Ijumaa kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam ikiwa ni mchezo wa ufunguzi wa michuano mipya ya African Football League (AFL) inayoshirikisha timu nane za Afrika.
Saido aliyetoa pasi ya bao la pili la Simba alisema wana furaha kwa matokeo hayo lakini si waliyokuwa wakiyataka kwani ushindi ndio muhimu zaidi japo anawapongeza wachezaji wenzake kwa namna walivyojitoa kupambana katika mchezo huo.
“Al Ahly ni timu kubwa na tunashukuru Mungu kwa matokeo haya, huu ni mchezo wa kwanza na sasa tunasubiri wa pili kuona tutafanya nini lakini binafsi nawapongeza kila mchezaji, kila mmoja alipambana, hii ni sare ya 2-2 lakini kwenye mpira lolote linatokea, tusubiri mechi ya pili,” alisema Saido.
Alisema kwa sasa wanakubaliana na matokeo hayo lakini wanakwenda kujipanga zaidi wakitambua mchezo wa ugenini hautakuwa mwepesi, akiamini kocha wao Roberto Oliveira ‘Robertinho’ atakuwa na mbinu za kuwavuruga wapinzani wao nyumbani kwao.
Timu hizo zinatarajia kurudiana keshokutwa Jumanne kwenye Uwanja wa Cairo uliopo mjini Cairo huku Simba ikihitaji ushindi au sare ya kuanzia mabao 3-3 ili kusonga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.

The post Saido hajayafurahia matokeo na Ahly first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/10/21/saido-hajayafurahia-matokeo-na-ahly/feed/ 0
Ntibazonkiza, Mayele wang’ara tuzo TFF https://www.greensports.co.tz/2023/06/13/ntibazonkiza-mayele-wangara-tuzo-tff/ https://www.greensports.co.tz/2023/06/13/ntibazonkiza-mayele-wangara-tuzo-tff/#respond Tue, 13 Jun 2023 09:03:34 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=6578 Na mwandishi wetuKitendawili cha mfungaji bora Ligi Kuu NBC kimeteguliwa kwa Fiston Mayele na Saido Ntibazonkiza wote kupewa tuzo hiyo baada ya kila mmoja kufunga mabao 17 na wote wameng’ara kwa kubeba tuzo nyingine mbili.Vinara wengine wa soka waliong’ara kwa ufungaji na kushinda tuzo ni Jentrix Shikangwa wa Simba Queens ambaye kama ilivyo kwa Mayele […]

The post Ntibazonkiza, Mayele wang’ara tuzo TFF first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Kitendawili cha mfungaji bora Ligi Kuu NBC kimeteguliwa kwa Fiston Mayele na Saido Ntibazonkiza wote kupewa tuzo hiyo baada ya kila mmoja kufunga mabao 17 na wote wameng’ara kwa kubeba tuzo nyingine mbili.
Vinara wengine wa soka waliong’ara kwa ufungaji na kushinda tuzo ni Jentrix Shikangwa wa Simba Queens ambaye kama ilivyo kwa Mayele na Ntibazonkiza naye amemaliza Ligi Kuu ya Wanawake (WPL) na mabao 17.
Naye mshambuliaji wa Ihefu, Andrew Simchimba yeye amebeba tuzo ya mfungaji bora wa michuano ya Kombe la FA (ASFC).
Hafla ya utoaji tuzo hizo ilifanyika Jumatatu hii usiku mjini Tanga ambapo awali zilikuwapo hisia miongoni mwa wadau wa soka kwamba TFF ingekuja na kigezo cha kumpa tuzo mfungaji bora mmoja kati ya Mayele au Ntibazonkiza.
Wachezaji hao mbali na kutwaa tuzo ya mfungaji bora, kila mmoja ana tuzo nyingine mbili, Mayele ana tuzo ya bao bora la msimu na ile ya mchezaji bora wa msimu wakati, Ntibazonkiza naye pia ana tuzo ya fair play na kiungo bora.

Fiston Mayele

Sambamba na tuzo hizo, Mayele na Ntibazonkiza pia wamo kwenye kikosi bora cha msimu wa 2022-23 ambao pia umehitimishwa Jumatatu hii kwa mechi ya fainali ya Kombe la FA kati ya Yanga na Azam, mechi iliyoisha kwa Yanga kuifunga Azam bao 1-0.
Ukiachana na wachezaji hao, kipa wa Yanga, Djigui Diarra yeye ametwaa tuzo mbili akiwa na tuzo ya kipa bora wa ASFC pamoja na ya Ligi Kuu NBC na yumo pia kwenye kikosi bora cha msimu.
Wachezaji wengine wa Yanga, beki Dickson Job amebeba tuzo ya beki bora wakati Bakari Mwamnyeto amebeba tuzo ya mchezaji bora wa ASFC na wote hao wameingia kwenye kikosi bora.
Katika kikosi bora cha msimu pia wamo Mohammed Hussein, Henoc Inonga, Mzamiru Yassin, Shomari Kapombe na Clatous Chama ambao wote ni wachezaji wa Simba wakati kocha wa Yanga, Nasredinne Nabi yeye ametwaa tuzo ya kocha bora.


Mshambuliaji wa Yanga, Clement Mzize ameshinda tuzo ya mchezaji bora kijana chini ya miaka 20 anayecheza ligi kuu wakati Lameck Lawi wa Coastal Union ameshinda tuzo ya mchezaji bora chipukizi katika ligi hiyo hiyo.
Kwa upande wa ligi ya Championship mchezaji bora wa ligi hiyo ni Edward Songo wa JKT Tanzania wakati meneja bora wa uwanja ni Omar Malule na tuzo ya gwiji wa zamani wa soka imekwenda kwa Leopold Mukebezi beki wa zamani wa timu ya Pan Africa na Taifa Stars.
Tuzo ya mwamuzi bora wa ligi hiyo imechukuliwa na Jonesia Rukyaa wakati ile ya mwamuzi msaidizi imebebwa na Frank Komba huku Jonesia Rukya, Zawadi Yusuph, Athuman Rajab na Ally Simba wakibeba tuzo ya seti bora ya waamuzi kwa namna walivyosimamia vizuri mechi ya Geita Gold na Dodoma Jiji na Isack Munisi amebeba tuzo ya kamishna bora.
Kwa upande wa WPL mbali na Jentrix (pichani juu) aliyetwaa tuzo ya mfungaji bora, Ally Ally wa JKT Queens ametwaa tuzo ya kocha bora wakati Donisia Minja akitwaa tuzo ya mchezaji bora, Winfrida Charles tuzo ya mchezaji bora chipukizi na Najat Abbas yeye amechukua tuzo ya kipa bora.
Katika WPL pia, tuzo ya mwamuzi bora imekwenda kwa Ester Adalbert wakati ile ya mwamuzi msaidizi imechukuliwa na Glory Tesha.

The post Ntibazonkiza, Mayele wang’ara tuzo TFF first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/06/13/ntibazonkiza-mayele-wangara-tuzo-tff/feed/ 0
Ntibazonkiza mchezaji bora mwezi Mei https://www.greensports.co.tz/2023/06/11/ntibazonkiza-ndiye-bora-mwezi-mei/ https://www.greensports.co.tz/2023/06/11/ntibazonkiza-ndiye-bora-mwezi-mei/#respond Sun, 11 Jun 2023 16:52:29 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=6547 Na mwandishi wetuKiungo mshambuliaji wa Simba, Saido Ntibazonkiza amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Mei wa Ligi Kuu NBC wakati kocha wake Roberto Oliviera ‘Robertinho’ amechaguliwa kuwa kocha bora.Uteuzi wa wawili hao umetangazwa leo Jumapili kupitia taarifa ya Idara ya Habari, Mawasiliano ya TFF ikiwa ni siku moja kabla ya kutolewa kwa tuzo za jumla […]

The post Ntibazonkiza mchezaji bora mwezi Mei first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Kiungo mshambuliaji wa Simba, Saido Ntibazonkiza amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Mei wa Ligi Kuu NBC wakati kocha wake Roberto Oliviera ‘Robertinho’ amechaguliwa kuwa kocha bora.
Uteuzi wa wawili hao umetangazwa leo Jumapili kupitia taarifa ya Idara ya Habari, Mawasiliano ya TFF ikiwa ni siku moja kabla ya kutolewa kwa tuzo za jumla za wachezaji wa ligi hiyo msimu wa 2022-23.
Katika tuzo hizo za jumla ambazo hafla yake itafanyika mkoani Tanga mara baada ya mechi ya fainali ya Kombe la FA kati ya Yanga na Azam, Ntibazonkiza pia anawania tuzo ya mfungaji bora akiwa amefungana idadi ya mabao na Fiston Mayele wa Yanga.
Wachezaji hao kila mmoja amezifumania nyavu mara 17 na mjadala uliopo sasa miongoni mwa wadau wa soka nchini ni kama TFF itawapa wachezaji hao wawili tuzo hiyo au itakuwa na kigezo cha kumpa mmoja.
Ntibazonkiza ametwaa tuzo ya mwezi Mei akibebwa na mabao saba aliyofunga katika mechi mbili, alifunga mabao mawili katika mechi na Coastal Union katika ushindi wa 3-1, akafunga mabao matano katika ushindi wa mabao 6-1 dhidi ya Polisi Tanzania.
Katika kipindi hicho hicho cha mwezi Mei, Ntibazonkiza pia alihusika katika mabao mawili ya Simba na hivyo kuwashinda Prince Dube wa Azam na Charles Ilamfya wa Mtibwa Sugar aliokuwa akichuana nao.
Kwa upande wa Robertinho ametwaa tuzo hiyo akibebwa na ushindi wa timu yake wa mabao 3-0 dhidi ya Ruvu Shooting, 6-1 dhidi ya Polisi Tanzania, 3-1 dhidi ya Coastal Union na sare ya bao 1-1 na Namungo.
Katika kuwania tuzo ya kocha bora, Robertinho aliwabwaga makocha wenzake Melis Medo wa Dodoma Jiji na Daniel Cadera wa Azam FC.
Naye meneja wa Uwanja wa Azam Complex wa Chamazi jijini Dar es Salaam, Amir Juma ametwaa tuzo ya meneja bora wa uwanja kwa mwezi Mei baada ya kufanya vizuri katika usimamizi wa matukio ya michezo pamoja na ubora wa miundombinu.

The post Ntibazonkiza mchezaji bora mwezi Mei first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/06/11/ntibazonkiza-ndiye-bora-mwezi-mei/feed/ 0
Ntibazonkiza amnasa Mayele kwa mabao https://www.greensports.co.tz/2023/06/09/ntibazonkiza-amnasa-mayele-kwa-mabao/ https://www.greensports.co.tz/2023/06/09/ntibazonkiza-amnasa-mayele-kwa-mabao/#respond Fri, 09 Jun 2023 15:19:03 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=6534 Na mwandishi wetuMabao saba aliyofunga Saido Ntibazonkiza wa Simba katika mechi mbili za mwisho za Ligi Kuu NBC msimu huu yamemfanya afungane mabao ya kufunga na Fiston Mayele kila mmoja akiwa na mabao 17.Kwa kipindi kirefu Mayele amekuwa kinara wa mabao wa ligi hiyo akiwa na mabao 16 wakati Ntibazonkiza alikuwa na mabao 10 kabla […]

The post Ntibazonkiza amnasa Mayele kwa mabao first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
Saido Ntibazonkiza

Na mwandishi wetu
Mabao saba aliyofunga Saido Ntibazonkiza wa Simba katika mechi mbili za mwisho za Ligi Kuu NBC msimu huu yamemfanya afungane mabao ya kufunga na Fiston Mayele kila mmoja akiwa na mabao 17.
Kwa kipindi kirefu Mayele amekuwa kinara wa mabao wa ligi hiyo akiwa na mabao 16 wakati Ntibazonkiza alikuwa na mabao 10 kabla mambo hayajabadilika katika mechi mbili za mwisho.
Katika mechi hizo, Ntibazonkiza alifunga mabao matano peke yake dhidi ya Polisi Tanzania katika ushindi wa 6-1 na leo Ijumaa amefunga mabao mawili katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Coastal Union.
Kwa matokeo ya mechi hizo za mwisho za ligi msimu wa 2022-23, wachezaji hao wanakuwa wamefungana kwa idadi ya mabao ya kufunga ingawa Ntibazonkiza anajivunia kwa kuwa na asisti nyingi, 12 dhidi ya nne za Mayele.
Katika vita ya kujinasua na janga la kucheza play-offs, mambo hayakuwa mazuri kwa timu za Mbeya City na KMC ambazo zitalazimika kucheza mechi hizo. KMC imeshika nafasi ya 13 licha ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 mbele ya Mbeya City.
Ushindi wa KMC umeifanya timu hiyo ifikishe pointi 32 ambazo hazikuweza kuitoa katika nafasi ya 13 wakati Mbeya City iliyokuwa nafasi ya 13 inashuka hadi nafasi ya 14 na pointi zake 31.
Polisi Tanzania inabaki nafasi ya 15 na Ruvu Shoting inabaki ikiburuza mkia katika nafasi ya 16.
Matokeo ya mechi za mwisho Ligi Kuu NBC msimu wa 2022-23 zilizochezwa leo Ijumaa ni kama ifuatavyo…
Azam 8-0 Polisi Tanzania
Coastal 1-3 Simba
Mtibwa Sugar 3-1 Geita Gold
Prisons 0-2 Yanga
Ihefu 2-0 Kagera Sugar
Mbeya City 0-1 KMC
Ruvu Shooting 0-1 Dodoma Jiji
Namungo 1-1 Singida Big

The post Ntibazonkiza amnasa Mayele kwa mabao first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/06/09/ntibazonkiza-amnasa-mayele-kwa-mabao/feed/ 0
Vita ya Mayele, Ntibazonkiza yafika patamu https://www.greensports.co.tz/2023/06/09/vita-ya-mayele-nitabazonkiza-yafika-patamu/ https://www.greensports.co.tz/2023/06/09/vita-ya-mayele-nitabazonkiza-yafika-patamu/#respond Fri, 09 Jun 2023 09:41:05 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=6526 Na Hassan KinguHuo ndio ukweli, mechi za mwisho za Ligi Kuu NBC zinanogeshwa na vita ya Fiston Mayele na Saido Ntibazonkiza kwenye tuzo ya mfungaji bora, ukiacha vita kali ya kujinasua na janga la kushuka daraja.Mechi hizo zinapigwa leo Ijumaa saa tisa na nusu alasiri, tuzo ya kuwania kiatu cha mfungaji bora ghafla imegeuka kuwa […]

The post Vita ya Mayele, Ntibazonkiza yafika patamu first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na Hassan Kingu
Huo ndio ukweli, mechi za mwisho za Ligi Kuu NBC zinanogeshwa na vita ya Fiston Mayele na Saido Ntibazonkiza kwenye tuzo ya mfungaji bora, ukiacha vita kali ya kujinasua na janga la kushuka daraja.
Mechi hizo zinapigwa leo Ijumaa saa tisa na nusu alasiri, tuzo ya kuwania kiatu cha mfungaji bora ghafla imegeuka kuwa mpambano wa Mayele na Ntibazonkiza.
Ntibazonkiza amebadili upepo ghafla kwa mabao yake matano aliyofunga katika mechi dhidi ya Polisi Tanzania na hivyo kufikisha mabao 15 akizidiwa bao moja na Mayele.
Na ingawa Ntibazonkiza amenukuliwa na GreenSports akisema hashindani na Mayele lakini si kweli kwamba haitaki tuzo ya mfungaji bora, atapambana kuhakikisha anafunga ili kuibuka mfungaji bora na hiyo maana yake ni kwamba yupo vitani.
Katika hali ya kawaida wachezaji wenzake wa Simba pia watapenda kuona anaibuka mfungaji bora, penalti, mipira ya adhabu na mazingira yote ya kupata bao watampa yeye ili aibuke mfungaji bora na kumbwaga Mayele ambaye kila mtu aliamini msimu huu tuzo hiyo ni mali yake.
Leo Yanga inakamilisha mechi yake ya mwisho ya ligi dhidi ya Prisons wakati Simba itaivaa Coastal Union, kama tutazichukulia mechi hizi kwa kuangalia yaliyopita, mashabiki wa Simba wana kila sababu ya kujipa matumaini kwamba mchezaji wao Ntibazonkiza ataibuka mfungaji bora na wale wa Yanga wataingiwa na huzuni na wasiwasi kwamba Mayele ataikosa tuzo hiyo kwa mara ya pili.
Prisons wamekuwa wagumu kwa Yanga wakati Coastal wanajulikana ni vibonde wa Simba, haitokuwa ajabu Simba kuifunga Coastal hata mabao matano na Yanga haitokuwa ajabu kutoka sare na Prisons.
Mazingira hayo hata hivyo hayana jibu la moja kwa moja kwamba nani ataibuka kinara wa mabao msimu huu, lolote linaweza kutokea katika mechi hizo za kufunga msimu.

Saido Ntibazonkiza

Msimu uliopita wa 2021-22 Mayele alipoteza tuzo hiyo katika hatua za mwisho mbele ya George Mpole na msimu huu anatakiwa kujiandaa kisaikolojia kwa hali hiyo kwani kwa hatua iliyofikia anaweza akashangazwa tena msimu huu wa 2022-23.
Matarajio yote makubwa ya awali yakafutika na badala yake akaishia nafasi ya pili kama ilivyokuwa msimu uliopita, chanzo cha yote ni huyu mtu anayeitwa Ntibazonkiza ambaye alikuwa naye Yanga kabla ya kutimuliwa na sasa anaelekea kuzima ‘mitetemo’ ya Mayele katika hatua za mwisho.
Ntibazonkiza ambaye alijiunga na Simba akitokea Geita Gold katika dirisha dogo, mabao yake mengine aliyafunga akiwa na timu hiyo, ametokea kuwa moto tangu atue Simba, si kwa kufunga mabao tu bali pia amekuwa mpishi muhimu wa mabao ya timu hiyo.
Ukiachana na Mayele na Ntibazonkiza janga la kujinasua na hatari ya kushuka daraja nalo lina vita yake inayohusisha timu za Mbeya City, iliyo nafasi ya 13 ikiwa na pointi 31, KMC ya 14 pointi 29, na Polisi Tanzania ya 15 pointi 25 na Ruvu Shooting ya 16 pointi 20.
Matokeo ya mechi za leo pia ndiyo yatakayoamua timu ipi itacheza play-off, zilizo katika hatari hiyo ni KMC, Coastal Union, Mbeya City na Mtibwa Sugar.
Mechi za leo Ijumaa za Ligi Kuu NBC ni kama ifuatavyo…
Prisons v Yanga
Simba v Coastal
Azam v Polisi Tanzania
Namungo v Singida Big
Ihefu v Kagera
Mbeya City v KMC
Mtibwa Sugar v Geita Gold
Ruvu Shooting v Dodoma Jiji

The post Vita ya Mayele, Ntibazonkiza yafika patamu first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/06/09/vita-ya-mayele-nitabazonkiza-yafika-patamu/feed/ 0
Ntibazonkiza: Sishindani na Mayele https://www.greensports.co.tz/2023/06/07/ntibazonkiza-sishindani-na-mayele/ https://www.greensports.co.tz/2023/06/07/ntibazonkiza-sishindani-na-mayele/#respond Wed, 07 Jun 2023 15:27:55 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=6502 Na mwandishi wetuMshambuliaji wa Simba, Saido Ntibazonkiza amesema hana mpango wa kushindana na mshambuliaji wa Yanga, Fiston Mayele kuwania kiatu cha ufungaji bora msimu huu kwa kuwa amewekeza nguvu kubwa kuisaidia timu kwanza.Ntibazonkiza alifunga mabao matano jana katika ushindi wa mabao 6-1 dhidi ya Polisi Tanzania kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam na […]

The post Ntibazonkiza: Sishindani na Mayele first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Mshambuliaji wa Simba, Saido Ntibazonkiza amesema hana mpango wa kushindana na mshambuliaji wa Yanga, Fiston Mayele kuwania kiatu cha ufungaji bora msimu huu kwa kuwa amewekeza nguvu kubwa kuisaidia timu kwanza.
Ntibazonkiza alifunga mabao matano jana katika ushindi wa mabao 6-1 dhidi ya Polisi Tanzania kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam na hivyo kufikisha mabao 15 nyuma ya Mayele aliyefunga mara 16.
Ntibazonkiza hata hivyo alisema anashukuru kuisaidia timu yake kupata matokeo na kama itatokea atatwaa kiatu cha ufungaji bora basi itakuwa vizuri lakini kwa sasa anaitanguliza Simba kisha mambo mengine yatafuata.

“Kwa sasa ni timu kwanza kupata matokeo mazuri kisha vingine hivyo tutaangalia kitakachotokea kwa uwezo wa Mungu. Fiston ni mfungaji mzuri, mshambuliaji mzuri kila mtu anamjua kwa hiyo ikitokea nikifanikiwa kuchukua nitamshukuru Mungu lakini timu kwanza,” alisema Ntibazonkiza.


Kwa mabao matano aliyofunga juzi, Ntibazonkiza anakuwa mchezaji wa kwanza msimu huu kufunga mabao mengi katika mechi moja lakini pia akifunga ‘hat-trick’ya pili msimu huu, sawa na nahodha wa Simba, John Bocco.

The post Ntibazonkiza: Sishindani na Mayele first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/06/07/ntibazonkiza-sishindani-na-mayele/feed/ 0
Ntibazonkiza amtikisa Mayele https://www.greensports.co.tz/2023/06/07/ntibazonkiza-amtikisa-mayele/ https://www.greensports.co.tz/2023/06/07/ntibazonkiza-amtikisa-mayele/#respond Wed, 07 Jun 2023 06:43:37 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=6494 Na mwandishi wetuYanga imetoka sare ya mabao 3-3 na Mbeya City wakati Simba ikiilaza Polisi Tanzania 6-1, Saido Ntibanzokiza akifunga mabao matano kati ya sita ya Simba na kufikisha mabao 15 katika Ligi Kuu NBC akimtikisa Fiston Mayele anayeshika usukani akiwa na mabao 16.Katika mechi hizo za ligi hiyo zilizopigwa Jumanne hii, matokeo hayo yameibua […]

The post Ntibazonkiza amtikisa Mayele first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Yanga imetoka sare ya mabao 3-3 na Mbeya City wakati Simba ikiilaza Polisi Tanzania 6-1, Saido Ntibanzokiza akifunga mabao matano kati ya sita ya Simba na kufikisha mabao 15 katika Ligi Kuu NBC akimtikisa Fiston Mayele anayeshika usukani akiwa na mabao 16.
Katika mechi hizo za ligi hiyo zilizopigwa Jumanne hii, matokeo hayo yameibua gumzo jipya la nani ataibuka mfungaji bora msimu huu wa 2022-23? Je Ntibazonkiza (pichani juu) atambwaga Mayele?
Katika mechi za kukamilisha ligi hiyo zitakazopigwa Juni 9, Simba itakuwa mwenyeji wa Coastal Union wakati Yanga itakuwa mgeni wa Tanzania Prisons, mechi ambazo matokeo ya pointi yanaweza yasiwe na maana badala yake mbio za kuwania kiatu cha mfungaji bora zikateka hisia za mashabiki.
Kati ya mabao 15 aliyofikisha Ntibazonkiza hadi sasa, mengine aliyafunga wakati akiichezea Geita Gold wakati kwa Mayele yote ameyafunga akiwa na Yanga.

Kwa Mayele (pichani) iwapo ataangushwa na Ntibazonkiza, itakuwa mara ya pili mfululizo kukutana na hali inayofanana na hiyo, msimu uliopita alishindwa kutamba mbele ya George Mpole. Mayele alipigwa bao na Mpole katika mechi za mwisho na safari hii huenda akakutana tena na hali hiyo.
Zaidi ya hilo, Mayele atakuwa ameshindwa kutimiza ndoto yake aliponukuliwa akisema angependa kumaliza msimu huu akiwa mfungaji mwenye mabao mengi katika Kombe la Shirikisho Afrika na Ligi Kuu NBC.
Tayari amefanikisha hilo kwenye Kombe la Shirikisho baada ya kuongoza na mabao yake saba lakini kwenye Ligi Kuu NBC ametikiswa kidogo, Ntibazonkiza amemsogelea na haitoshangaza wakifungana kwa mabao au hata akapitwa.
Katika mechi ya Simba ukiacha mabao ya Ntibazonkiza, bao jingine la Simba lilifungwa na Israel Mwenda wakati bao pekee la Polisi likifungwa na Steven Mayala.
Yanga nao ambao tayari ni vinara wa Ligi Kuu NBC, matokeo ya mechi hiyo japo yamewaumiza mashabiki wake lakini yamezidi kuiweka pagumu Mbeya City ambayo ilitakiwa ishinde ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kuepuka janga la kushuka daraja.
Wakati Polisi ikiwa tayari imeshuka daraja, Mbeya City yenye pointi 31 italazimika kupambana kufa na kupona ili ishinde mechi yake ya mwisho na KMC na hivyo kufikisha pointi 34.
Ugumu wa mechi hiyo unachangiwa na mazingira ya KMC yenye pointi 29 ambayo pia inahitaji ushindi ili ifikishe pointi 32. Je nani atashinda na kujinasua na janga la kushuka daraja? KMC kwa sasa inashika nafasi ya 14 wakati Mbeya City inashika nafasi ya 13.

The post Ntibazonkiza amtikisa Mayele first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/06/07/ntibazonkiza-amtikisa-mayele/feed/ 0