Simba - Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz Michezo na Burudani ni zaidi ya ajira Sun, 22 Mar 2026 14:21:09 +0000 en-GB hourly 1 https://wordpress.org/?v=6.9.4 https://www.greensports.co.tz/wp-content/uploads/2021/09/cropped-WhatsApp-Image-2021-09-02-at-13.12.19-1-32x32.jpeg Simba - Greensports: Michezo na Burudani https://www.greensports.co.tz 32 32 Pamba yaibana mbavu Simba https://www.greensports.co.tz/2026/03/20/pamba-yaibana-mbavu-simba/ https://www.greensports.co.tz/2026/03/20/pamba-yaibana-mbavu-simba/#respond Fri, 20 Mar 2026 14:18:04 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14467 Na mwandishi wetuMatarajio ya Simba kutoka na pointi tatu katika mechi yake ya Ligi Kuu NBC dhidi ya Pamba Jiji yamekwama baada ya timu hizo kutoka sare ya bao 1-1.Matokeo ya mechi hiyo iliyopigwa Alhamisi Machi 19, 2026 kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza yamewakera mashabiki wa Simba waliojipa matumaini ya kubeba pointi tatu hasa […]

The post Pamba yaibana mbavu Simba first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Matarajio ya Simba kutoka na pointi tatu katika mechi yake ya Ligi Kuu NBC dhidi ya Pamba Jiji yamekwama baada ya timu hizo kutoka sare ya bao 1-1.
Matokeo ya mechi hiyo iliyopigwa Alhamisi Machi 19, 2026 kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza yamewakera mashabiki wa Simba waliojipa matumaini ya kubeba pointi tatu hasa baada ya hasimu wao Yanga kutoka sare ya bao 0-0 na TRA United.
Simba ndio waliokuwa wa kwanza kuzichana nyavu za Pamba katika dakika ya 32 kwa bao lililofungwa na Anicet Oura lakini shuti la mbali lililopigwa na James Mwashenga dakika tatu baadaye lilitosha kuipa Pamba bao la kusawazisha.
Kwa matokeo hayo, Simba ambao hadi sasa wamecheza mechi 13 wamefikisha pointi 28 na kutulia nafasi ya tatu wakiachwa kwa tofauti ya pointi tisa na mahasimu wao Yanga wanaoshika usukani wa ligi hiyo wakiwa wamecheza mechi 15.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo, Mashujaa FC waliutumia vyema uwanja wao wa nyumbani wa Lake Tanganyika kulazimisha sare ya bila kufungana na Azam FC.

The post Pamba yaibana mbavu Simba first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/03/20/pamba-yaibana-mbavu-simba/feed/ 0
Simba yailaza Singida Black 2-1 https://www.greensports.co.tz/2026/03/12/simba-yailaza-singida-black-2-1/ https://www.greensports.co.tz/2026/03/12/simba-yailaza-singida-black-2-1/#respond Thu, 12 Mar 2026 15:04:54 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14417 Na mwandishi wetuBaada ya sare mbili za bila kufungana dhidi ya Yanga na Dodoma Jiji, Simba imefufua upya matumaini ya kulisaka taji la Ligi Kuu NBC msimu huu wa 2025-26 baada ya kuichapa Singida Black Stars mabao 2-1.Ushindi huo uliopatikana Jumatano Machi 11, 2026 kwenye Uwanja wa Airtel umeifanya Simba kufikisha pointi 27 ikitulia nafasi […]

The post Simba yailaza Singida Black 2-1 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Baada ya sare mbili za bila kufungana dhidi ya Yanga na Dodoma Jiji, Simba imefufua upya matumaini ya kulisaka taji la Ligi Kuu NBC msimu huu wa 2025-26 baada ya kuichapa Singida Black Stars mabao 2-1.
Ushindi huo uliopatikana Jumatano Machi 11, 2026 kwenye Uwanja wa Airtel umeifanya Simba kufikisha pointi 27 ikitulia nafasi ya tatu baada ya kucheza mechi 12 wakiwa wamezidiwa na vinara wa ligi hiyo, Yanga kwa tofauti ya pointi tano.
Simba walianza kuzichana nyavu za Singida BS katika dakika ya saba ya mchezo huo kwa bao lililofungwa na Anicet Oura aliyefunga baada ya kuinasa pasi ya Alassane Kante.
Singida BS walifanikiwa kusawazisha bao hilo katika dakika ya 37 mfungaji akiwa ni Mossi Ndumumwe akimalizia pasi aliyounganishiwa na Lamine Jarjou.
Dakika sita kabla ya kutimia dakika 90, Elly Mpanzu aliihakiksihai Simba pointi tatu muhimu kwa kuiandikia Simba bao la pili na la ushindi akiitumia vizuri pasi ya Clatous Chama.
Matokeo hayo yanazidi kuiweka Singida BS pagumu katika ligi hiyo kwani katika mechi 13 ilizocheza hadi sasa imeambulia pointi 19 na inashika nafasi ya 10.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Azam FC ikiwa ugenini ilitoka kidedea mbele ya Dodoma jiji kwa kuilaza mabao 3-0 wakati Namungo ikiwa ugenini Karatu ilichapwa mabao 2-0 na TRA United.

The post Simba yailaza Singida Black 2-1 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/03/12/simba-yailaza-singida-black-2-1/feed/ 0
Simba yakwama, Yanga yapiga mtu mkono https://www.greensports.co.tz/2026/02/26/simba-yakwama-yanga-yapiga-mtu-mkono/ https://www.greensports.co.tz/2026/02/26/simba-yakwama-yanga-yapiga-mtu-mkono/#respond Thu, 26 Feb 2026 16:33:22 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14367 Na mwandishi wetuWakati Yanga ikishangilia ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mechi ya Ligi Kuu NBC, mambo hayakuwa mazuri kwa mtani wake Simba aliyelazimishwa sare ya bila kufungana na Dodoma Jiji FC.Mechi hizo zilizochezwa Jumatano Febuari 25, 2026 ni mechi za mwisho baina ya watani hao wa jadi kabla ya kukutana […]

The post Simba yakwama, Yanga yapiga mtu mkono first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Wakati Yanga ikishangilia ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mechi ya Ligi Kuu NBC, mambo hayakuwa mazuri kwa mtani wake Simba aliyelazimishwa sare ya bila kufungana na Dodoma Jiji FC.
Mechi hizo zilizochezwa Jumatano Febuari 25, 2026 ni mechi za mwisho baina ya watani hao wa jadi kabla ya kukutana Machi Mosi, 2026 kwenye dimba la New Amaan, Zanzibar katika mwendelezo wa mechi za ligi hiyo.
Karamu ya mabao matano ya Yanga au mkono ilipatikana kwenye Uwanja wa KMC, Kinondoni, Dar es Salaam kwa mabingwa hao watetezi wa ligi kuandika bao la kwanza kunako dakika ya saba mfungaji akiwa ni Mohamed Hussein au Zimbwe Junior baada ya kuinasa pasi ya Prince Dube.
JKT walipambana na kuonesha uhai na hadi timu zinakwenda mapumziko Yanga walikuwa mbele kwa bao hilo pekee licha ya mashambulizi ya mara kwa mara langoni mwa JKT.
Kipindi cha pili mambo yalianza kuwaharibikia JKT katika dakika ya 60 baada ya kufungwa bao la pili, mfungaji akiwa Dilson Depu aliyeitumia vizuri pasi ya Israel Mwenda.
Matumaini ya JKT kutaka bao la kufufua matumaini yalianza kufifia dakika tatu baada baada ya bao la Depu pale, Mudathir Yahya alipoiandikia Yanga bao la tatu.
Mabao mengine mawili ya Yanga yalifungwa na Dube katika dakika ya 83 na Shekhan Khamis aliyekamilisha karamu ya mabao hayo katika dakika ya 89.
Kwa ushindi huo Yanga imejikita kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa na pointi 28 katika mechi 10 sawa na JKT ingawa Yanga ina faida katika mabao ya kufunga na kufungwa.
Kwa upande wa Simba hali ilikuwa tete kwa dakika zote 90 kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana matokeo yanayowafanya mashabiki wa timu hiyo kubaki wakitafakari hatma ya timu yao kabla ya kuivaa Yanga.
Mechi hiyo kwa upande mwingine ilikuwa neema kwa kipa wa Dodoma Jiji, Daniel Mgore ambaye aliibuka mchezaji bora kwa namna ambavyo alifanikiwa kuzima ndoto za washambuliaji wa Simba kupata bao katika dakika zote 90.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo, Azam FC ikiwa nyumbani kwenye dimba la Azam Complex ilitoka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mtibwa Sugar.

The post Simba yakwama, Yanga yapiga mtu mkono first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/02/26/simba-yakwama-yanga-yapiga-mtu-mkono/feed/ 0
Simba yaaga ligi ya mabingwa kwa ushindi https://www.greensports.co.tz/2026/02/15/simba-yaaga-ligi-ya-mabingwa-kwa-ushindi/ https://www.greensports.co.tz/2026/02/15/simba-yaaga-ligi-ya-mabingwa-kwa-ushindi/#respond Sun, 15 Feb 2026 11:08:00 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14341 Na mwandishi wetuSimba imemaliza kwa kishindo mechi yake ya mwisho ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Stade Malien ya Mali huku ikiaga mashindano hayo katika hatua ya makundi kwa msimu huu wa 2025-26.Ikiwa nyumbani kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, Jumamosi Februari 14, Simba iliandika bao hilo […]

The post Simba yaaga ligi ya mabingwa kwa ushindi first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Simba imemaliza kwa kishindo mechi yake ya mwisho ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Stade Malien ya Mali huku ikiaga mashindano hayo katika hatua ya makundi kwa msimu huu wa 2025-26.
Ikiwa nyumbani kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, Jumamosi Februari 14, Simba iliandika bao hilo pekee mapema dakika ya tatu ya mchezo, bao lililofungwa na Anicet Oura.
Ushindi huo wa mechi ya Kundi D hata hivyo haukuwa na maana yoyote kwa Simba badala yake ni ushindi wa mechi ya kukamilisha ratiba ya michuano hiyo mikubwa kwa ngazi ya klabu barani Afrika.
Huo ndio ushindi pekee wa Simba katika kundi hilo, katika mechi zake sita za makundi timu hiyo imepoteza tatu, sare mara mbili na kushinda mechi moja.
Simba imemaliza kundi lake ikiwa mkiani baada ya kukusanya pointi tano wakati Malien wao walishafuzu na ndio vinara wa kundi hilo baada ya kukusanya pointi 11 na wanaungana na Esperance ya Tunisia ambayo pia imefuzu.
Esperance imefuzu hatua ya robo fainali ikiwa na pointi tisa baada ya ushindi wa nyumbani wa mabao 2-0 katika mechi na Petro Atletico ya Angola, mechi ambayo pia imechezwa siku moja na mechi ya Simba na Malien.
Timu nyingine zilizofuzu robo fainali ni Al Hilal ya Sudan na Mamelodi ya Afrika Kusini kutoka Kundi C ambapo Al Hilal imemaliza kundi hilo ikiwa kinara baada ya kukusanya pointi 11.
Katika Kundi B, Al Ahly ya Misri tayari imeshafuzu ikiwa imekusanya pointi tisa huku hatma ya timu ya pili ikisubiri matokeo ya mechi za Jumapili Februari 15, 2026 ambapo Yanga ya Tanzania itacheza na JS Kabylie wakati Al Ahly itaumana na AS FAR Rabat ya Morocco.
Yanga hadi sasa ina pointi tano wakati FAR Rabat ina pointi nane na kwa upande wa Kabylie ina pointi tatu na itacheza mechi yake na Yanga kukamilisha ratiba kwani haina nafasi ya kusonga mbele.

The post Simba yaaga ligi ya mabingwa kwa ushindi first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/02/15/simba-yaaga-ligi-ya-mabingwa-kwa-ushindi/feed/ 0
Sare yaitoa rasmi Simba Ligi ya Mabingwa https://www.greensports.co.tz/2026/02/08/sare-yaitoa-rasmi-simba-ligi-ya-mabingwa/ https://www.greensports.co.tz/2026/02/08/sare-yaitoa-rasmi-simba-ligi-ya-mabingwa/#respond Sun, 08 Feb 2026 13:41:38 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14321 Na mwandishi wetuHesabu za Simba kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika sasa ni rasmi zimefikia tamati kwa msimu huu wa 2025-26 baada ya sare ya bao 1-1 na Petro Atletico ya Angola katika mechi iliyopigwa Jumamosi Februari 7, 2026.Ile hadithi ya haiishi mpaka iishe, hatimaye imekwisha rasmi, Simba sasa itacheza mechi yake ya mwisho ya Kundi […]

The post Sare yaitoa rasmi Simba Ligi ya Mabingwa first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Hesabu za Simba kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika sasa ni rasmi zimefikia tamati kwa msimu huu wa 2025-26 baada ya sare ya bao 1-1 na Petro Atletico ya Angola katika mechi iliyopigwa Jumamosi Februari 7, 2026.
Ile hadithi ya haiishi mpaka iishe, hatimaye imekwisha rasmi, Simba sasa itacheza mechi yake ya mwisho ya Kundi D dhidi ya Stade Malien kwa ajili ya kukamilisha ratiba za ligi hiyo.
Kabla ya mechi na Petro, Simba walikuwa wakijipa matumaini ya ushindi na kuwaombea njaa wapinzani wake wa kundi hilo lakini kwa sare yao na Petro nafasi hiyo haipo, sasa ni kujipanga kwa msimu ujao wa 2026-27.
Wakati Simba ikibaki mkiani na pointi zake mbili, Petro wao wamefikisha pointi sita na kushika nafasi ya tatu huku Stade Malien wakiendelea kushika usukani na pointi zao 11 na Esperance ya pili na pointi sitana timu hizo zitaumana Jumapili katika mechi nyingine ya kundi hilo.
Petro wakiwa nyumbani walianza mchezo kwa kasi na kupata bao la kuongoza katika dakika ya 13 mfungaji akiwa ni Pedro Pinto, bao ambalo lilidumu kwa dakika 45 za kwanza.
Zikiwa zimebakia dakika 10 kabla ya kutimia dakika 90, Simba walifanikiwa kupata bao la kusawazisha lililofungwa na Anicet Ora na kutuliza kelele za mashabiki wa Petro waliokuwa kwenye uwanja wa nyumbani.

The post Sare yaitoa rasmi Simba Ligi ya Mabingwa first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/02/08/sare-yaitoa-rasmi-simba-ligi-ya-mabingwa/feed/ 0
Simba: Waliomfanyia fujo Mangungu waadhibiwe https://www.greensports.co.tz/2026/02/02/simba-waliomfanyia-fujo-mangungu-waadhibiwe/ https://www.greensports.co.tz/2026/02/02/simba-waliomfanyia-fujo-mangungu-waadhibiwe/#respond Mon, 02 Feb 2026 18:31:05 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14316 Na mwandishi wetuUongozi wa klabu ya Simba umelitaka jeshi la polisi nchini kuwachukulia hatua za kisheria waliohusika kumfanyia fujo mwenyekiti wa klabu hiyo, Murtaza Mangungu.Mangungu alijikuta katika kadhia hiyo kutoka kwa watu wanaodhaniwa kuwa mashabiki wa soka ambao walimbughudhi na kumtolea lugha chafu baada ya mechi yao na Esperance ya Tunisia iliyoisha kwa sare ya […]

The post Simba: Waliomfanyia fujo Mangungu waadhibiwe first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Uongozi wa klabu ya Simba umelitaka jeshi la polisi nchini kuwachukulia hatua za kisheria waliohusika kumfanyia fujo mwenyekiti wa klabu hiyo, Murtaza Mangungu.
Mangungu alijikuta katika kadhia hiyo kutoka kwa watu wanaodhaniwa kuwa mashabiki wa soka ambao walimbughudhi na kumtolea lugha chafu baada ya mechi yao na Esperance ya Tunisia iliyoisha kwa sare ya mabao 2-2.
Matokeo ya mechi hiyo ya Ligi ya Mabingwa Afrika iliyochezwa Jumapili Januari Mosi, 2026 kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam yamewakera baadhi ya mashabiki ambao inaaminika waliamua kumalizia hasira zao kwa Mangungu.
Katika tukio hilo, Mangungu alijikuta akizongwa na kama si juhudi za maofisa usalama wa uwanjani hapo huenda hali ingeweza kuwa mbaya kwa kiongozi huyo kwa namna ambavyo idadi ya mashabiki ilikuwa kubwa.
Taarifa ya klabu ya Simba iliyotolewa na mwenyekiti wa bodi ya klabu hiyo, Crecentius Magori muda mfupi baada ya mechi hiyo, ilieleza kusikitishwa na tukio hilo na kulitaja kuwa si la kiungwana na halikubaliki.
Magori katika taarifa hiyo alisema kuwa sambamba na kutoa pole kwa Mangungu lakini pia alifafanua kuwa tukio hilo halitafumbiwa macho.
Alilitaka jeshi la polisi kuchukua hatua za kisheria kwa wote waliohusika au kula njama katika tukio hilo dhidi ya Mangungu na bodi ya klabu hiyo haitavumilia wala kubariki mtu yeyote atakayeharibu taswira ya klabu kwa namna yoyote.
Mashabiki wengi wanaoaminika kuwa wa Simba walikerwa na matokeo ya sare ya 2-2 ambayo yamezidi kufifisha kama si kufuta matumaini ya timu hiyo kucheza hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

The post Simba: Waliomfanyia fujo Mangungu waadhibiwe first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/02/02/simba-waliomfanyia-fujo-mangungu-waadhibiwe/feed/ 0
Esperance yaiweka pagumu Simba https://www.greensports.co.tz/2026/02/02/esperance-yaiweka-pagumu-simba/ https://www.greensports.co.tz/2026/02/02/esperance-yaiweka-pagumu-simba/#respond Mon, 02 Feb 2026 08:59:25 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14311 Na mwandishi wetuMambo magumu kwa Simba kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 na Esperance ya Tunisia katika mechi iliyochezwa Jumapili Januari mosi, 2026 kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.Matokeo hayo yanaifanya Simba kupoteza kwa kiasi kikubwa matumaini ya kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano hiyo […]

The post Esperance yaiweka pagumu Simba first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Mambo magumu kwa Simba kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 na Esperance ya Tunisia katika mechi iliyochezwa Jumapili Januari mosi, 2026 kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.
Matokeo hayo yanaifanya Simba kupoteza kwa kiasi kikubwa matumaini ya kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano hiyo mikubwa kwa ngazi ya klabu barani Afrika.
Simba hadi sasa inashikilia mkia katika kundi lake ikiwa na pointi moja, Esperance inashika nafasi ya pili na pointi zake sita na Petro Atlético ya tatu ikiwa na pointi tano wakati Stade Malien ndiye kinara wa kundi hilo akiwa na pointi nane.
Mazingira ya kundi hilo yanaonesha kuwa Simba ikishinda mechi mbili zilizobaki itafikisha pointi saba kwa hiyo ili iweze kusonga mbele itahitaji Esperance na Petro Atlético zipoteze mechi zao mbili zilizobaki au kila moja ipoteze moja na moja iishe kwa sare.
Kwa maana nyingine Simba si tu inatakiwa kushinda mechi zilizobaki bali ishinde kwa mabao mengi lakini pia ile dhana ya adui yako muombee njaa nayo pia imebeba hatma ya Simba katika Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu wa 2025-26.
Kilichoifikisha Simba katika hali hiyo ni mechi yao na Esperance, mechi ambayo ilitoa matumaini ya timu hiyo kupata ushindi kabla ya mambo kuharibika na kujikuta wakitoa sare ya 2-2 huku Esperance wakikosa penalti.
Simba iliuanza mchezo huo vizuri na kuonesha kila dalili za kutoka uwanjani na pointi tatu baada ya kupata bao la kwanza dakika ya 39 lililofungwa na Shomari Kapombe.
Shamrashamra za mashabiki wa Simba baada ya bao hilo ziliongezeka kwa mara ya pili baada ya Yusuph Kagoma kuongeza bao la pili katika dakika za nyongeza kabla ya timu kwenda mapumziko.
Mambo yalianza kuiendea kombo Simba katika dakika ya 64 baada ya Aboubacar Diakité kuipatia Esperance bao la kwanza kabla Kouceila Boualia hajasawazisha dakika 15 baadaye na kuwaacha mashabiki wa Simba vichwa chini.
Kama hiyo haitoshi mashabiki hao waliingia unyonge tena katika dakika za nyongeza baada ya Esperance kupata penalti lakini Hamza Jelassi alishindwa kuitumia penalti hiyo kuipatia Esperance bao.
Katika mechi zijazo Simba itakuwa ugenini Angola kuumana na Petro de Luanda wakati Esperance itasafiri hadi Mali kuikabili Stade Malien.

The post Esperance yaiweka pagumu Simba first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/02/02/esperance-yaiweka-pagumu-simba/feed/ 0
Esperance yailaza Simba 1-0 https://www.greensports.co.tz/2026/01/25/esperance-yailaza-simba-1-0/ https://www.greensports.co.tz/2026/01/25/esperance-yailaza-simba-1-0/#respond Sun, 25 Jan 2026 11:04:58 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14290 Na mwandishi wetuMambo si mazuri kwa Simba baada ya kuchapwa bao 1-0 na Esperance ya Tunisia katika mechi ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika iliyochezwa Jumamosi Januari 24, 2026 kwenye Uwanja wa Hammadi Agrebi mjini Rades.Kwa matokeo hayo, Esperance wanashikilia usukani wa Kundi D wakiwa na pointi tano baada ya kucheza mechi […]

The post Esperance yailaza Simba 1-0 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Mambo si mazuri kwa Simba baada ya kuchapwa bao 1-0 na Esperance ya Tunisia katika mechi ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika iliyochezwa Jumamosi Januari 24, 2026 kwenye Uwanja wa Hammadi Agrebi mjini Rades.
Kwa matokeo hayo, Esperance wanashikilia usukani wa Kundi D wakiwa na pointi tano baada ya kucheza mechi tatu wakati Simba ikiendelea kuburuza mkia katika kundi hilo ambalo pia lina timu za Stade Malien ya Mali na Petro De Luanda ya Angola.
Bao pekee lililowapa ushindi wenyeji Esperance lilipatikana katika dakika ya 21 mfungaji akiwa ni Jacques Diarra baada ya kuiwahi pasi ndefu na kumzidi kasi beki wa Simba, Shomari Kapombe kabla ya kuujaza mpira wavuni.
Matokeo hayo pia yanazidi kufikisha matumaini ya Simba kucheza hatua ya robo fainali ya michuano hiyo ya klabu Afrika kwani hadi sasa timu hiyo imepoteza mechi zake zote tatu kati ya sita inazopaswa kucheza.
Kabla ya mechi ya Simba, mahasimu wao Yanga nao walikuwa ugenini Misri wakiumana na Al Ahly na Yanga kupoteza mchezo huo kwa kufungwa mabao 2-0.
Wawakilishi wengine wa Tanzania kwenye michuano ya klabu Afrika, Jumapili hii Januari 25, 2026 wataingia katika viwanja tofauti kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho, Azam wakiwa wageni wa Nairobi United na Singida Black Stars watakuwa wenyeji wa AS Otoho ya Congo Brazzaville.

The post Esperance yailaza Simba 1-0 first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/01/25/esperance-yailaza-simba-1-0/feed/ 0
Chama arudi Simba, aelekea Tunisia https://www.greensports.co.tz/2026/01/24/chama-arudi-simba-aelekea-tunisia/ https://www.greensports.co.tz/2026/01/24/chama-arudi-simba-aelekea-tunisia/#respond Sat, 24 Jan 2026 11:22:18 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14277 Na mwandishi wetuKiungo Mzambia, Clatous Chota Chama amerejea katika klabu yake ya Simba na tayari ameungana na wachezaji wenzake wa timu hiyo walioelekea Tunisia kwa ajili ya mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi.Chama amejiunga na Simba akitokea Singida Black Stars hatua ambayo inamfanya kurudi kwa mara nyingine katika klabu hiyo aliyoichezea kwa […]

The post Chama arudi Simba, aelekea Tunisia first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Kiungo Mzambia, Clatous Chota Chama amerejea katika klabu yake ya Simba na tayari ameungana na wachezaji wenzake wa timu hiyo walioelekea Tunisia kwa ajili ya mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi.
Chama amejiunga na Simba akitokea Singida Black Stars hatua ambayo inamfanya kurudi kwa mara nyingine katika klabu hiyo aliyoichezea kwa mafanikio makubwa kabla ya kuihama.
Chama alijiunga na Simba mwaka 2018 akitokea Lusaka Dynamos ya Zambia na baada ya kutamba akiwa mmoja wa wachezaji tegemeo alisajiliwa na RS Berkane ya Morocco Agosti 2021 lakini mambo hayakwenda vizuri na Januari 2022 alirudi tena Simba.
Uwezo na umahiri wa CHama vilijidhihirisha kwa namna alivyotoa mchango mkubwa kwa Simba kwenye ligi ya Tanzania na Afrika kabla ya kuachana na Simba Julai 2024 na kujiunga na mahasimu wao Yanga.
Alidumu Yanga kwa msimu mmoja kabla ya kutimkia Singida Black Stars Septemba mwaka jana lakini Januari mwaka huu amekuwa habari kubwa baada ya kurudi Simba akitajwa kama mchezaji aliyerudi nyumbani.
Jumamosi hii Januari 24, 2026, Simba itaumana na Esperance ya Tunisa, katika Ligi ya Mabingwa ambapo Chama anatajwa kuziba pengo la Jean Ahoua, kiungo wa Simba aliyeihama timu hiyo hivi karibuni na kujiunga na CR Belouizdad ya Algeria.
Simba ambayo ipo Kundi D katika Ligi ya Mabingwa, mwenendo wake si mzuri katika michuano hiyo kwa msimu huu na kumekuwapo hali ya wasiwasi kwamba huenda timu hiyo ikaishia hatua ya makundi.

The post Chama arudi Simba, aelekea Tunisia first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/01/24/chama-arudi-simba-aelekea-tunisia/feed/ 0
Azam yaiadhibu Simba https://www.greensports.co.tz/2026/01/09/azam-yaiadhibu-simba/ https://www.greensports.co.tz/2026/01/09/azam-yaiadhibu-simba/#respond Fri, 09 Jan 2026 19:34:51 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=14260 Na mwandishi wetuKocha mpya wa Simba, Steve Barker ameonja machungu ya kufungwa mara ya kwanza baada ya timu yake kutolewa kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi kwa kupokea kichapo cha bao 1-0 mbele ya Azam FC.Katika mechi hiyo iliyopigwa Alhamisi Januari 8, 2026, bao pekee lililoizamisha Simba lilifungwa na Lameck Lawi katika dakika ya 73 […]

The post Azam yaiadhibu Simba first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>

Na mwandishi wetu
Kocha mpya wa Simba, Steve Barker ameonja machungu ya kufungwa mara ya kwanza baada ya timu yake kutolewa kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi kwa kupokea kichapo cha bao 1-0 mbele ya Azam FC.
Katika mechi hiyo iliyopigwa Alhamisi Januari 8, 2026, bao pekee lililoizamisha Simba lilifungwa na Lameck Lawi katika dakika ya 73 na kuwaondoa Simba mashindanoni.
Matokeo hayo ni pigo la kwanza kwa Barker ambaye amejiunga na Simba Desemba mwaka jana akitokea Stellenbosch ya Afrika Kusini na hadi sasa tayari ameiongoza timu hiyo katika mechi tatu na kati ya hizo ameshinda mbili.
Wakati Simba ikiaga kwneye Kombe la Mapinduzi, Azam imefuzu hatua ya fainali ya michuano hiyo ya kila mwaka na sasa inasubiri kucheza mechi ya fainali dhiddi ya mshindi wa mechi kati ya Yanga na Singida Black Stars.
Barker amekabidhiwa jukumu la kuinoa Simba baada ya kutimuliwa kwa Dimitar Pantev, bado ana kibarua kingine kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika katika hatua ya makundi pamoja na Ligi Kuu NBC.
Simba sasa inarejea Dar es Salaam ikijiandaa kwa ligi kuu wakati kwenye ligi ya mabingwa itakuwa na kibarua Januari 23 mwaka huu dhidi ya Esperance ya Tunisia.

The post Azam yaiadhibu Simba first appeared on Greensports: Michezo na Burudani.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2026/01/09/azam-yaiadhibu-simba/feed/ 0